Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Mapato Stars, Afrika ya Kati kwenda Gongo la Mboto Send to a friend Saturday, 19 March 2011 11:46

wamburatff.jpg
Ofisa habari wa TFF, Boniface Wambura

Calvin KiwiaSHIRIKISHO la soka Tanzania (tff) limedhamiria kutoa asilimia moja ya mapato ya mchezo wa kimataifa waTaifa Stars dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati mwezi huu kusaidia waathirika wa mabomu wa Gongo la Mboto.

Mchezo huo wa kutafuta tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika mwaka 2012 nchini Gabon na Guinea ya Ikweta utachezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Machi 26 mwaka huu.

Ofisa habari wa shirikisho hilo, Boniface Wambura alisema jana wakati akitangaza viingilio vya mchezo huo kuwa timu hiyo tayari imeanza maandalizi ya kuikabili Afrika ya Kati, kinara wa Kundi D ikiwa chini ya kocha Jan Poulsen.

"Tumepanga viingilio vya mechi hiyo viwe; VIP A Sh 40,000. VIP B Sh 20,000 na VIP C Sh 10,000.'

" Viti vya rangi ya kijani na bluu ni Sh 3,000. na vyenye rangi ya machungwa (orange) ni Sh 5,000 na tiketi hizo zitaanza kuuzwa Machi 24,' alisema Wambura.

Alivitaja vituo ambavyo vitatumika kuuza tiketi hizo kuwa ni; Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Big Bon (Kariakoo), Steers Samora/Ohio, Oil Com (Ubungo), Uwanja wa Uhuru, Kobil Buguruni na Polisi Tandika.

Alisema mpaka sasa hawajafahamu kuwa timu hiyo itafika lini nchini , lakini bado wanaendelea kufanya nao mawasiliano kujua itawasili siku gani.

'Utaratimu wa mawasilano bado unaendelea kati yetu na shirikisho la soka la huko (Afrika ya Kati) kufahamu watawasili lini nchini," alisema Wambura na kuongeza kuwa wakiwa nchini wageni hao wataishi kwenye hoteli ya Tansoma, Gerezani jijini Dar es Salaam.
 
Vita ya karne Chelsea v Man United Send to a friend Saturday, 19 March 2011 11:43

NYON, Uswisi
CHELSEA imepangwa kuchuana na Manchester United, zote za England katika mchezo wa robo fainali wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na ambao unaamsha hisia ya fainali ya ligi hiyo mjini Moscow, Russia mwaka 2008.

Katika fainali hiyo, Man United iliilaza Chelsea kwa mikwaju ya penalti baada ya suluhu baina ya timu hizo na kutwaa ubingwa kwa mara ya tatu katika historia yake huku beki na nahodha John Terry akikosa bao muhimu.

Kitu kikubwa zaidi ni kwa timu hizo kukutana tena katika mchezo mwingine baada ya mwezi uliopita Chelsea ilipoilaza Man United kwa mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu England na kuzusha lawama kutoka kwa kocha Alex Ferguson.

Mchezo huo, hadi sasa umekuwa mwiba kwa Ferguson baada ya kufungiwa mechi tano na Chama cha Soka (FA) kutokana na kumkashifu mwamuzi Martin Atkinson aliyechezesha mchezo huo kwamba aliwapendelea wenyeji.

Kauli hiyo ilimsababisha Ferguson kufungiwa na FA mechi tano, adhabu ambayo inaanza leo kwenye mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Bolton na itaendelea hadi Mei Mosi mwaka huu wakati wakicheza na Arsenal kwenye Uwanja wa Emirates jijini London.

Kulingana na Shirikisho la Soka Ulaya, Uefa, Real Madrid v Tottenham zitacheza Aprili 5, Chelsea v Manchester United zikiuamana Jumatano, Aprili 6.

Katika ratiba hiyo,Real Madrid ambao wameingia robo fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2004, wamepangiwa vijana wa Tottenham Hotspur ya England chini ya Harry Redknapp, ambao wameshangaza wengi kwa kufuzu kwa mara ya kwanza kucheza hatua hiyo tangu msimu wa 1961/62 na ambao mwaka mmoja na nusu uliopita, pia walikuwa mkiani mwa Ligi Kuu.

Kivutio kingine cha ratiba hiyo ya Uefa ni uwezekano wa Real Madrid na Barcelona ambayo imepangiwa Shakhtar Donetsk ya Ukraine kukutana katika nusu fainali mwezi Aprili, endapo zitamudu kuwatoa wapinzani wao.

Mechi nyingine ya robo fainali hiyo itakuwa baina ya Internazionale (Italia) v Schalke 04 kutoka Ujerumani

Wakati timu hizo zikiwa zimefuzu kucheza hatua hiyo, wafuatao ndio vinara wa mabao :

Barcelona- Lionel Messi (8) Spurs- Gareth Bale, Peter Crouch (4), Schalke 04- Jefferson Farfán (4), Shakhtar Donetsk -Eduardo, Luiz Adriano (4), Internazionale - Samuel Eto'o (8), Man United- Javier Hernández (3), Chelsea- Nicolas Anelka (7) na Real Madrid - Karim Benzema (6)
 
JB: Umakini unanibeba kwa mashabiki


na Abdallah Menssah


amka2.gif
MKALI wa sanaa ya filamu hapa nchini, Jacob Stephen ‘JB' ameeleza kuwa umakini katika fani hiyo ndiyo siri pekee inayomfanya akubalike na kuvuta mashabiki wengi kila anapofyatua kazi mpya.
JB, kati ya waigizaji nguli, mwenye makeke na vibweka vingi anapokuwa kazini, aliyasema hayo jana, katika mazungumzo maalumu na mwandishi wa habari hizi yaliyofanyika Sinza, jijini Dar es Salaam.
"Unajua, ukitaka kufanya vema katika kazi zako, lazima kwanza katika maandalizi uweke mbele matakwa ya mashabiki, pamoja na wapenzi wako na si kukurupuka kutayarisha kazi kwa utashi wa mapendekezo yako binafsi," alisema JB.
Alisema amejiwekea mkakati wa kuandaa filamu zilizoko katika mtindo wa kuchekesha ili kuvuta hisia za wengi zaidi, kwani mashabiki hawapendi kuchoshwa kwa kuangalia filamu isiyochanganyika na ucheshi hata kidogo.
 
Mashabiki watofautiana kuhama kwa Dede


na Mwandishi wetu


amka2.gif
MASHABIKI wa dansi hapa nchini wamekuwa na maoni tofauti juu ya hatua ya mwimbaji mahiri, Shaaban Dede, kurejea tena katika bendi ya Msondo Ngoma Music.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, mashabiki hao walisema, Dede amewafanyia Sikinde kitu ambacho hawatakisahau kwa urahisi.
"Unajua, pia Dede amejitia aibu mwenyewe, kwa sababu Msondo alikorudi sasa ndiko kule alikofukuzwa mara mbili huko nyuma," alisema shabiki aliyejitambulisha kwa jina la Jerry Wammy.
Shabiki mwingine aliyefahamika kwa jina la Kassim Juma alieleza kuwa kwa kitendo hicho, thamani ya Dede itapungua na kushuka mbele ya mashabiki pamoja na wapenzi wake.
 
Milioni 100/- Simba wakiiua Mazembe leo


na Mwandishi wetu


amka2.gif
MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Simba, iliondoka nchini jana asubuhi kwa ndege na kuwasili salama Lubumbashi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), tayari kuwakabili TP Mazembe huku ikiwa imeahidiwa donge nono endapo itaibuka na ushindi au kwenda sare.
Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu, kundi maarufu la marafiki wa Simba ‘Friends of Simba' limetoa ofa ya sh milioni 100 endapo Simba itashinda huku ikienda sare watazawadiwa sh milioni 50, katika mechi ya leo itakayopigwa dimba la Kenya mjini Lubumbashi.
Wekundu hao wa Msimbazi waliwasili nchini humo wakiwa na morali wa hali ya juu kuwakabili ipasavyo mabingwa hao watetezi, katika pambano litakalopigwa leo kwenye Uwanja wa Kenya mjini humo na kuzua hofu kwa wenyeji.
Kutokana na Mazembe kuwa na hofu ya pambano hilo, naye Rais wake, Mosea Katumbi Chapwe amewaahidi dola 50,000 za Marekani vijana wake endapo wataibuka na ushindi katika mechi ya leo.
Hofu ya Mazembe kwa Simba inatokana na rekodi ya Wekundu hao wa Msimbazi kuwavua ubingwa Zamalek ya Misri mwaka 2003, hivyo wako makini historia isije kujirudia.
Simba inatarajia kupata sapoti ya Watanzania kadhaa kutoka miji ya jirani na wale madereva wa magari makubwa, huku pia wanazi wa FC Lupopo nao wakiahidi kuwa upande wa Wekundu wa Msimbazi, leo katika mechi hiyo inayatabiriwa kuwa ngumu.
Desemba mwaka jana, TP Mazembe chini ya Kocha wake Lamine N'Diaye iliweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza Afrika kufika hatua ya fainali ya mabingwa wa mabara kwa klabu kabla ya kufungwa na Inter Milan chini ya Kocha Rafael Benitez katika mechi ya fainali iliyochezwa Desemba 18, mwaka jana.
Kikosi cha Simba kilichotua Lubumbashi jana chini ya Mwenyekiti wake, Alhaj Ismail Aden Rage, kiko na Juma Kaseja, Ally Mustapha ‘Barthez', Juma Nyoso, Meshack Abel, Kelvin Yondan, Juma Jabu ‘JJ', Amri Kiemba, Amiri Maftah, Patrick Ochan, Haruna Shamte, Jerry Santo na Nicco Nyagawa.
Wengine ni Emmanuel Okwi, Mussa Hassan Mgosi, Mbwana Samatta, Ally Ahmed Shiboli, Rashid Gumbo na Shija Mkina.
Wakati huo huo, Mwandishi Wetu, Asha Bani anaripoti kuwa, Chama cha Wananchi (CUF), kimeungana na Watanzania wote, hususan wapenda michezo, kuwatakia kila la heri mabingwa hao wa soka nchini waibuke na ushindi katika mechi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba, inawataka Watanzania kuungana kwa pamoja ili kuipa nguvu timu hiyo.
"CUF kwa pamoja licha ya kuutambua uwezo walionao TP Mazembe, ambapo ndiyo timu ya kwanza katika Afrika kufika fainali za Klabu Bingwa ya Dunia na kutolewa na Inter Milan ya Italia, lakini tunawataka wachezaji wa Simba kutokuogopa uwezo huo na kuona ndiyo chachu kwao ya kuwatia ari ya kuonyesha kuwa hata wao wanaweza wakafikia kiwango walicho nacho timu hiyo," alisema Prof. Lipumba.
Aidha, aliwatanabaisha wachezaji wa Simba, kutambua kuwa ndiyo timu pekee iliyobakia katika mashindano ya kimataifa, hivyo inatakiwa kuwatoa kimasomaso Watanzania ili kuleta sifa, si kwa timu pekee, bali kwa taifa zima.
 
Shekhan aiua Yanga Dar


na Makuburi Ally


amka2.gif
TIMU ya nyota wa zamani ‘All Stars' waliowahi kukipiga katika klabu ya Simba, jana waliibuka kidedea katika mechi maalumu ya kuwachangia waathirika wa mabomu ya Gongo la Mboto baada ya kuwalaza mahasimu wao Yanga kwa bao 1-0.
Katika mechi hiyo iliyovuta hisia za mashabiki wengi wa soka kutaka kuona vitu adimu vya nyota hao wa zamani, pande zote zilianza mchezo kwa kasi ili kutaka kujipatia bao la mapema.
Walikuwa ni Simba waliofanya shambulizi katika dakika ya 6 tu ya mchezo, lakini shuti la Yussuf Macho ‘Musso' lilidakwa na kipa Peter Manyika, huku Edwin Mukenya katika dakika ya 14, akifanya kazi ya ziada ya kuwapangua wachezaji wa Yanga lakini alishindwa kumalizia kuukwamisha wavuni mpira.
Dakika ya 15 Yanga walijibu mashambulizi lakini Ally Yussuf aliyeukwamisha mpira wavuni alikuwa ameotea.
Simba walijipatia bao la kwanza dakika ya 34 kwa mkwaju wa adhabu wa Shekhan Rashid uliokwenda moja kwa moja nyuzi 90, baada ya Ally Mayai kumwangusha Yussuf Macho nje ya 18. Bao lililodumu hadi dakika 45 za kwanza.
Kipindi cha pili, licha ya mabadiliko kwa timu zote na Yanga kujaribu kuchomoa bao lao kupitia kwa washambuliaji wake Ben Mwalala na Edibily Lunyamila, lakini ngome ya Simba ilikuwa makini kuondosha hatari zote, hivyo hadi filimbi ya mwisho, Simba 1, Yanga 0.
Simba: Issa Manofu, Abubakar Kombo/ Bakari Idd/ Tom Kipese ‘Uncle Tom', Ramazani Wasso, Said Kokoo, Boniface Pawasa, Edwin Mukenya, Said Sued, Shekhan Rashid, Madaraka Selemani ‘Mzee wa Kiminyio'/ Kamba Lufo, Bita John/ Haruna Moshi ‘Boban na Yussuf Macho ‘Musso'/ Mrisho Moshi.
Kocha: Madaraka Selemani.
Yanga: Peter Manyika, Omar Kapilima, Mwanamtwa Kihwelo/ Chibe Chibindu, Bakari Malima ‘Jembe Ulaya', Shabani Ramadhani, Waziri Mahadhi/Idd Moshi, Steven Nyenge/ Deo Lucas, Sekilojo Chambua/ Oscar Makoye, Salvatory Edward ‘Doctor'/ Akida Makunda, Ally Yussuf ‘Tigana'/ Ally Mayai ‘Tembele', Ben Mwalala/ Kudra Omar na Edibily Lunyamila/ Omar Changa. Kocha: Ken Mwaisabula ‘Mzazi'.
 
Barrick kujikita kuendeleza michezo


na Chalila Kibuda


amka2.gif
KAMPUNI ya African Barrick Gold (ABG), imedhamiria kuendeleza michezo mbalimbali hapa nchini ili kutoa fursa kwa vijana kuibua vipaji vyao na kuwa sehemu ya ajira.
Hayo yalibainishwa hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Meneja Uhusiano wa Ndani wa ABG, Blandina Mughezi, wakati akitoa msaada wa sh milioni 20 kwa Kocha wa tenisi nchini, Boaz Mwakusa, kwa ajili ya ujenzi wa viwanja vya mchezo huo katika Shule ya Msingi Isamilo iliyopo jijini Mwanza.
Mughezi alisema kuwa msaada huo unatokana na faida ya biashara ya madini, kwa kurudisha katika huduma za jamii ikiwemo michezo.
Alisema, wanafunzi wataweza kujifunza na kuibua vipaji vyao ambavyo vitaweza kuitangaza Tanzania kupitia mchezo huo.
Mughezi aliongeza kuwa vijana wanaweza kuandaliwa katika nyanja mbalimbali ambazo zitawasaidia katika maisha kwa kutumia vipaji vyao kwenye mchezo.
Aidha alisema ABG itaendelea kuangalia fursa mbalimbali za kuweza kuendeleza michezo ili iweze kukua, ambako ni faida kwa taifa kwa kuwa na vijana wenye vipaji vya kimataifa.
Alisema kujenga kiwanja hicho ni sehemu ya hatua ya awali, hivyo kazi iliyobaki ni kusimamia kuhakikisha kiwanja kinajengwa kwa kiwango kinachostahili.
Naye Kocha wa tenisi nchini, Boaz Mwakyusa, alishukuru msaada huo na kusema atahakikisha wanajenga uwanja kwa kiwango kinachostahili kwa ajili ya mchezo huo.
Alisema mchezo wa tenisi unahitaji kiwanja ambacho kitawezesha wachezaji kucheza katika hali ambayo ni ya kisasa zaidi kuliko mingine.
Mwakyusa alisema kazi yao kubwa ni kuendelea kuhamasisha wadau wa michezo katika kuwa na viwanja vya tenisi, ambavyo vijana watavitumia kuibua vipaji vyao.
 
Gofu kushiriki Kanda ya Sita Nairobi


na Samia Mussa


amka2.gif
WACHEZAJI 10 wa timu ya taifa ya gofu wanatarajiwa kushiriki michuano ya Kanda ya Sita itakayoanza kutimua vumbi Aprili 11 hadi 15 Mombasa, Kenya.
Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Faray Chitengwa, alisema kuwa kabla ya mashindano hayo watashiriki michuano ya Pro- Am inayotarajiwa kufanyika siku moja kabla ya Kenya Open ambayo itafanyika Machi 31, Nairobi, Kenya.
Alisema kuwa kushiriki kwa timu hiyo katika mashindano hayo ni sehenu ya maandalizi ya mashindano ya Kanda ya Sita.
Chitengwa alisema kuwa anaamini wachezaji aliowachagua wana uwezo mzuri wa kucheza, hivyo Watanzania watarajie ushindi mnono katika mashindano yote.
 
Hati ya Uwanja Kaunda yapotea Send to a friend Saturday, 19 March 2011 11:41

Sweetbert Lukonge
UBABAISHAJI mwingine umejitokeza ndani ya klabu ya Yanga baada ya kubainika kuwa hati ya umiliki wa uwanja wa Kaunda ulioko klabuni hapo kupotea.

Klabu hiyo imeeleza kuwa hati hiyo imetoweka na hivyo kuwaomba wanachama wake na watu wengine kujitokeza kutoa ripoti kuhusu ilipo hati ambayo imedaiwa kukwamisha mradi wa kuendeleza uwanja huo wa Shilingi 3 bilioni.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) hivi karibuni limezitaka klabu za Ligi Kuu kuwa na viwanja vyake wenyewe huku Yanga wakidai wameshindwa kuendeleza uwanja huo kutokana na kutokuwa kibali cha kumiliki eneo hilo.

Ofisa habari wa klabu hiyo, Louis Sendeu alisema jana kuwa hati hiyo haijulikani ilipo. Klabu hiyo inamiliki pia jengo lililopo Mtaa wa Mafia, Kaliakoo.

Akizungumza na Mwananchi jana Ofisa habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema kuwa kufuatia hali hiyo uongozi kwa kushirikiana na kamati inayoshugulikia ujenzi wa uwanja huo inaendelea na mchakato wa kuhakikisha inapata hati hiyo ili ujenzi wa uweze kuanza mara moja.

"Tunatoa wito kwa wanachama wetu kushirikiana kwa hili ili kuhakikisha hati hiyo inapatikana kwa sababu mpaka sasa hajulikani kuwa ipo kwa nani. Nasi tayari tumeripoti polisi.

"Kwa yeyote atakaye kuwa na taarifa juu ya hati hiyo tunamwomba awasiliane na uongozi wetu au atoe taarifa katika kituo chochote cha polisi ili suala hili la ujenzi wa uwanja wetu liweze kuanza mara moja," alisema.

Alisema ujenzi wa uwanja huo unatarajia kugharimu kiasi cha Tsh 3 bilioni ili uweze kuwa katika hali nzuri na yakuvutia.
 
Nchimbi tumeona lakini isiwe siasa

ban_tahariri.jpg

amka2.gif
HIVI karibuni Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Emmanuel Nchimbi ameanza kusaka ‘mchawi' wa maendeleoya michezo hapa nchini kwa kuzuru maeneo stahili.
Nchimbi ambaye inaonekana alikerwa na mwenendo mbovu wa michezo nchini, akang'amua njia ya kusaka namna ya kuendeleza na kukuza michezo ni kufika kwa vyama husika ili kusikiliza namna ya kupiga hatua kwa michezo hapa nchini.
Tanzania Daima ni taasisi ambayo iko katika mrengo wa kukuza na kuendeleza jamii ambayo kila uchao ni kelele ambazo hazipati ufumbuzi kutoka viongozi ambao wanapewa dhamana ya kuongoza lakini wanashindwa kupata ufumbuzi wa matatizo.
Tutakuwa wachoyo wa fadhila tukiacha kumpongeza Nchimbi kwa kuliona hilo ambalo viongozi lukuki wameshikilia wizara hiyo ambayo ni moja ya wizara nyeti.
Mara nyingi viongozi wa vyama wamekuwa wakipiga kelele kushindwa kufikia malengo wanayojipangia kutokana na kuwa kama yatima ambao wamesahauliwa na serikali ambayo imefanya michezo kama sehemu ya siasa.
Ilikuwa inashangaza kwa waliopata wadhifa wa kuitumikia wizara hiyo lakini walikuwa wamelala usingizi wa pono na kushindwa kuamka ili michezo ipige hatua na Tanzania ipate sifa.
Viongozi hao walishindwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ambaye mara nyingi alijitambulisha kwamba si mwanamichezo lakini alichokifanya tumekiona ambacho-ametuachia uwanja wa kisasa na mipangilio ya kujenga viwanja vingine pembezoni mwa uwanja wa taifa.
Ulipoanzia Nchimbi usiachie njiani kwa sababu pamoja na kutembelea vyama vichache vya michezo kwa upeo wako kwa haraka haraka, umegundua tatizo ambalo unaweza kuanza nalo.
Inashangaza kwa viongozi wa michezo hasa ya michezo ambayo imeshindwa kuonyesha kwamba Tanzania inaweza kupiga hatua zaidi kupitia michezo kama zilivyo nchi zilizoendelea kama Marekani.
Inaonyesha kwamba tumeona njia ya kutokea katika michezo na sanaa, sasa hatutarajii kwamba mpangilio huo hautochukua muda mrefu katika utekelezaji wake.
Kwani Tanzania kupiga hatua kupitia michezo inawezekana, Nchimbi usikatishwe tamaa na lolote, wanamichezo wako nyuma yako kwa ushauri na mapendekezo, endelea kusaka wachawi wa michezo hapa nchini.
Inashangaza kwamba Tanzania miaka iliyopita ilikuwa tishio katika kila mchezo jambo ambalo nchi nyingi za Afrika ziliitambua kupitia michezo na hata nchi kama Brazil zilileta timu zake kucheza na Tanzania kwa sababu ya umahiri wake katika michezo; lakini hali hiyo haipo tena.
 
TFF ‘iwabebe' wachezaji wa zamani
ban.mtazamo.jpg


Makuburi Ally​

amka2.gif
TANZANIA imebarikiwa kuwa na wachezaji lukuki katika michezo mbalimbali ambao baadhi yao wameiletea sifa nchi kupitia michezo waliyoshiriki kwa nyakati tofauti, ingawa hivi sasa kuna wanaojaribu.
Kwenye soka kuna wachezaji walioiletea sifa Tanzania kama Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga, Jellah Mtagwa, Maulid Dilunga, Kitwana na Sunday Manara ambao ni baadhi ya wachezaji wa zamani wan chi yetu.
Wachezaji hao hadi sasa ndio tunaojigamba nao katika medani ya soka hapa nchini ingawa katika michezo mingine Tanzania bado ina sifa bora kama kwenye riadha kwa waliokuwa wachezaji kama kina Filbert Bayi ambaye ni Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) na Suleiman Nyambui ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania(RT).
Nikirejea katika mtazamo wangu, leo napenda kuzungumzia wachezaji waliowahi kucheza soka hapa Tanzania na ambao waliletea sifa; inaonekana kama TFF ina mshikamano kidogo na wachezaji hao ukilinganisha na mchango walioutoa.
Napendekeza Rais Tenga ambaye ni mmoja wa wachezaji walioiletea sifa Tanzania ambaye anawafahamu wenzake, awe nao karibu ingawa kuna baadhi ambao yuko nao karibu na anafanya nao baadhi ya kazi za TFF ila kasi iongezeke.
Pendekezo langu linaangukia kwa Mtagwa ambaye hivi sasa ana matatizo ya kiharusi, ukikumbuka miaka aliyokuwa akicheza katika timu ya taifa, kwa heshima aliyoipata, picha yake ilitumika katika stempu za barua.
Mtagwa ambaye alikuwa akicheza nafasi ya ulinzi wa kati na Tenga, ambao kwa pamoja waliiletea sifa Tanzania katika soka na leo ana matatizo ambayo anafikia hatua ya kutangatanga huku na huko kusaka namna ya kupata matibabu.
Mchezaji huyo ndiye ambaye tunamuona kwa haraka, ila kuna wengine wengi ambao maisha yao ni ya mashaka, TFF inaweza kusaka namna ya kuwasaidia.
Lakini inashangaza kukosa mwelekeo kwa wachezaji waliowahi kuiletea sifa Tanzania wakati anayeliongoza soka la Tanzania ni mmoja wa wachezaji wa zamani; hao wanaosota ni wenzake ambao, leo wanataabika pasi na kupata msaada.
Sababu za kupendekeza TFF iwabebe wachezaji wa zamani ni kutokana na kwamba soka walilocheza kina Tenga na Mtagwa si kama la sasa ambalo limejaa wafadhili lukuki ukitofautisha na la zamani ambalo mara nyingi wachezaji walicheza kwa sifa ya nchi.
Miaka michache iliyopita TFF ilijaribu kuwakusanya wachezaji hao na kujaribu kuandaa utaratibu wa kuwapa vitambulisho vya kuingilia mpirani bure ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao kwa taifa.
Japo kuna baadhi ya wachezaji waliopata bahati ya kupata vitambulisho hivyo lakini wengi bado wamekuwa wakisukumwa na kunyanyaswa na walinzi wakati wa michezo mbalimbali ya Ligi Kuu na ile ya kimataifa.
Kwa mtazamo wangu wangu kuingia uwanjani bure hakuwatoshi wachezaji hao na bado TFF inapaswa kwenda mbali zaidi kwa kuwatafutia kozi za ukocha na kuwatumia katika kufundisha timu za vijana ikiwamo kusaka vipaji vya wachezaji mbalimbali ili viweze kulisaidia taifa kupiga hatua katika medani ya kimataifa.
Nchi nyingi ambazo zimepiga hatua katika maendeleo ya soka duniani, zimewatumia wachezaji wa zamani wa timu ya taifa na klabu katika kusaka vipaji na hatimaye zikaweza kufanikiwa kwa kuundwa kwa vituo mbalimbali vya michezo vikiongozwa na wanasoka hao wa zamani.
Lakini bado TFF inaweza kuwaenzi wachezaji hao ambao wengi wao wana kipato kidogo na kukabiliwa na maisha magumu kutokana na wakati waliokuwa wakicheza mpira ilikuwa ni kama kujifurahisha zaidi, kwa kuwaandalia mechi mbalimbali zitakazokuwa zikiwahusisha wachezaji hao na kuzitafutia wadhamini na pesa itakayokuwa ikipatikana zikiingizwa katika mfuko wao ukiwa kama Saccos ili waweze kujikwamua kimaisha.


h.sep3.gif

Tuwasiliane kwa simu 0773-508779
 
Wakali wa milima ya Uluguru wanataka kurejea Ligi Kuu
ban.blank.jpg


Ghisa Abby​

amka2.gif
BAADA ya kutwaa ubingwa wa mkoa wa Morogoro katika michuano ya ligi ya taifa ngazi ya mkoa, kazi iliyobaki kwa timu ya soka ya Tumbaku FC, ni kujipanga vizuri zaidi, ikiwa ni safari ya kucheza Ligi Kuu bara.
Timu hiyo ya Tumbaku FC, inayomilikiwa na kampuni ya Tumbaku ya TTPL, hivi karibuni, ilinyakua ubingwa huo wa mkoa kwa kuibuka kinara na kujitwalia sh 100,000 na kombe.
Kwa mujibu wa kocha wa timu hiyo, Experious Mchonde ‘Super,' mafanikio hayo hayakuja kama mvua, bali yaliandaliwa na kujengwa kwa takribani mwaka mmoja.
"Kabla ya kuanza kwa ligi hii, nilihakikisha ninawandaa vizuri vijana ili kuwa na timu shindani na ndivyo ilivyotokea, nashukuru sana, nawapongeza wachezaji na kampuni ya Tumbaku kwa sapoti," anasema.
Mchonde anasema, kutokana na maandalizi hayo mazuri, licha ya kukutana na timu zenye uwezo mkubwa kisoka, vijana wake walijitahidi kupata matokeo mazuri, hadi mwisho wa siku, wakaibuka mabingwa.
Je, ni timu gani ilikuwa tishio katika michuano hiyo? Mchonde anasema zote zilitoa upinzani mkubwa, lakini Alliance One ndio walikuwa wagumu zaidi hasa ikizingatiwa walikuwa wakitetea taji.
"Timu hii nayo ilijiandaa vizuri, kwa sababu walikuwa wakitetea ubingwa wao, lakini tunashukuru tumezima ndoto yao ya kutaka kutwaa ubingwa mara mbili mfululizo," anasema Mchonde.
Ni mara ya ngapi timu yake kucheza mashindano hayo? Mchonde anasema ni zaidi ya mara nne bila mafanikio, hivyo safari hii wakaamua kujiandaa vizuri ili kupata mafanikio makubwa kuliko miaka iliyotangulia.
"Safari hii tuliweka malengo ya kutwaa ubingwa, hivyo kwa jitihada, malengo na sapoti kutoka kwa uongozi wa kampuni, tumefanikiwa."
Kocha Mchonde ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya Tumbaku anasema, anamshukuru Mungu kwani matunda hayo yamekuja ukiwa ni mwaka mmoja tu tangu aanze kuinoa.
Mbali ya mashindano hayo, Mchonde anasema timu yake imewahi kushiriki mara mbili mashindano ya Shirikisho la Michezo, Mashirika ya Umma na Makampuni binafsi (SHIMMUTA), na mashindano ya Mei Mosi waliyoshiriki mara tatu.
"SHIMMUTA tumeshiriki mara mbili na mara ya mwisho ilikuwa ni mwaka jana, ambapo tulitwaa ubingwa, mashindano ambayo yalifanyika mkoani Tanga," anasema.
Aidha, timu hii imewahi kushiriki mashindano ya Mei mosi na kutwaa ubingwa mwaka jana, hivyo safari hii watashiriki wakiwa mabingwa watetezi.
Akizungumzia matarajio ya timu yake katika Ligi ya Taifa, Mchonde anasema kazi kubwa inayowakabili ni kujiandaa vizuri, ili kutimiza azma ya kurejea Ligi Kuu ya bara waliyowahi kushiriki kabla ya kushuka.
Anasema, timu hiyo ni kati ya vigogo vya soka vilivyowahi kutikisa soka ya Tanzania wakati huo ikicheza Ligi Kuu hadi katikati ya miaka ya 1980.
Anasema, tangu iliposhuka, timu hiyo ilikaa muda mrefu bila kushiriki mashindano yoyote kutokana na mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi wa kiwanda.
"Kwa sasa uongozi wa kampuni uliopo madarakani unapenda sana masuala ya michezo, ndio maana tunafanya vizuri katika kila mashindano," anasema.
Pamoja na timu hii kumilikiwa na kampuni ya Tumbaku ya TTPL, bado inakabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo upungufu wa vifaa vya michezo kama viatu, mipira na jezi.
Kocha huyu, anatoa wito kwa wadau wa michezo mkoani Morogoro kuisaidia kwa hali na mali, ili timu hiyo iweze kuleta sifa katika mkoa huo.
Aidha, ameuomba uongozi wa Chama cha Soka Mkoa wa Morogoro (MRFA), kuonyesha ushirikiano katika kukabiliana na mashindano yajayo.
Mchonde anasema siri ya mafanikio ya timu, ni maandalizi hivyo timu hiyo inapaswa kuandaliwa vizuri ili iweze kuwa shindani kwa maslahi ya soka ya mkoa huo na taifa.
Anasema, lengo ni kuuwakilisha vizuri mkoa, hivyo wanaelekeza nguvu katika mazoezi ili kuwa shindani katika Ligi ya Taifa ngazi ya taifa.
Naye Buya Kassim ambaye ni mchezaji wa timu hiyo, aliyeibuka mfungaji bora wa ligi ya mkoa, anasema licha ya kutopatiwa zawadi kutokana na kutokuwepo kwa zawadi hiyo, kwake ni faraja kubwa.
Anasema zawadi ya kitu ni matokeo ya kufanya vizuri, lakini kutokabidhiwa zawadi rasmi ya ufanisi wa kazi, bado hakuondoi ufanisi wenyewe, hivyo ataongeza juhudi akijua ipo siku atapata zawadi.
"Licha ya kutotangazwa na kupewa zawadi ya ufungaji bora wa ligi, lakini kitendo cha kuwa kinara wa mabao katika ligi hii, kwangu ni zawadi tosha ambayo itakuwa changamoto ya mimi kujituma zaidi kukuza kipaji changu," anasema Kassim.
Anasema, juhudi zake binafsi pamoja na kuzingatia maelekezo ya kocha wake, ndio siri kubwa ya mafanikio yake dimbani akiifungia timu yake jumla ya mabao sita.
Naye Katibu Mkuu wa MRFA, Hamisi Semka, anasema timu hiyo ilitwaa ubingwa baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Alliance One katika mechi ya mwisho.
Anasema, wanashukuru kwa sababu timu yao imekuwa na mwendo mzuri tangu kuanza kwa michuano hiyo kwa kutofungwa, hivyo kumaliza wakiwa vinara kwa pointi 12.
Anasema kutokana na mafanikio hayo, timu hiyo itauwakilisha mkoa kwenye mashindano ya ligi ya Taifa ngazi ya taifa yatakayotangazwa baadaye na Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF).
Katika michuano hiyo iliyofikia tamati hivi karibuni, timu ya Mitumba ilitwaa nafasi ya pili, hivyo kujitwalia kombe dogo na shilingi 50,000.
Aidha, katibu huyo amewashukuru wakazi wa mkoni hapa kwa ushirikiano mkubwa kwa kipindi chote cha michuano hiyo na kusihi moyo huo uendelee kwa maslahi ya timu hiyo na soka ya Mkoa wa Morogoro.



h.sep3.gif
 
Hata wa kumrithi Kipingu hatumpati
ban.blank.jpg


Mwandishi wetu​

amka2.gif
UNAPOITAJA shule ya sekondari Makongo, kwa wadau wa michezo hususan wa soka, watakuelewa mara moja kwamba, unataka kuzungumzia vipaji vya soka vilivyoibuliwa na kuendelezwa shuleni hapo.
Baada ya klabu kongwe za Simba, Yanga, Pamba ya Mwanza na nyinginezo kushindwa kuendeleza ule mpango wao wa kuzalisha nyota wao wenyewe, basi shule ya Makongo ilivipokea vigogo hivyo jukumu la kuvivumbua na kuviendeleza vipaji.
Nyota wote waliotamba katika timu mbalimbali za Ligi Kuu na ligi nyingine za soka hapa nchini kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 2000, walikuwa wamepitia katika chuo hicho kisicho rasmi cha sekondari ya Makongo, iliyokuwa chini ya Kanali Idd Kipingu ambaye hivi sasa amestaafu.
Ingawa shule hii inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), haikuwa ikipatiwa msaada wa moja kwa moja kutoka serikalini hususan wizara yenye dhamana na michezo, lakini iliweza kuwapokea vijana wenye vipaji vya soka na michezo mingine na kuwasomesha bure, lengo likiwa ni kuviendeleza vipaji vyao, badala ya kuachwa wakihangaika mitaani.
Mambo yaliyokuwa yakifanywa na shule hiyo, kwa kiasi kikubwa yalizishawishi shule kadhaa za jijini Dar es Salaam, nazo kufuata mkondo huo.
Kati ya hizo, ni pamoja na sekondari za Jitegemee chini ya Kanali Fabian Massawe ambaye naye ni mstaafu hivi sasa, Tegeta chini ya Patrick Makoyola ni kati ya zilizoipokea vema changamoto hiyo iliyoanzishwa na Makongo, kwani nazo ziliweza kuwapika nyota katika michezo kadhaa, ambao baadaye walikuja kutikisa na wengine wanaendelea katika medani ya soka na michezo mingine.
Wakati huo, mfano Jitegemee chini ya Kanali Massawe na Makongo chini ya Kanali Kipingu kutokana na kuwa maarufu kupika vipaji, kukaleta hamasa na ushindani wa hali ya juu kisoka, pale zinapokutana sambamba na Tegeta.
Mechi baina ya shule hizi, ilikuwa na ushindani kama ule wa Simba na Yanga, lakini hii ilikuwa na tofauti moja kwamba, haikutawaliwa na mambo ya kishirikina kama ilivyo kwa klabu hizo kongwe, hapa ilikuwa ni uwezo wa makocha na vipaji vyenyewe basi.
Utaalamu waliokuwa nao wachezaji hawa, unapokolezwa na vipaji vyao, ilikuwa ni burudani ambayo, kwa mpenzi yeyote wa soka asingesita kunyanyuka kitini na au kushangilia ama kufurahia mambo yanayofanyika uwanjani.
Nyota wengi waliotamba nchini kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 2000, walikuwa wamepitia hapo, ingawa baadhi wameshaacha soka, lakini baadhi bado wangali wanaendelea kutesa hadi sasa.
Wachache kati ya nyota wengi waliopitia Jitegemee, Makongo na Tegeta ni pamoja na makipa Juma Mpongo na Juma Kaseja, wapo pia Ephraim Makoye, Aaron Nyanda, Ally Mayai, Boniface Pawasa, Kudra Omari, Shabani Dihile, Henry Joseph na wachezaji wa mwisho mwisho kupikwa katika shule hizo akina Jerryson Tegete, Kigi Makasi na John Boko ‘Adebayor'.
Swali, ni je kuondoka kwa kina Kanali Kipingu, Massawe ama Makoyola, ndio mwisho wa kupikwa vipaji katika shule hizi tatu zinazomilikiwa na JWTZ, JKT na Jumuiya ya Wazazi?
Ni jambo la kustikisha sana, kuona kuwa miaka michache tu baada ya waliokuwa wakuu wa shule hizo kuondoka, mambo yamebadilika, Makongo, Jitegemee na Tegeta sio tena vitalu vya kupika vipaji vya wanamichezo, kama ilivyokuwa.
Kwa hakika, kujitokeza kwa shule hizi, kulisaidia kwa kiasi kikubwa sio tu kuwapika wachezaji kisoka, lakini hata kuleta hamasa ya soka, kwani shule hizo zilileta upinzani wa kimichezo kuanzia kwa watoto wanaosoma hapo hadi kwa wazazi ndugu na marafiki wa watoto wa shule hizo.
Kwa kweli hili ni jambo la kusikitisha sana kuona, waliorithi nafasi za waliokuwa wakuu wa shule hizo kipindi hicho, wameshindwa kuuendeleza zaidi msingi uliokuwa umejengwa kwa muda mrefu.
Tofauti na Simba na Yanga, Jitegemee, Makongo na Tegeta, ziliwapa wachezaji elimu ya sekondari na kuwafumbua macho kimaisha, lakini sasa zinatoweka na cha kusikitisha hakuna wahusika walioweza kulibaini hili.
Walipaswa kukutana wahusika na kujadili kilichowakumba na kuona jinsi watakavyoweza kutatua, vinginevyo ndio tutakuwa tunayarudia yale yale yaliyofanywa na Simba, Yanga na klabu nyingine.
Inasikitisha kusema kwamba, Makongo ilikuwa ni Kipingu, Jitegemee ilikuwa ni Massawe, Tegeta ilikuwa Makayola, bila hawa hakuna Makongo, Jitegemee wala Tegeta za soka, netiboli, kikapu na michezo mingine, bali ni masomo kama zilivyo shule nyingine, hakika kwa staili hii hatufiki.
 
Jinsi ubalozi wa Brazil unavyowekeza katika michezo na utamaduni Tanzania
ban.blank.jpg


Mariana Mathias​

amka2.gif
NCHI ya Brazil si ngeni miongoni mwa Watanzania wengi, hasa kutokana na kujipambanua zaidi kimataifa kupitia michezo hususan soka ambayo imeweza kuwanadi zaidi kimataifa.
Ushirikiano kati ya Brazil na Tanzania umekuwa ukizidi kuimarika kila kukicha kupitia nyanja mbalimbali ikiwamo utamaduni na michezo.
Ofisi ya ubalozi wa Brazil nchini Tanzania, ina Kitengo cha Utamaduni na Michezo, ambacho kwa nyakati tofauti kimekuwa na programu mbalimbali za ushirikiano, ambazo kwa namna moja ama nyingine kimeweza kuwa msaada mkubwa kwa Watanzania.
Lazaro Ngimba ni Mkurugenzi wa Utamaduni na Michezo Ubalozi wa Brazil nchini Tanzania, ambaye anaeleza programu mbalimbali zinazowekezwa hapa nchini na kitengo chake.
Ngimba anasema, kati ya programu walizofanikiwa kuziendesha ni pamoja na kuwekeza katika kuwasaidia watoto yatima wanaolelewa katika shule iliyo ndani ya Taasisi ya Utamaduni na Michezo (NVRF), Manzese jijini Dar es Salaam.
Anasema, walishawishika kuwasaidia na kuwatia moyo watoto hao, hasa kutokana na kutambua kuwa hivi sasa kundi la yatima na watoto waishio katika mazingira magumu limekuwa likizidi kuongezeka kila siku hapa nchini, hivyo kuona umuhimu wa kuwasaidia.
Ngimba anasema, pia ubalozi wa Brazil umeweza kutambulisha na kuhamasisha mchezo ujulikanao kama Kapoeira ambao ulifanikiwa kuanza rasmi jijini Dar es Salaam Dar es Salaam Februari 20 mwaka jana.
Anasema, kupitia Balozi wa Brazil nchini, Francisco Luz, walifanikiwa kwa kuhamasisha watu na kutoa elimu juu ya mchezo wa Kapoeira na kuanzisha kikundi cha Utamaduni wa Kapoeira Dar es Salaam.
"Tulipigania mchezo huu uanzishwe rasmi Tanzania, kwa kuwa ni mchezo ambao una asili ya Kiafrika na Kibrazil ambao ulianzishwa na watumwa weusi, waliokuwa wakitawaliwa na Wareno na waliutumia mchezo huu, katika kupanga mipango ya kuwatoroka askari waliokuwa wakiwatumikisha," anasema Ngimba.
Anasema, mchezo huo ulikuwa ukipigwa vita, kwani watumwa walikuwa wakikaa vikao kupanga mbinu za kutoroka na pindi askari wa Kireno wakitokea, walianza kucheza Kapoeira ikiwa njia ya kuwazuga kuwa hawakuwa na jambo jingine zaidi ya kujifurahisha kwa kucheza.
"Japokuwa mchezo huo ulipigwa vita sana, ulisambaa kwa kasi sana na ulianza kufika nchini Angola, Afrika Kusini na hatimaye kuenea nchini Brazil ambapo waliufanya kama mchezo wao wa kiutamaduni na baada ya hapo ulifika Afrika Mashariki na kwa Tanzania ulianza kufikia Zanzibar," anasema Ngimba.
Ngimba anasema, mchezo huo unaochezwa kwa mapigano, ngoma na nyimbo zenye sauti tofauti, kulingana na aina ya mapigano, ulianza kukubalika na kupendwa na watu wengi na hatimaye alifanikiwa kuuhamasisha shuleni na hata kufanikiwa kuchezwa katika matamasha mbalimbali nchini.
Mkurugenzi huyo anaongeza kuwa katika kuinua vijana kimichezo, waliamua kudhamini mashindano yaliyojulikana kama Kawe Cup ambayo yamemalizika hivi karibuni.
Anasema, lengo la mashindano hayo yalikuwa ni kusaka vijana wenye vipaji, kwa ajili ya kuwapeleka Brazil kwa mafunzo zaidi ya soka katika chuo kijulikanacho kama Curabita kilicho nchini humo.
Anasema, tayari vijana watano wamepatikana na wanatarajiwa kwenda nchini Brazil mwezi ujao, wakiwa huko watapokelewa na aliyekuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Soka Tanzania, Taifa Stars, Marcio Maximo.
Pokea ujumbe kutoka katika Makala hii na uutendee kazi, kwa ushauri na mchango wasiliana nami :
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom