Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Kuyt aimaliza Man U Send to a friend Monday, 07 March 2011 12:42

LIVERPOOL, England
MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Dirk Kuyt alifunga mabao matatu na kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi mkubwa wa mabao 3-1 dhidi ya Manchester United katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyokuwa na ushindani wa juu iliyofanyika kwenye Uwanja wa Anfield.

Kwa ushindi huo iliopata Liverpool imefungua milango ya kinyang'anyiro cha kuwania ubingwa wa ligi hiyo kwa timu zilizo juu kwenye msimamo.

Bao la kwanza la Liverpool lilifungwa na Kuyt katika dakika ya 34 baada ya Luis Suarez kuwapiga chenga mabeki watatu wa Manchester United na kumpasia Kuyt aliyefunga kirahisi.

Kuyt alifunga tena bao la pili katika dakika ya 39 baada ya Nani kukosea kupiga kichwa mpira ambao ulirudi kwenye goli lao na kumpita Chris Smalling na kumkuta Kuyt ambaye alifunga bao hilo kwa kichwa.

Timu hizo zilienda mapumziko huku Liverpool ikiwa inaongoza kwa mabao mawili, lakini katika kipindi cha pili Dirk Kuyt aliongeza bao la tatu baada ya Luis Suarez kupiga faulo ambayo ilipanguliwa na kipa Va der Sar na mpira ulimkuta Kuyt ambaye hakusita kuuweka wavuni.

Manchester ilipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 91 ambalo lilifungwa na Javier Hernandez kwa kichwa ambaye aliunganisha krosi ya Ryan Giggs.

Hivi sasa Liverpool inashika nafasi ya sita ikiwa na pointi 42 wakati Manchester United imeendelea kuongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 60 na kuipa nafasi Arsenal inayoshika nafasi ya pili ikiwa na pointi 57 ya kuweza kuifikia.

Wiki iliyopita Manchester United ilifungwa bao 2-1 na Manchester United huku Liverpool ikifungwa bao 3-1 na West Ham United.
 
Vigogo wazisusa Yanga, Simba Send to a friend Monday, 07 March 2011 12:40

Mwandishi Wetu
HUKU Yanga na Simba kila moja ikichuma Shilingi 51,194,793 kati ya Sh243m zilizopatikana katika mchezo baina yao juzi, watu wenye uwezo kifedha walizisusa tiketi za kuangalia mchezo huo.

Kulingana na ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuhusu mapato ya mechi hiyo ambayo iliingiza mashabiki 46,539 kati ya zaidi ya 57,000 waliotarajiwa, viti 309 kati ya 748 vya VIP A-C ndivyo vilivyonunuliwa na mashabiki katika mchezo huo.

Mchanganuo wa mauzo ya tiketi hizo, Wambura alieleza kuwa viti vyote vya kijani ,19,648 na vile vya bluu ambavyo ni 7,045 tiketi zake ziliuzwa.

Alisema maeneo ambayo tiketi hazikuuzwa zote ni viti vya rangi ya chungwa , VIP C, VIP B na VIP A ambapo tiketi zilizouzwa ni 309 kati ya viti 748 vilivyopo.

Kwa mujibu wa ofisa huyo, viingilio katika mechi hiyo iliyooneshwa moja kwa moja (laivu) na Star TV na Super Sport 9 ya Afrika Kusini vilikuwa Sh 3,000 (viti vya kijani), Sh 5,000 (viti vya bluu), Sh 7,000 (rangi ya chungwa, Sh10,000 (VIP C), Sh 20,000 (VIP B) na Sh 30,000 kwa VIP A.

Alisema baada ya kuondoa gharama za mchezo na mgao kwa uwanja, Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kila timu ilipata mgao wao kulingana na kanuni zilizopo.

Pambano hilo la Ligi Kuu ya Vodacom lilichezwa juzi, Machi 5 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam likiwa ni mwendelezo wa mzunguko wa pili wa ligi hiyo ambao umebakisha mechi sita.

Hadi sasa, Yanga inaongoza ikiwa na pointi 39 na kufuatiwa na Simba yenye pointi 38 na Azam, pointi 36. Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea Machi 9, Jumatano.
 
Uongozi Simba wamkomalia Mbaga Send to a friend Monday, 07 March 2011 12:38

Clara Alphonce na Doris Maliyaga
HUKU vumbi la mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga likitua, uongozi wa klabu ya Simba umemkomalia mwamuzi Oden Mbaga.

Mwenyekiti wa klabu hiyo, , Ismail Aden Rage amesema kuwa anatarajia kumshitaki mwamuzi huyo katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Rage alidai juzi kutoridhishwa na maamuzi ya Mbaga kila anapochezesha mechi inayoihusu timu yake.

Katika mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaamu juzi timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.

Rage aliiambia Mwananchi kuwa katika uchunguzi ambao ameufanya unaonyesha wazi kuwa mwamuzi huyo amekuwa haitendei haki Simba kila anapochezasha iwe katika mechi nyingine tofauti na Yanga, jambo ambalo alidai kuwa linalenga kuiua timu hiyo ishindwe kufanya vizuri kwenye ligi hiyo.

ìTunatarajia kumshitaki Mbaga TFF kutokana na kutolizishwa na maamuzi yake kila anapochezesha mechi zinazoihusu Simba ukilinganisha na waamuzi wengine.

ìKatika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Yanga kwa hakika mwamuzi huyo alilenga kutuumiza kutokana na kutokuwa na maamuzi mazuri kwa upande wetu, hivyo kufuatia hali hiyo tunatarajia kumshitaki TFF na tunacho subiri ni kupata baadhi ya mikanda ya video ya mechi zote alizochezesha dhidi yetu,î alisema Rage.

Alisema katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Yanga mwamuzi huyo alikuwa haitendei haki timu yake na kuongeza kuwa wapinzani wao walikuwa wakifanya makosa ya wazi na hakuchukua hatua yoyote.

Naye makamu mwenyekiti wa klabu hiyo, Godfrey Nyange ëKaburuí alieleza kumshangaa mwamuzi Mbaga akidai kuwa kiwango chake kilikuwa kidogo.

Alisema Super Sport ilimuumbua mwamuzi huyo kutokana na maamuzi yake yasiyo ya halali baada ya kuwekwa wazi.

Aliiambia Mwananchi kuwa, maamuzi yake hayakuwa sahihi na kama si televisheni hiyo ya Afrika Kusini iliyokuwa inarusha wazi kurudia tukio la bao la Simba yangekuwa mengine.

"Mechi ilikuwa nzuri, lakini mwamuzi aliuharibu mchezo hasa bao lililofungwa na Simba, yeye alishindwa kuamua hadi mshika kibendera wa pili alipoingilia kati,ííalisema Kaburu.

ëíHii ni kwa sababu ya televisheni ile ilimuumbua baada ya kurudia tukio lile mara kwa mara naweza kusema kiwango cha waamuzi wetu bado ni kidogo sana,ííaliongeza Kaburu.

Katika mchezo huo Yanga ilikuwa ya kwanza kupata bao kwa penalti iliyotokana na Davies Mwape kudondoshwa eneo la hatari na Juma Nyosso na beki Stephano Mwasika kufunga wakati Simba ilisawazisha kupitia kwa Mussa Hassan ëMgosií.
 
Majimaji wakumbuka shuka kukiwa tayari kumekucha Send to a friend Monday, 07 March 2011 12:37

Happy Kiula
UONGOZI wa timu ya Majimaji ya Songea 'Wanalizombe' umepania kufanya vizuri katika mechi nne zilizobaki ili kuhakikisha wanabaki Ligi Kuu msimu ujao.

Akizungumza na Mwananchi, mwenyekiti wa klabu hiyo, Ahmed Dzumba alisema wamebakiza mechi tatu ambazo watachezea uwanja wa nyumbani na mechi ya mwisho watamaliza na Simba kwenye Uwanja wa Uhuru.

Alisema hawakuridhika na sare dhidi ya Azam FC kwa kocha Sebastian Nkoma aliyekuwa akiwaangusha wameshamtimua na wamekania kufanya vizuri ili wasishuke daraja.

Aidha, timu ambayo ina pointi 12 ikiwa ya pili kutoka mwisho imesaliwa na michezo minne na watakutana na Toto Africa, Kagera Sugar, Ruvu Shooting na Simba, huku wajifariji kufunga kwa michezo hiyo.

Dzumba alisema: ''Tumeazimia kushinda michezo iliyobaki ingawaje mchezo wa Simba bado unatuweka shakani na hatujielewi kama tutawafunga au la lakini hiyo mengine tuna uhakika,'' alisema.

AFC ndiyo timu pekee inayoonekana kukata tamaa kwani ndiyo iliyofungwa mabao 31 ikilinganishwa na timu nyingine kwenye ligi hiyo huku ikishikilia mkia ikiwa na pointi zake 11.

Timu hiyo imebakisha michezo mitano na ili kujikwamua, inatakiwa kushinda yote walau kufufua matumaini, kitu ambacho hakiwezi kutokea.
 
Kipa Mtibwa amshukuru Mungu kumwepusha kifo Send to a friend Monday, 07 March 2011 12:26

Jessca Nangawe
KIPA wa Mtibwa Sugar, Ally Omari amesema alichungulia kaburi siku ya mchezo wao na Simba uliofanyika hivi karibuni kwenye Uwanja wa Uhuru.

"Unajua ilikuwaje, nilimwona jamaa yule (Mkina) Shija anakuja na mpira, nikautokea kama kawaida, sasa ile kwenda chini, sikuona kitu kilichoendelea.

"Alinikanyaga shingoni, nikaona nyota, sikuona tena wala sikumbuki kama nilikuwa uwanjani, nilishtukia niko hospitali ya Agakhan.

Aliongeza kuwa alipata fahamu majira ya saa tatu usiku na kitu cha kwanza alisikia habari kuwa timu yake imefungwa magoli 4-1 kitu ambacho kilimuumiza lakini alijipa moyo na kuamini bado wana nafasi nzuri ya kufanya vizuri katika michezo yake inayokuja.

Omary aliyewahi kuichezea Mlandege ya Zanzibar kabla ya kuhamia Mtibwa alieleza kuwa katika maisha yake ya soka hajawahi kukutana na rafu mbaya kama ile iliyomsababishia kupoteza fahamu kwa muda mrefu.

Alikiri kuwa yalikuwa ni makosa ya kibinadamu ambayo hayazuiliki katika mpira.

"Ni rafu ambayo awali katika maisha yangu ya soka sijawahi kukutana nayo, nakiri ni moja ya matokeo yoyote yanayoweza kutokea lakini ni kitu ambacho sitaweza kukisahau katika maisha yangu,"anaelezea Omary.

Anasema kuwa kuumia kwake kumechangia kwa kiasi kikubwa matokeo yale kutokana na kuwa anaamini endapo angebaki golini wasingeweza kufungwa magoli mengi kama yale.

"Nilijisikia vibaya hasa baada ya kuzinduka na kusikia tumefungwa magoli manne, sisemi kama kipa mwenzangu hana uwezo, lakini kama mnavyotambua ni mechi chache ambazo anapewa kucheza ukilinganisha nami au Kado Shaaban," alieleza.

Aidha, kipa huyo aliongeza katika mahojiano na Mwananchi kuwa kumekuwepo na ushindani mkubwa katika ligi hiyo ambayo licha ya kukaribia ukingoni bado hawezi kutabiri ubingwa utakwenda wapi kutokana na timu nyingi kukaribiana kwa idadi ya pointi.
 
Mukenya: Wachezaji wa kigeni viwango duni Send to a friend Monday, 07 March 2011 12:24

Sweetbert Lukonge
BEKI wa zamani wa kimataifa wa Kenya aliyezichezeaYanga na Simba , Edwin Mukenya amesema kuwa anashangazwa na viwango vya baadhi ya wachezaji kutoka nje ya Tanzania waliosajiliwa na klabu mbalimbali za Ligi Kuu nchini kutokuwa na sifa za kuwa wachezaji wa kulipwa.

Akizungumza na Mwananchi jana, Mukenya ambaye kwa sasa anachezea Tusker ya Kenya alisema kuwa amekuwa akifuatilia Ligi Kuu ya Tanzania Bara kila wakati lakini amekuwa akishangazwa na viwango vya baadhi ya nyota hao wa kigeni hususani wale wa klabu za Simba na Yanga kuwa ni vya chini sana ukilinganisha na uwezo wa wazawa.

ìKwa hakika haipendezi kwa mchezaji wa kulipwa (professional ) kuwa na kiwango cha chini kuliko wazawa ambao wanapaswa kujifunza kutoka kwake na pia kuwapa ushauri mbalimbali ambao pia utawasaidia na wao kufikia hatua kama yako.

ìLakini, kwa baadhi ya wachezaji wa kulipwa wa sasa waliopo Tanzania kwa hakika hawakustaili kuwepo kutokana na uwezo wao kuwa chini ukilinganisha na wakati nilipokuwa Simba pia Yanga ambapo uwezo wa wachezaji wote wa kigeni ulikuwa juu na tulizisaidia timu zetu kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya Ligi Kuu pamoja na yale ya kimataifa,î alisema Mukenya.

Alisema viongozi wa klabu zote nchini wanatakiwa kuwa makini katika suala zima la usajili wa wachezajikutoka nje ya nchini ili kuepukana na wachezaji ambao baadaye baada ya kujiunga na timu zao wakuwa mizigo na hawana mchango wowote ndani na nje ya timu.

Mbali na suala hilo pia amewataka kushirikiana na wataalamu mbalimbali kabla ya kufanya usajili ikiwa ni pamoja na kupata historia ya wakati ulipo ya mchezaji husika na kuachana iliyopita ili kuhakikisha kuwa mchezaji wanaye msajili yupo katika kiwango kizuri.

Hivi karibuni Shirikisho la soka Tanzania (TFF) liliamua kupitisha shelea ya usajili wa wachezaji wa kigeni ambayo itaanza kutumika katika msimu wa 2012 -2013 kwa klabu kusajili wachezaji wasiozidi watatu hii ni kutoka na kutolizishwa na viwango vya wachezaji wa kigeni.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom