Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,508
- 911,249
- Thread starter
- #13,741
Timu ya Wawakilishi yapigwa jeki
Imeandikwa na Nafisa Madai, Maelezo Zanzibar; Tarehe: 28th March 2011 @ 23:00 Imesomwa na watu: 26; Jumla ya maoni: 0
TIMU ya Soka ya Baraza la Wawakilishi imekabidhiwa vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya michezo ya Pasaka.
Akikabidhi vifaa hivyo, Meneja wa timu hiyo, Omar Yussuf Mzee ameitaka kuhakikisha inakuwa bingwa wa mashindano ya Pasaka, Tamasha litakalofanyika mjini hapa mwezi ujao.
Mzee alisema timu hiyo inaundwa na wachezaji makini, anaamini wanaweza kutoa ushindani mkubwa katika tamasha hilo akimtaja mmojawapo kuwa Hamza Hassan Juma ambaye ni miongoni mwa washambuliaji mahiri wa kikosi hicho.
Vifaa alivyokabidhi Meneja huyo ni jezi, jozi za soksi, mipira ambapo vifaa hivyo ni sehemu ya maandalizi ya mashindano mbalimbali na kuwaomba wahisani wengine kusaidia timu hiyo inayoundwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao kwa sasa wanajiandaa na mechi za kirafiki.
Meneja Msaidizi wa timu hiyo, Nassor Salum Ali, ametamba timu yake itaibuka na ushindi dhidi ya timu ya Exim Bank, ambapo aliwataka mashabiki wa soka kujitokeza kuiunga mkono timu hiyo.
Naye Mwenyekiti wa timu hiyo, Hamza Hassan Juma, aliwapongeza viongozi waliotoa msaada huo kwani umetolewa wakati muafaka katika kipindi ambacho timu hiyo inakabiliwa na mashindano mbalimbali.
Kwa upande wake Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo , Abdillah Jihadi Hassan ameshauri wajumbe wa Baraza kuendeleza mazoezi kwa ajili ya mashindano mbalimbali.
Imeandikwa na Nafisa Madai, Maelezo Zanzibar; Tarehe: 28th March 2011 @ 23:00 Imesomwa na watu: 26; Jumla ya maoni: 0
TIMU ya Soka ya Baraza la Wawakilishi imekabidhiwa vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya michezo ya Pasaka.
Akikabidhi vifaa hivyo, Meneja wa timu hiyo, Omar Yussuf Mzee ameitaka kuhakikisha inakuwa bingwa wa mashindano ya Pasaka, Tamasha litakalofanyika mjini hapa mwezi ujao.
Mzee alisema timu hiyo inaundwa na wachezaji makini, anaamini wanaweza kutoa ushindani mkubwa katika tamasha hilo akimtaja mmojawapo kuwa Hamza Hassan Juma ambaye ni miongoni mwa washambuliaji mahiri wa kikosi hicho.
Vifaa alivyokabidhi Meneja huyo ni jezi, jozi za soksi, mipira ambapo vifaa hivyo ni sehemu ya maandalizi ya mashindano mbalimbali na kuwaomba wahisani wengine kusaidia timu hiyo inayoundwa na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao kwa sasa wanajiandaa na mechi za kirafiki.
Meneja Msaidizi wa timu hiyo, Nassor Salum Ali, ametamba timu yake itaibuka na ushindi dhidi ya timu ya Exim Bank, ambapo aliwataka mashabiki wa soka kujitokeza kuiunga mkono timu hiyo.
Naye Mwenyekiti wa timu hiyo, Hamza Hassan Juma, aliwapongeza viongozi waliotoa msaada huo kwani umetolewa wakati muafaka katika kipindi ambacho timu hiyo inakabiliwa na mashindano mbalimbali.
Kwa upande wake Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo , Abdillah Jihadi Hassan ameshauri wajumbe wa Baraza kuendeleza mazoezi kwa ajili ya mashindano mbalimbali.
PRINT