Duh, imenikumbusha kuna siku nilikuwa nimeenda kazini. Nyumbani hakuna mtoto wala nini, nimenunua kitu changu cha Samsung 46 inches nimekiweka chumba cha wageni.
Basi katika kufunga miguu ile imekaa kama v za antennae, huku miwili, kule miwili, yote kutoka kati, nikaona kama haijakaa sawa. Kamaimekaaupande hivi.
Nikawa naiweka sawa, naiweka sawa, ikawa kama naharibu zaidi.
Nikasema ngoja niiache, kesho nitaitafutia muda niitengeneze isimame vizuri.
Kesho yake nimeenda kazini, nimerudi home, nakuta kitu kimeanguka chini kwenye zulia.
Nikajua salaaaale, nishakosa TV. Nikainyanyua kuiangaliakama imevunjika, haijavunjika.
Nikasema hii bila shaka haiwaki tena.
He, kuiwasha, inawaka bila chenga wala mawenge.
Mpaka leo ile TV ninayo chumba cha wageni.
Nikaiheshimu sana Samsung katika ku absorb shock. Upande wa juu ulipiga chini, salama yangu kuna zulia halafu hakukuwa na kitu kingine.