Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,504
- 911,249
- Thread starter
- #9,261
Sikubaliani nao- Kaijage Send to a friend Tuesday, 01 March 2011 20:20
Sosthenes Nyoni
ALIYEKUWA ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Florian Kaijage ameibuka na kupinga ripoti ya kamati ya uchunguzi ya tukio la kutopigwa nyimbo za taifa wakati wa mechi Taifa Stars na Morocco iliyofanyika Oktoba 9 mwaka jana ambayo inamtuhumu kuwa mhusika mkuu.
Kamati hiyo iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hamidu Mbwezeleni ilitoa ripoti ya uchunguzi Jumanne wiki hii na kumtaja Kaijage kuwa chanzo cha tukio hilo kwa madai alishindwa kutekeleza majukumu yake kama alivyoagizwa na kamati ya maandalizi ya mchezo huo iliyokuwa chini ya Leonard Thadeo.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam jana, Kaijage alisema hakubaliani na utaratibu uliotumiwa na kamati ya uchunguzi hasa namna ya kutoa taarifa zake baada ya kumaliza kazi iliyopewa na TFF.
Alisema kwa uzoefu wake na akiwa ameshuhudia kamati mbili zilizoundwa kuchunguza matukio ya timu ya taifa ya umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys kudanganya umri na waamuzi kula rushwa,mara baada ya kamati ya Mbwezeleni kumaliza uchunguzi wake ilitakiwa kuwasilisha taarifa TFF ambao ndio walitakiwa kuchukua hatua.
"Mimi sikuwa mwajiriwa wa kamati bali TFF,ilichotakiwa kufanya kamati ni kuikabidhi TFF taarifa badala ya wao kuutangazia umma,"alisema Kaijage.
Kaijage alisema ameshindwa kuyaelewa matokeo ya kamati hiyo hasa kwa kuwa ni wajumbe wawili tu kati ya watano walioteuliwa ndio alionana nao kwa ajili ya mahojiano.
"Sote tunajua kamati ilikuwa na wajumbe watano walioteuliwa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga, kimsingi kamati ilinihoji mara mbili, mara ya kwanza ilikuwa Jumanne Januari 25 kuanzia saa sita 6 mchana na mara ya pili ilikuwa Februari 12, 2011, mara zote mbili ni mwenyekiti na katibu wa kamati ndiyo walionihoji. Sikutarajia mara zote mbili wajumbe wangekuwa wawili tu hasa ukizingatia tayari TFF ilikuwa imenitaja kama mhusika mkuu,"alisema Kaijage.
Alisema hata shahidi aliyeelezwa na kamati kwamba alidanganya kwa nia ya kuwapumbaza wajumbe yeye hakuwahi kumwita wala kumpendekeza na kudai kama shahidi alifanya hivyo ilikuwa ni kwa matakwa yake.
Aidha, alisema ameshangazwa na kitendo cha kuondoka kwa fundi ambaye ni raia wa China kwenye mitambo na kuonekana ni kosa la lake yeye (Kaijage).
"Ifahamike kuwa fundi huyo wa mitambo alikuwa anaonana na ofisa habari siku ya mchezo kwa sababu ndiyo sehemu yake ya kazi na uhusiano baina yetu ni kwenye mitambo, pia tukumbuke kwamba hajui Kiingereza zaidi ya Kichina, sasa najiuliza kama alikuwa anamtafuta Kaijage alimuuliza nani na yeye anaongea Kichina tu? Kosa langu hapa ni lipi,ili ni swali ambalo halina jibu,"alisema Kaijage.
Katika mechi hiyo ambayo iliyoshuhudiwa pia na Rais Jakaya Kikwete, CD iliyopaswa kupigwa nyimbo za taifa za Morocco na Tanzania ziligoma na kusababisha shughuli hiyo kufanywa kipindi cha pili cha mchezo, hivyo Tenga kutangaza kumsimamisha kazi kwa Kaijage .
Sosthenes Nyoni
ALIYEKUWA ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Florian Kaijage ameibuka na kupinga ripoti ya kamati ya uchunguzi ya tukio la kutopigwa nyimbo za taifa wakati wa mechi Taifa Stars na Morocco iliyofanyika Oktoba 9 mwaka jana ambayo inamtuhumu kuwa mhusika mkuu.
Kamati hiyo iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Hamidu Mbwezeleni ilitoa ripoti ya uchunguzi Jumanne wiki hii na kumtaja Kaijage kuwa chanzo cha tukio hilo kwa madai alishindwa kutekeleza majukumu yake kama alivyoagizwa na kamati ya maandalizi ya mchezo huo iliyokuwa chini ya Leonard Thadeo.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam jana, Kaijage alisema hakubaliani na utaratibu uliotumiwa na kamati ya uchunguzi hasa namna ya kutoa taarifa zake baada ya kumaliza kazi iliyopewa na TFF.
Alisema kwa uzoefu wake na akiwa ameshuhudia kamati mbili zilizoundwa kuchunguza matukio ya timu ya taifa ya umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys kudanganya umri na waamuzi kula rushwa,mara baada ya kamati ya Mbwezeleni kumaliza uchunguzi wake ilitakiwa kuwasilisha taarifa TFF ambao ndio walitakiwa kuchukua hatua.
"Mimi sikuwa mwajiriwa wa kamati bali TFF,ilichotakiwa kufanya kamati ni kuikabidhi TFF taarifa badala ya wao kuutangazia umma,"alisema Kaijage.
Kaijage alisema ameshindwa kuyaelewa matokeo ya kamati hiyo hasa kwa kuwa ni wajumbe wawili tu kati ya watano walioteuliwa ndio alionana nao kwa ajili ya mahojiano.
"Sote tunajua kamati ilikuwa na wajumbe watano walioteuliwa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga, kimsingi kamati ilinihoji mara mbili, mara ya kwanza ilikuwa Jumanne Januari 25 kuanzia saa sita 6 mchana na mara ya pili ilikuwa Februari 12, 2011, mara zote mbili ni mwenyekiti na katibu wa kamati ndiyo walionihoji. Sikutarajia mara zote mbili wajumbe wangekuwa wawili tu hasa ukizingatia tayari TFF ilikuwa imenitaja kama mhusika mkuu,"alisema Kaijage.
Alisema hata shahidi aliyeelezwa na kamati kwamba alidanganya kwa nia ya kuwapumbaza wajumbe yeye hakuwahi kumwita wala kumpendekeza na kudai kama shahidi alifanya hivyo ilikuwa ni kwa matakwa yake.
Aidha, alisema ameshangazwa na kitendo cha kuondoka kwa fundi ambaye ni raia wa China kwenye mitambo na kuonekana ni kosa la lake yeye (Kaijage).
"Ifahamike kuwa fundi huyo wa mitambo alikuwa anaonana na ofisa habari siku ya mchezo kwa sababu ndiyo sehemu yake ya kazi na uhusiano baina yetu ni kwenye mitambo, pia tukumbuke kwamba hajui Kiingereza zaidi ya Kichina, sasa najiuliza kama alikuwa anamtafuta Kaijage alimuuliza nani na yeye anaongea Kichina tu? Kosa langu hapa ni lipi,ili ni swali ambalo halina jibu,"alisema Kaijage.
Katika mechi hiyo ambayo iliyoshuhudiwa pia na Rais Jakaya Kikwete, CD iliyopaswa kupigwa nyimbo za taifa za Morocco na Tanzania ziligoma na kusababisha shughuli hiyo kufanywa kipindi cha pili cha mchezo, hivyo Tenga kutangaza kumsimamisha kazi kwa Kaijage .
PRINT