Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
JKT yapanga kuitibulia Simba Send to a friend Sunday, 03 April 2011 20:25

Sosthenes Nyoni
NAHODHA wa timu ya JKT Ruvu, Shahibu Nayopa ameiambia Simba wao sio daraja la kuchukulia ubingwa hivyo wajiandae kutibuliwa malengo.Simba na JKT zitakabiliana katika pambano la Ligi Kuu litakalofanyika jijini Dar es Salaam Aprili 6.

Mchezo huo ambao unasubiriwa na wengi unahesabiwa kuwa mtihani wa mwisho kwa Simba yenye pointi 45 kabla kutangazwa ubingwa ili hali ikisubiri kuivaa Majimaji ambayo tayari imeshuka daraja.

Akizunguza na Mwananchi jana, Nayopa alisema kuwa hawatarudia makosa kama yale yaliyowasababisha wakafungwa katika mechi ya mzunguko wa kwanza.

"Sisi si daraja bwana, kama wanafikiri watatangaza ubingwa kwetu watakuwa wanajidanganya tu kwa sababu hata sisi tunataka pointi tatu,"alisema Nayopa.

"Tuliangalia makosa yaliyosababisha tukafungwa katika mpambano wa mzunguko wa kwanza hivyo kila mmoja wetu alilitambua hilo na amelifanyia kazi,"alisema Nayopa.

Alisema kuwa ana uhakika wataibuka kidedea kwa kuwa hata katika mpambano wao wa mzunguko wa kwanza walionyesha kiwango cha hali ya juu, lakini walishindwa kutumia nafasi walizopata tofauti na wenzao.
 
Waziri asifu maonyesho ya Harusi Send to a friend Sunday, 03 April 2011 20:23

Vicky Kimaro
NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Ally Mwalim, jana alipata muda wa kutembelea maonyesho yanayoendelea ya Harusi ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee.

Akizungumza baada ya kutembelea mabanda yote yanayokadiriwa kuwa zaidi ya 50 ya wajasiriamali tofauti wanaojihusisha na masuala ya harusi, Naibu Waziri alimsifu muaandaaji wa maonyesho hayo, mbunifu mahiri wa mavazi nchini, Mustafa Hassanali kuwa ni mjasiriamali anayejituma kuwa ni mfano wa kuigwa.

"Kwa kweli Mustafa amefanya kitu cha kipekee sana, na ni mfano wa kuigwa, hii inawapa wafanyabiashara hususani wale wa mapambo na keki kuweza kujitangaza na kujifunza mengi kutoka kwa wenzao," alisema Waziri Mwalim.

Naibu waziri alipata wasaa wa kubadilishana mawazo na wadau na washiriki wa maonyesho hayo ambao walimpokea kwa furaha huku wakimpa zawadi mbalimbali, aliwasihi na kuwapa moyo wa kuendelea kujituma kwa ari bila kuchoka ili kujipatia kipato na kuwapa huduma wananchi kwa uzuri na usasa zaidi.

Naye muaandaji wa maonyesho hayo Mustafa Hassanali, alisema maonyesho ya mwaka huu wamekuwa na aina yake kutokana na kujipanga kwa timu nzima ya uandaaji, huku baadhi ya mambo yakiwa yameongezeka tofauti na mwaka jana.

Akizungumzia kuhusu muitikio wa watu kutembela maonyesho hayo, Mustafa Hassanali alisema kuwa "kwa mwaka huu, namba ya washiriki imeongezeka zaidi ya ile ya mwaka jana, huku watu wanaokuja kutembelea maonyesho haya pia inaongezeka siku hadi siku, jana walikuwa wachache, na hii ilitokana na kuwa jana ilikuwa ni siku ya kazi, ila leo kwakweli tumepokea watu wengi sana, na bado tunawaomba watu wajitokeze kwa wingi kwa siku ya kesho ambao ndo tunafunga rasmi maonyesho haya."

Hii ni mara ya pili kwa maonyesho haya ya Harusi kufanyika nchini, huku yakiwa na matarajio ya kuishirikisha mikoa mingi zaidi nchini kwa miaka ijayo, tofauti na mwaka huu ambapo mikoa ya Arusha, Zanzibar na Dar es salaam tu ndio iliyoshiriki.
 
Mawaziri wa michezo kushirikiana Send to a friend Sunday, 03 April 2011 20:28

Imani Makongoro
MAWAZIRI wa Michezo wa nchi za Afrika Mashariki wametakiwa kuwa na mawasiliano ya karibu ili kupeana uzoefu wa maandalizi ya timu za nchi hizo zinazotarajiwa kushiriki Fainali za Michezo ya Afrika (All Afrika Games).

Michezo hiyo ambayo inaandaliwa na Umoja wa Afrika (AU) imepangwa kufanyika mapema Septemba mjini Maputo, Msumbiji na kushirikisha wanamichezo mbalimbali kutoka nchi za Bara la Afrika ikiwamo Tanzania.

Akizungumza katika ufunguzi wa mashindano ya Majiji uliofanyika juzi nchini Kampala, Mgeni rasmi katika mashindano hayo Meya wa Manispaa ya Kampala Kati na Rais wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Nchini Uganda (UABF), Godfrey alisema mashindano hayo ni kipimo kizuri kwa mabondia wa nchi hizo.

"Mawaziri wa Michezo wa nchi ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wanatakiwa kuwa na mawasiliano ya karibu ili kufanya pamoja maandalizi ya wanamichezo wao kabla ya kushiriki mashindano makubwa ya kimataifa,"alisema Godfrey.

Alisema, "Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), linatakiwa kuwasiliana na ofisi za Meya katika Majiji yote nchini mwao ili waanze maandalizi ya mashindano ya Majiji mwakani kama ilivyokuwa kwa UABF."

"Sisi tumeweka mikakati mbalimbali kwa mabondia wetu ili
kuiwezesha nchi yetu kufanya vizuri katika mashindano ya Afrika, yaliyopangwa kufanyika Maputo, nchini Msumbiji, Septemba mwaka huu,"alisema Godfrey.

Alisema, "Tumeanza kuandaa timu yetu ambayo tunaamini itafanya vizuri katika mashindano yaliyopo mbele yetu, upo umuhimu mkubwa wa viongozi wa Serikali katika nchi wanachama wa EAC kukaa pamoja ili kupeana uzoefu wa namna ya kuandaa wanamichezo ambao watabeba bendera ya Taifa katika mashindano ya Afrika na mengine ya kimataifa."
 
Rekodi ya Mourinho yavunjwa Send to a friend Sunday, 03 April 2011 20:24

MADRID, Hispania
REKODI ya Jose Mourinho ya kutofungwa nyumbani kwa miaka tisa imehalibika Jumamosi baada ya kuishudia Real Madrid ikipokea kipigo cha kushangaza cha bao 1-0 dhidi ya Sporting Gijon katika ligi ya La Liga.

Mreno huyo mara ya mwisho kushudia timu yake ikifungwa mbele ya mashabiki wake ni wakati Porto ilipofungwa na Beira Mar mwezi Feb. 23, 2002 na baada ya hapo aliweka rekodi ya kutofungwa mechi 150 za ligi akiwa na Porto, Chelsea, Inter Milan na Real.

Gijon ilipata ushindi huo wa kushangaza dakika ya 79, kwenye Uwanja wa Bernabeu wakati Miguel Angel de las Cuevas alipopiga shuti kutokea upande wa kushoto na kumpita kipa Iker Casillas na kutinga wavuni.
Kipigo hicho pia kimetibua rekodi nzuri ya Real nyumbani msimu huu wa La Liga wakiwa wameshinda mechi 14 kwenye Uwanja wake wa Bernabeu.

"Tumepoteza pointi tatu muhimu ambazo hatukustahiri kupoteza," alisema beki wa Madrid, Sergio Ramos.

"Kuna baadhi ya watu hawapo, lakini hiyo haiwezi kuwa sababu. Tulikuwa kwenye hali nzuri, lakini tulishindwa kufunga."

Mshambuliaji wa Argentina, Gonzalo Higuain aliyekuwa nje ya uwanja tangu mwezi Novemba ni mchezaji pekee aliyeonyesha kiwango cha juu kwa Real, wanaojiandaa na mechi yao ya Ligi ya Mabingwa hapo kesho dhidi ya Tottenham Hotspur kwenye Uwanja wa Bernabeu.

Madrid ilicheza mchezo huo bila ya Cristiano Ronaldo, Karim Benzema na Marcelo wanaosumbuliwa na majeruhi pamoja na kiungo wa Hispania, Xabi Alonso aliyefungiwa.
 
Kidunda achapwa Kampala Send to a friend Sunday, 03 April 2011 20:27

Imani Makongoro
BONDIA wa timu ya Taifa ya ngumi za ridhaa, Selemani Kidunda, juzi alikung'utwa kwa pointi 3-2 na bondia wa Kampala A, Nyeko Godfrey katika mashindano ya majiji.

Mashindano hayo yameanza kutimua vumbi Ijumaa kwenye ukumbi wa Hoteli ya Lake Victoria Resort Munyonyo
iliyopo katikati ya Jiji la Kampala nchini Uganda.

Habari zilizoifikia Mwananchi kutoka Uganda zilieleza kuwa Pambano la Kidunda lilikuwa na utata
mkubwa baada ya matokeo kutangazwa.

Habari hizo zilifafanua kuwa katika pambano hilo mpinzani wa Kidunda aliangushwa chini mara mbili na Kidunda aliangushwa mara moja, lakini matokeo yalipotangazwa yalikuwa tofauti na matarajio ya mashabiki ukumbini hapo.

"Matokeo ya Kidunda yaliwashangaza watu wengi hata Waganda wenyewe kwani waliamini Kidunda ameshinda kutokana na ngumi nyingi alizompiga mpinzani wake ambaye muda mwingi alikuwa akizuia mashambulizi," kilieleza chanzo hicho.

Kwa upande wa mabondia wengine wa Tanzania, Victor Njaiti atazichapa na Hakizimana Ngarma wa Burundi, katika pambano la uzito wa Welter kg 64, wakati Yahaya Maliki, atasubiri mshindi kati ya bondia Emili Bigilimana wa Burundi na Semitara Rogers wa Kampala B pambano la uzito wa Fly kg. 52.
 
Suluhisho ya Dede yawakuna wengi


na Juma Kasesa


amka2.gif
WIMBO mpya wa mtunzi na mwimbaji wa bendi ya Msondo Ngoma Shabani Dede, ‘Mzee wa Loliondo' unaokwenda kwa jina la ‘Suluhisho' umeonekana kuwakuna wapenzi wa muziki wa dansi kutokana na ubora wa mashairi yaliyomo ndani yake.
Wakizungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam, mashabiki wa muziki wa dansi, waliokuwa wamefurika katika ukumbi wa TCC Chang'ombe Temeke, wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza, walisema mashairi yaliyomo ndani ya wimbo huo, yamedhihirisha uwezo wa kutunga alionao Dede.
Walisema, wimbo huo ambao ni kama jibu la kibao kingine alichowahi kutunga akiwa Sikinde, kinachokwenda kwa jina la ‘Talaka Rejea', umezidi kumuongezea chati na kuwakumbusha uwezo aliokuwanao mwanamuziki kipenzi wa bendi hiyo, hayati Ally Mhoja Kishiwa ‘TX Moshi William', ambaye Machi 29 mwaka huu alitimiza miaka mitano ya kifo chake.
Aidha, mashabiki hao walisema, wanaamini Dede atakuwa na msaada mkubwa katika kuienzi Msondo, kwa kushirikiana na wanamuziki waliopo sasa, ili iweze kurudi katika enzi za miaka ya 1980 ilipokuwa ikiwika sana kutokana na ubora wa mashairi na uwezo wa waimbaji ambao wengi wao wamefariki dunia.
 
Extra Bongo kusaka wengine wanne


na Juma Kasesa


amka2.gif
BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo Next Level, ‘Wazee wa Kizigo' imeanza mchakato wa kusaka wanamuziki wengine wanne wapya kwa lengo la kuzidi kujiimarisha na ushindani wa muziki uliopo hivi sasa hapa nchini.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa bendi hiyo, Ally Choki, mchakato huo utahusisha wanamuziki chipukizi na wazoefu kutoka bendi mbalimbali zinazowika.
Alisema tayari wameishaona nyota kadhaa kutoka katika bendi hizo na hatua inayofuata ni kuanza mazungumzo ya kuwasainisha mikataba, ili kuanza kuitumikia Extra Bongo, ambayo kwa sasa inatamba na nyimbo zake mbili mpya zinazokwenda kwa jina la ‘Mtenda Akitendewa' na ‘Neema'.
Hivi karibuni, bendi hiyo ilifanikiwa kunyakua wanamuziki kutoka bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta', ambao ni mtunzi na mwimbaji mahiri Rogert Hega ‘Katapila', Saulo John ‘Ferguson', Hosea, Hassan Nyamwela na mnenguaji Otilia Boniface.
 
Twins Records kufunguliwa Dar leo


na Abdallah Menssah


amka2.gif
KAMPUNI inayojihusisha na ukuzaji vipaji vya wasanii nchini, Twins Art Production kesho inatarajia kufungua studio ya kurekodi muziki itakayojulikana kama ‘Twins Records'.
Meneja Mkuu wa Twins Art, Daud Juma Mwandalima, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa studio hiyo itakuwa ikirekodi kazi mbalimbali za wasanii wa muziki.
Aidha, Mwandalima alieleza kuwa, studio hiyo ambayo itakuwa chini ya Mkurugenzi Mkuu wake, Vick Kanyoka, vile vile itakuwa ikiandaa matamasha pamoja na kuwasaidia wasanii walio katika mazingira magumu.
"Pia tutakuwa na kikundi cha wasanii mahiri, ambao kazi yao itakuwa ni kurekodi matangazo ya kibiashara kwenye kampuni mbalimbali tutakazokubaliana nazo, ndani na nje ya nchi," alisema Mwandalima.
Kwa mujibu wa Mwandalima, studio hiyo yenye kusheheni vifaa vya kisasa vya kurekodia, itakuwa maeneo ya Ubungo River Side, karibu na Hoteli ya Land Mark.
 
Simba vs. Mazembe leo: Ni tambo tupu
• TP: Tumekuja na kikosi cha maangamizi

na Dina Ismail


amka2.gif
WAKATI leo zinashuka kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam kukwaana katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, timu za Simba na TP Mazembe kila moja imejitapa kutoka kifua mbele.
Wakizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jana, viongozi wa timu hizo, kila mmoja aliahidi timu yake kuibuka na ushindi katika mechi ya leo.
Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia Patrick Phiri, alisema kwamba amekiandaa vema kikosi chake na hasa kurekebisha makosa yaliyojitokeza katika mechi ya awali, hivyo ana uhakika watatoka kifua mbele.
Alisema, anajisikia fahari kucheza na vinara wa soka mara mbili mfululizo barani Afrika, lakini hilo haliwatii hofu wachezaji wake kucheza vema na hatimaye kushinda mechi hiyo.
"Mazembe ni kama walimu wa soka Afrika, wamekuja kutufunza soka...lakini hiyo si sababu ya kutufanya tupoteze mechi yetu, naamini tutashinda na kuweka historia," alisema Phiri.
Kocha huyo aliongeza kuwa wachezaji wake wako katika hali nzuri ya mchezo huo, ambao kwa namna moja au nyingine ni lazima washinde ili kusonga mbele.
Naye Meneja wa TP Mazembe, Tzediric Kitenge alisema kuwa wamekuja na kikosi cha maangamizi, hivyo ni lazima waibuke na ushindi.
Alisema bao pekee walilolipata Simba katika mechi yao ya awali iliyochezwa katika Jiji la Lubumbashi si kigezo kuwa wataweza kuwafunga mabao zaidi na kuwatoa katika michuano hiyo.
Katika hatua nyingine, Kitenge alikana tuhuma dhidi ya timu yao kudaiwa kutaka kutoa rushwa kwa waamuzi katika mechi yao ya awali na Simba na kudai kuwa zina lengo la kuwaharibia.
"Kama kuna kitu hicho, mtu aje na kuthibitisha, timu yetu ni nzuri na imewahi kuzifunga mabao mengi timu kubwa ikiwemo Esperance (Tunisia), na nyinginezo, hiyo ni katika kupakana matope," alisema.
Naye mshambuliaji wa Simba, Mussa Hassan Mgosi, alisema wako vizuri kimchezo na leo lazima historia ya mwaka 2003 ijirudie.
Ili kusonga mbele, Simba inahitaji kushinda mabao 2-0, kwani katika mechi ya awali ugenini walilala 3-1.
Iwapo Simba itashinda mechi ya leo, itaweka historia ya mwaka 2003 walipoivua ubingwa Zamalek ya Misri.
 
Mo, Friends of Simba waahidi mil. 100/- tena


na Dina Ismail


amka2.gif
MBUNGE wa Singida Mjini, Mohammed Dewji ‘Mo', pamoja na kundi la Marafiki wa Simba, ‘Friends of Simba' wameahidi dau la sh milioni 100 iwapo Wekundu hao wa Msimbazi watafanikiwa kuiondosha TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), leo.
Simba na TP Mazembe wanakwaana leo kuanzia majira ya saa 9:30 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, ambapo Mo na Friends of Simba kila mmoja ameahidi kuwapa wachezaji sh milioni 50. Mechi ya awali waliahidiwa wakishinda sh milioni 100 na wakienda sare milioni 50.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Dewji, ambaye aliwahi kuwa mfadhili wa klabu hiyo, alisema ana imani Simba itashinda mechi hiyo kutokana na ubora walionao.
Alisema wachezaji wa Simba wana kiwango kikubwa cha soka, hivyo kama wataondoa hofu ya kuwa wanacheza na timu fulani (TP Mazembe), uwezekano wa kushinda ni mkubwa.
"Kama waliweza kuwavua ubingwa wa Afrika Zamalek, kwa nini washindwe kwa Mazembe, kwani wachezaji wao ni wa kawaida kabisa," alisema Mo.
Aidha, mbunge huyo ambaye pia ni mmiliki wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL), aliitakia kila la heri Simba na kuwaomba Watanzania kuiombea dua, sambamba na kujitokeza kwa wingi kwenda kuishangilia.
 
Judo Zanzibar kuwasili nchini leo


na Stella Mushi


amka2.gif
WACHEZAJI wanne wa judo Zanzibar wanatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ndege ya Misri ‘Egypt Air' wakitokea nchini Japan walikokwenda kwa mafunzo ya mchezo huo.
Kwa mujibu wa Rais wa Chama cha Judo Zanzibar (ZJA), Tsuyoshi Shimaoka, wachezaji hao watawasili Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere alfajiri ya Aprili 4 saa 11:20 na watapumzika kwa muda katika Hoteli ya Kibodia karibu na Mnara wa Saa, Mtaa wa Nkurumah jijini kwa ajili ya mahojiano na waandishi wa habari.
Shimaoka alisema timu hiyo iliondoka jijini Dar es Salaam Januari 3 ambapo wakiwa nchini humo walijifua kwa takriban miezi mitatu katika eneo la Juba, ambapo wamepata uzoefu wa kutosha sambamba na kuongeza kiwango cha mbinu za kimataifa, ikiwa ni moja ya maandalizi ya michezo ya Afrika ‘All African Games' itakayoanza kutimua vumbi Septemba mwaka huu nchini Msumbiji.
"Japokuwa kulikuwa na matetemeko na sunami nchini Japan, tuliendelea na judo kila siku katika Chuo Kikuu cha Juntendo, pia tulienda kujifunza maeneo mbalimbali na kucheza na wachezaji wa aina mbalimbali wa judo wa Japan," alisema Shimaoka.
Shimaoka alisema mara baada ya kuwasilia Dar es Salaam, mahojiano hayo yatafanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 3:00 asubuhi, ambapo baada ya shughuli hiyo msafara huo utaelekea visiwani Zanzibar kwa boti.
Rais huyo wa judo Zanzibar, aliwataja wachezaji hao kuwa ni pamoja na nahodha Lawa Shauri Henry, Abdallah Abdulsamad Alawi, Khamis Azzan Hussein na Abeid Omar Dola.
 
Lescott hails 'dominant' City


RivalsDM



PRINT RSS

1

Updated Apr 3, 2011 2:15 PM ET
Joleon Lescott acknowledged the quality of Manchester City's performance after Sunday's 5-0 drubbing of Sunderland in the Premier League.
Adam Johnson, Carlos Tevez, David Silva, Patrick Vieira and Yaya Toure got the goals as Roberto Mancini's men romped to victory at Eastlands.
And City defender Lescott told Sky Sports: "We dominated from start to finish.

Sat., Apr. 2
West Ham 2-4 Man Utd | Recap
Birmingham 2-1 Bolton | Recap
Everton 2-2 Aston Villa | Recap
Newcastle 4-1 Wolves | Recap
Stoke City 1-1 Chelsea | Recap
West Brom 2-1 Liverpool | Recap
Wigan 0-0 Tottenham | Recap
Arsenal 0-0 Blackburn | Recap
Sun., Apr. 3
Fulham 3-0 Blackpool | Recap
Man City 5-0 Sunderland | Recap
BPL Scores | Table | Fixtures


"You can't ask for that level of performance every week...it's nice to get results - and today we got the result as well as the performance."
Team-mate Nigel de Jong said: "Our main goal at the start of the season was to qualify for the Champions League and that's still our main target, so it was a helpful three points today.
"There are still seven games to go and anything can happen but this is a great confidence boost for our team - we are real contenders for the Champions League places."
Mancini was pleased with a win which moves his FA Cup semi-finalists up to third in the Premier League table, a point clear of Chelsea.
He said : "I think we played very well. We started well and pressed from the first minute."
The Italian believes his team's league form is benefiting from fewer fixtures.
He explained: "In the last 45 days we've played every three days and we've had more player injuries. That was the problem.
"Now all the players have recovered and we play Saturday-Saturday we don't have a problem.
"We hope we continue to play very well like today - but sometimes it depends on the opponents."
Sunderland manager Steve Bruce said: "We were certainly nowhere near good enough - we were second best all afternoon all over the pitch.
"You can say Manchester City were very, very good but in a lot of positions we were nowhere near where we should be and we've certainly got to do better than we were today.
"We responded when we had a setback at Newcastle a few months ago and we've got to do the same thing again.
"The performance disappointed me more than it surprised me but I don't want to make excuses - we were simply second best in every department. We got our backsides well and truly kicked."
Asked if the sale of striker Darren Bent to Aston Villa has halted the progress of a team who have picked up just one point from their last seven games, Bruce added on Sky Sports: "You can look at all sorts of stuff.
"Statistically, when you look at it, of course - but it's no good looking at what's happened in the past.
"We've got to pull our socks up and look forward to the challenge of the last seven games."
 
Van Persie retains title hope


RivalsDM



PRINT RSS

0

Updated Apr 4, 2011 6:43 AM ET
Robin van Persie retains the belief that Arsenal can still win the Premier League and hopes the Champions League will affect Manchester United.
Arsenal's title destiny is now out of their own hands following the 0-0 home draw with Blackburn Rovers on Saturday which left Arsene Wenger's side seven points adrift of United.


The Gunners do have a game in hand, and still have to welcome United to Emirates Stadium in May, to leave van Persie clinging to hope.
United also meet domestic rivals Chelsea in the Champions League quarter-finals and van Persie is keen for Arsenal to take advantage of any tiredness in the Red Devils camp.
"The way I look at it is that United have two extra big games before they have to play us," said van Persie.
"Hopefully they will have to dig deep into their reserves and come here tired. That's how I am looking at it because I want us to have the biggest chance against them.
"We start working hard on Monday again and everyone will be positive.
"We cannot be different. We do believe.
"We still play them and we have a chance to get three points there.
"It's up to us. Everyone stays positive and speaks to each other and says 'Come on, we've eight games to play for, give it your all'. We will do that."
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom