Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,508
- 911,249
- Thread starter
- #13,661
Mosha arejeshwa Yanga kwa kishindo
• Wanachama wamchomoa nyumbani kwake
na Mwandishi wetu
UNAWEZA usiamini, lakini ndio ukweli wenyewe kwamba kundi la wanachama wa klabu ya Yanga, jana waliamua kukata mzizi wa fitna kwa kumwendea Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Davis Mosha, na kumsihi abatilishe uamuzi wake wa kujiuzulu kwenye nafasi hiyo.
Walichofanya wanachama wa matawi yapatayo 11 kutoka mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, ni kufunga msafara wa Coaster nne, Hiace mbili, bajaji na magari binafsi, na kuvamia nyumbani kwa Mosha maeneo ya Mikocheni kwa lengo moja la kumsihi arejee madarakani kwa hoja ya maslahi ya klabu hiyo kwa sababu ndiye mwenye uwezo wa kuiongoza Yanga.
Wakiwa katika msururu huo, wanachama hao walipofika kwa Mosha na kueleza kilichowapeleka, Mosha alionekana kuwa mgumu kwa hoja kuwa alijiuzulu kutokana na hali halisi iliyoko Yanga hasa baada ya kushauriana na familia yake.
Baada ya mazungumzo marefu, wanachama hao walimuomba aambatane na wao hadi makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, jijini Dar es Salaam kwa majadiliano zaidi kwa maslahi ya Yanga.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wanachama hao walisema wameona Yanga inayumba baada ya kujiuzulu kwake, hivyo hana budi kurejea ili kuinusuru klabu hiyo.
Wakienda mbali zaidi, wanachama hao walidai kuwa licha ya mwenyekiti wao Lloyd Nchunga kudai hawezi kufanya kazi pamoja na Mosha, uchunguzi wao umebaini kuwa mwenyekiti ndiye chanzo cha msigano baina yao kwa sababu amekuwa akifumbia macho vitendo vya kihuni anavyofanyiwa Mosha.
"Sisi tuko nyuma yako na ndiyo maana tulikupa kura nyingi kuliko kiongozi yeyote katika uchaguzi, hivyo tunakuamini na tunakuomba urejee kukataa kwako kutafanya Yanga ikose asilimia 85 ya wanachama ambao ndio tumekuchagua," alisema mmoja ya wanachama Saidi Bakari (0035).
Kwa upande wake Mosha alisema kuwa aliamua kujiuzulu kutokana na sababu tofauti ikiwamo kutishiwa maisha, ukiukwaji wa katiba, sambamba na kufanyiwa fujo na baadhi ya wanachama hali ambayo aliona inamshushia hadhi yake aliyonayo katika jamii.
"Nimewasikia na nitaendelea kuwa pamoja nanyi kwani mimi ni mwanachama halali lakini nilitoka baada ya kuona hali si nzuri ili kulinda heshima yangu, hata hivyo mnatakiwa mkazungumze na Kamati ya Utendaji iitishe Mkutano Mkuu," alisema Mosha.
Mosha aliongeza kuwa kuna baadhi ya viongozi ambao wameingia Yanga kwa ajili ya kujipatia maslahi yao na wamekuwa wakiwatuma baadhi ya watu kumletea vurugu, lakini yeye amekwenda Yanga kwa ajili ya kuisaidia na si kuvuna.
"Mimi nimeingia Yanga kwa ajili ya kuisaidia wala si kuvuna, uongozi si elimu bali kipaji na mimi kipaji hicho ninacho, Yanga si sehemu yangu ya kwanza kuongoza lakini nimekuwa nikisikitishwa na mwenendo wa baadhi ya viongozi wenzangu dhidi yangu," alisema.
Baada ya kutoa dukuduku lake hilo Mosha aliongozana na msafara wa wanachama hao mpaka makao makuu ya klabu hiyo ambako baada ya kusikiliza tena maombi ya wanachama, aliamua kuendelea kuingoza Yanga.
• Wanachama wamchomoa nyumbani kwake
na Mwandishi wetu
Walichofanya wanachama wa matawi yapatayo 11 kutoka mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, ni kufunga msafara wa Coaster nne, Hiace mbili, bajaji na magari binafsi, na kuvamia nyumbani kwa Mosha maeneo ya Mikocheni kwa lengo moja la kumsihi arejee madarakani kwa hoja ya maslahi ya klabu hiyo kwa sababu ndiye mwenye uwezo wa kuiongoza Yanga.
Wakiwa katika msururu huo, wanachama hao walipofika kwa Mosha na kueleza kilichowapeleka, Mosha alionekana kuwa mgumu kwa hoja kuwa alijiuzulu kutokana na hali halisi iliyoko Yanga hasa baada ya kushauriana na familia yake.
Baada ya mazungumzo marefu, wanachama hao walimuomba aambatane na wao hadi makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, jijini Dar es Salaam kwa majadiliano zaidi kwa maslahi ya Yanga.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wanachama hao walisema wameona Yanga inayumba baada ya kujiuzulu kwake, hivyo hana budi kurejea ili kuinusuru klabu hiyo.
Wakienda mbali zaidi, wanachama hao walidai kuwa licha ya mwenyekiti wao Lloyd Nchunga kudai hawezi kufanya kazi pamoja na Mosha, uchunguzi wao umebaini kuwa mwenyekiti ndiye chanzo cha msigano baina yao kwa sababu amekuwa akifumbia macho vitendo vya kihuni anavyofanyiwa Mosha.
"Sisi tuko nyuma yako na ndiyo maana tulikupa kura nyingi kuliko kiongozi yeyote katika uchaguzi, hivyo tunakuamini na tunakuomba urejee kukataa kwako kutafanya Yanga ikose asilimia 85 ya wanachama ambao ndio tumekuchagua," alisema mmoja ya wanachama Saidi Bakari (0035).
Kwa upande wake Mosha alisema kuwa aliamua kujiuzulu kutokana na sababu tofauti ikiwamo kutishiwa maisha, ukiukwaji wa katiba, sambamba na kufanyiwa fujo na baadhi ya wanachama hali ambayo aliona inamshushia hadhi yake aliyonayo katika jamii.
"Nimewasikia na nitaendelea kuwa pamoja nanyi kwani mimi ni mwanachama halali lakini nilitoka baada ya kuona hali si nzuri ili kulinda heshima yangu, hata hivyo mnatakiwa mkazungumze na Kamati ya Utendaji iitishe Mkutano Mkuu," alisema Mosha.
Mosha aliongeza kuwa kuna baadhi ya viongozi ambao wameingia Yanga kwa ajili ya kujipatia maslahi yao na wamekuwa wakiwatuma baadhi ya watu kumletea vurugu, lakini yeye amekwenda Yanga kwa ajili ya kuisaidia na si kuvuna.
"Mimi nimeingia Yanga kwa ajili ya kuisaidia wala si kuvuna, uongozi si elimu bali kipaji na mimi kipaji hicho ninacho, Yanga si sehemu yangu ya kwanza kuongoza lakini nimekuwa nikisikitishwa na mwenendo wa baadhi ya viongozi wenzangu dhidi yangu," alisema.
Baada ya kutoa dukuduku lake hilo Mosha aliongozana na msafara wa wanachama hao mpaka makao makuu ya klabu hiyo ambako baada ya kusikiliza tena maombi ya wanachama, aliamua kuendelea kuingoza Yanga.