Spurs 'inaishi kweny ndoto' Send to a friend Thursday, 10 March 2011 20:00
LONDON, England
KOCHA Harry Redknapp amekiri kuwa Tottenham ipo kwenye nchi ya ahadi baada ya kufanikiwa kufuzu kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya AC Milan.
Vijana hao wa Redknapp walionekana kuwa kwenye wakati mgumu mbele ya Milan kwenye Uwanja wa White Hart Lane, lakini walifanikiwa kupata suluhu na kufuzu kwa 16 bora baada ya kupata bao moja kwenye mchezo wa kwanza shukrani kwa Peter Crouch aliyefanya vitu vyake kwenye uwanja wa San Siro.
Wakati Redknapp alipowasili White Hart Lane, na kuichukua timu hiyo ikiwa kwenye janga la kushuka daraja, lakini sasa timu hiyo imejiwekea ndoto ya kucheza fainali ya Ulaya kwenye Uwanja wa Wembley.
Baada ya miaka mingi ya kufunikwa na kivuli cha mahasimu wao Arsenal, sasa Tottenham imerudi kwenye mstari wake, huku Gunners watakuwa mashuhuda wa michuano hiyo kwenye televisheni baada ya kutolewa na Barcelona, Redknapp amewataka mashabiki wake kuongeza ushirikiano kwa kufikia mafanikio hayo.
"Sijui ni wapi tutaishia, lakini kwa sasa tumefanya kazi kubwa," alisema Redknapp. "Kama ningesema miaka miwili iliyopita kwamba tutafikia kwenye nane bora ya Ligi ya Mabingwa mgeweza kuniambia kwamba ninawazimu.
"Mashabiki wetu sasa wanaishi. Kwa tulipofika sasa ni kitu cha kusadikika tu. "Hii ni mara ya kwanza kwenye historia ya klabu hii kwenye Ligi ya Mabingwa. Kufanya hichi tulichokifanya, kwanza tulikuwa kwenye kundi gumu na tumeweza kuifunga AC Milan, watakuwa wakifurahi kwa muda mrefu zaidi.
xxxxxxxx
Raul ashangilia kuibeba Schalke
MUNICH, Ujerumani
MSHAMBULIAJI nyota wa Schalke 04, Raul amefurahishwa na kitendo cha timu yake kufuzu kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa ushindi wa 3-1 na kusonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-2 dhidi ya Valencia.
Mshambuliaji huyo mkongwe wa Hispania, aliyewahi kutwaa taji hilo mara tatu akiwa na Real Madrid katika mwaka 1998, 2000 na 2002, aliongeza kusema kuwa sasa wamefurahishwa na kupiga hatua hiyo kubwa.
"Ulikuwa mchezo mgumu, lakini ukiwa sawa kwa pande zote," alisema Raul, ambaye yuko kwenye msimu wake wa kwanza na Schalke.
"Hata hivyo sisi tulikuwa na bahati zaidi. "Nimefurahi kwa sababu ili ni jambo zuri zaidi kwangu.
"Tunasubili kuona ni nani tutakutana naye kwenye robo fainali, lakini si jambo linalotuumiza sana kichwa kwa sababu ni sehemu ya mchezo huo.."
Mara ya mwisho kwa klabu hiyo kutinga kwenye hatua hiyo ni mwaka 2008, Schalke ilijihakikishia nafasi yake kwa mabao yaliyofungwa na winga Jefferson Farfan na mshambuliaji Mario Gavranovic.
Wenyeji hao walilazimika kusawazisha kwanza baada ya Valencia kupata bao la mapema kupitia Ricardo Costa.
"Ni vigumu kuanza kupambana na presha toka mwanzo, lakini baada ya kufungwa 1-0 hatukuwa na chakupoteza," alisema kocha wa Schalke, Felix Magath.