Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Taswa FC yapigwa jeki

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:50 Imesomwa na watu: 15; Jumla ya maoni: 0








HOTELI mpya ya New Avon imetangaza kuidhamini timu ya soka ya waandishi wa habari za michezo nchini, Taswa FC .

Mkurugenzi Mtendaji wa New Avon Shaheed Dhanani alisema kuwa wanatambua mchango mkubwa wa timu hiyo katika maendeleo ya soka na michezo nchini.

Shaheed alisema kuwa kwa vile wanaingia rasmi katika biashara ya hoteli na kutokana na ubora wa hoteli yao, wameamua kuisapoti timu hiyo na wanaamini watafanya vyema kupitia udhamini wao.

"New Avon Hotel itatoa jezi zenye thamani ya dola za Marekani 900 ambazo kwa sasa zinachapishwa huko Dubai, ni jezi za kisasa na zina ubora wa hali ya juu," alisema Shaheed.

Alisema kuwa mbali ya jezi, pia watatoa soksi kwa wachezaji ili waonekane nadhifu kama ilivyo hoteli yao ambayo ipo katika makutano ya mitaa ya Aggrey na Jamhuri (Mnazi Mmoja).

Alisema kuwa wanatarajia kuongoza katika soko la hoteli nchini kutokana na huduma zao na ubora wa hoteli hiyo na ndiyo maana wameamua kuidhamini Taswa FC ikiwa ni timu bora ambayo toka kuanza kwa mwaka huu haijafungwa.

Mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary aliipongeza New Avon Hotel na kuahidi kutoa ushirikiano mkubwa katika kuinadi hoteli hiyo katika mechi na shughuli zake.

"Tunajivunia kuwa na New Avon Hotel, tunakubali msaada wao na tunaahidi kufanya vyema katika mechi zetu kupitia msaada wa hoteli hiyo, " alisema Majuto.
 
Polisi Arusha yaongoza netiboli Morogoro

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:45 Imesomwa na watu: 21; Jumla ya maoni: 0



Habari Zaidi: Azam yapania kuishusha Yanga
Wasanii wahamasishwa kusaidia waathirika wa mabomu
Taswa FC yapigwa jeki
Polisi Arusha yaongoza netiboli Morogoro
Wenye ulemavu waandaliwa tamasha
Ngoma nzito fainali Daraja la Kwanza
Wanachama Yanga wazodoana
TFF yaahidi kulipa madeni
Kamati ya sakata la Kaijage yakamilisha uchunguzi
Ligi Tanzania mbovu-Fifa
Coastal Union yarejea Ligi Kuu Bara
Ray afagilia filamu yake mpya
Kalunde kujitambulisha mikoani
Kamuzora kuzikwa leo Bukoba
Ligi ya Taifa moto Morogoro
Kamati Tamasha la Pasaka kusaidia waathirika Gongo la Mboto
Simba kidali po, Yanga yatamba
JKT Oljoro yaingia Ligi Kuu, Villa yaona mlango
Toto yatibua hesabu za Simba
Yanga kumalizia hasira kwa Kagera

Habari zinazosomwa zaidi: Balaa lingine kwa Chenge
Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
‘Housigeli' anataka kuniharibia ndoa
Vatican yamvua jimbo Askofu
Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
TIMU ya Netiboli ya Polisi Arusha inayoshiriki Ligi Daraja la Pili ngazi ya Taifa katika mashindano yanayofanyika mkoani Morogoro imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika kundi B baada ya kuifunga timu ngumu ya Ruvu JKT mabao 25-17.

Mchezo huo wa kundi hilo ulifanyika jana asubuhi, ulitawaliwa kwa majigambo tambo na shamrashamra kutoka kwa baadhi ya wachezaji na mashabiki wa timu hizo kufuatia jezi zilizovaliwa na wachezaji wa pande hizo.

Timu ya Polisi Arusha ilivalia jezi za rangi nyekundu zinazotumiwa na timu ya soka ya Simba, ambapo Ruvu JKT yenyewe walivalia jezi za rangi ya njano ambazo pia huvaliwa na timu ya Yanga hali iliyosababisha ushangiliaji kuwa ni wa Yanga na Simba.

Hata hivyo mchezo huo ulikuwa wa vuta nikuvute na ufundi mwingi kutoka kwa wachezaji wa pande zote ambapo hadi mapumziko Polisi Arusha ilikuwa mbele kwa mabao 12-9 ya wapinzani wao.

Timu hizo katika kipindi cha pili zilicheza kufa na kupona, lakini vijana wa Polisi Arusha walikitawala kipindi hicho kwa kuongeza mabao mengine 13 dhidi ya 8 ya wapinzani wao.

Hadi mchezo huo unamalizika Polisi Arusha walijipatia mabao hayo 25 -17, hata hivyo Ruvu ilipata pigo baada ya mshambuliaji wao mahiri kuumia kabla ya mapumziko.

Mshambuliaji na mfungaji huyo mahiri wa timu hiyo, Jawa Iddi aliumia mkono wa kushoto ambapo kipindi cha pili alicheza dakika chache na kutoka nje na nafasi yake ilichukuliwa na Zainab Lukindo.

Katika mchezo mwingine ulikuwa na ushindani mkubwa uliofanyika awali ulikuwa ni kati ya timu ya Mzinga na Alliance One , zote za mkoani hapa ambapo timu ya Mzinga ilishinda mchezo huo kwa kuifunga Alliance One mabao 23- 19.

Hadi timu hizo zilizochuana vikali katika kipindi hicho cha kwanza zinakwenda mapumziko zilikuwa sare kwa mabao 11- 11 .

Kwa upande wake nahodha wa timu ya Ruvu JKT Anna Masaga akizungumzia mchezo dhidi ya wapinzani wao alisema ulikuwa mzuri na wamefungwa kutokana na makosa madogo madogo yaliyojitokeza.

Hata hivyo alisema wanashukuru kushika nafasi ya pili katika kundi lao hilo, baada ya kushinda michezo mitatu na kufungwa mmoja na Polisi Arusha, ambapo alizitaja timu walizozifunga ni Tandahimba mabao 40-20, Black Sisters mabao 47- 10 na Tigo kwa mabao 30-14 .

Naye Nahodha wa timu ya Polisi Arusha, Jackline Kishimbo, alisema ligi hiyo imekuwa na ushindani ambapo katika mchezo huo na Ruvu JKT waliweza kutulia na kufanya mashambulizi ya kujipanga hasa katika kipindi cha pili na kuibuka kidedea.

Kwa mujibu wa Nahodha huyo, kufuatia matokeo hayo, Polisi Arusha imeongoza kundi hilo baada ya kushinda michezo yake yote kwa kuzifunga timu ya Tigo mabao 25-14, Tandahimba 25- 6, Black Sister mabao 35-6 na Ruvu JKT kwa mabao 25-17.

Hivyo alisema kuwa wanasubiri utaratibu mwingine wa waandaaji wa mashindano hayo kuweza kupangwa kwenye hatua ya robo fainali.
 
Polisi Arusha yaongoza netiboli Morogoro

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:45 Imesomwa na watu: 21; Jumla ya maoni: 0


TIMU ya Netiboli ya Polisi Arusha inayoshiriki Ligi Daraja la Pili ngazi ya Taifa katika mashindano yanayofanyika mkoani Morogoro imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika kundi B baada ya kuifunga timu ngumu ya Ruvu JKT mabao 25-17.

Mchezo huo wa kundi hilo ulifanyika jana asubuhi, ulitawaliwa kwa majigambo tambo na shamrashamra kutoka kwa baadhi ya wachezaji na mashabiki wa timu hizo kufuatia jezi zilizovaliwa na wachezaji wa pande hizo.

Timu ya Polisi Arusha ilivalia jezi za rangi nyekundu zinazotumiwa na timu ya soka ya Simba, ambapo Ruvu JKT yenyewe walivalia jezi za rangi ya njano ambazo pia huvaliwa na timu ya Yanga hali iliyosababisha ushangiliaji kuwa ni wa Yanga na Simba.

Hata hivyo mchezo huo ulikuwa wa vuta nikuvute na ufundi mwingi kutoka kwa wachezaji wa pande zote ambapo hadi mapumziko Polisi Arusha ilikuwa mbele kwa mabao 12-9 ya wapinzani wao.

Timu hizo katika kipindi cha pili zilicheza kufa na kupona, lakini vijana wa Polisi Arusha walikitawala kipindi hicho kwa kuongeza mabao mengine 13 dhidi ya 8 ya wapinzani wao.

Hadi mchezo huo unamalizika Polisi Arusha walijipatia mabao hayo 25 -17, hata hivyo Ruvu ilipata pigo baada ya mshambuliaji wao mahiri kuumia kabla ya mapumziko.

Mshambuliaji na mfungaji huyo mahiri wa timu hiyo, Jawa Iddi aliumia mkono wa kushoto ambapo kipindi cha pili alicheza dakika chache na kutoka nje na nafasi yake ilichukuliwa na Zainab Lukindo.

Katika mchezo mwingine ulikuwa na ushindani mkubwa uliofanyika awali ulikuwa ni kati ya timu ya Mzinga na Alliance One , zote za mkoani hapa ambapo timu ya Mzinga ilishinda mchezo huo kwa kuifunga Alliance One mabao 23- 19.

Hadi timu hizo zilizochuana vikali katika kipindi hicho cha kwanza zinakwenda mapumziko zilikuwa sare kwa mabao 11- 11 .

Kwa upande wake nahodha wa timu ya Ruvu JKT Anna Masaga akizungumzia mchezo dhidi ya wapinzani wao alisema ulikuwa mzuri na wamefungwa kutokana na makosa madogo madogo yaliyojitokeza.

Hata hivyo alisema wanashukuru kushika nafasi ya pili katika kundi lao hilo, baada ya kushinda michezo mitatu na kufungwa mmoja na Polisi Arusha, ambapo alizitaja timu walizozifunga ni Tandahimba mabao 40-20, Black Sisters mabao 47- 10 na Tigo kwa mabao 30-14 .

Naye Nahodha wa timu ya Polisi Arusha, Jackline Kishimbo, alisema ligi hiyo imekuwa na ushindani ambapo katika mchezo huo na Ruvu JKT waliweza kutulia na kufanya mashambulizi ya kujipanga hasa katika kipindi cha pili na kuibuka kidedea.

Kwa mujibu wa Nahodha huyo, kufuatia matokeo hayo, Polisi Arusha imeongoza kundi hilo baada ya kushinda michezo yake yote kwa kuzifunga timu ya Tigo mabao 25-14, Tandahimba 25- 6, Black Sister mabao 35-6 na Ruvu JKT kwa mabao 25-17.

Hivyo alisema kuwa wanasubiri utaratibu mwingine wa waandaaji wa mashindano hayo kuweza kupangwa kwenye hatua ya robo fainali.
 
Wenye ulemavu waandaliwa tamasha

Imeandikwa na Elizabeth John, MIJO; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:40 Imesomwa na watu: 12; Jumla ya maoni: 0








KAMPUNI ya kukuza na kutangaza vipaji vya wasanii wenye ulemavu CHESCO PROMOTERS and DISTRIBUTORS (CDP) iliyopo Tabata imeanzisha tamasha la kuonesha vipaji vya watu wenye ulemavu kwa lengo la kuvikuza na kuviendeleza ili waweze kujiajiri wenyewe hali itakayowafanya kumudu maisha yao na kuondokana na utegemezi ambao ndio chanzo kikubwa cha umasikini.

Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Joseph Magutu walemavu wana vipaji vingi ambavyo vikitumiwa vizuri vitawasaidia kutatua matatizo yao.

Mfano ombaomba, wakiendelezwa kutokana na vipaji vyao wanaweza kuondokana na tabia hiyo.

"Watu binafsi na mashirika wamekuwa wakiwasaidia chakula na mahitaji madogomadogo, lakini sisi tumeona tuwawezeshe kukuza kile walichonacho kiwasaidie siku zote za maisha yao," alisema katika taarifa hiyo Magutu.

"Mtu akikuomba samaki usimpe samaki bali unatakiwa umfundishe kuvua,"aliongeza. "Katika kutekeleza sehemu ya malengo yetu tunaandaa tamasha la wasanii wenye ulemavu na wasio na ulemavu ili kuweza kufanikisha malengo yetu tuliyonayo" .

Aidha, Magutu alisema wanaomba wadhamini ambao wapo tayari kushirikiana nao wajitokeze ili waweze kufanikisha malengo yao na kwamba wanatoa shukrani zao kwa Rais Kikwete pamoja na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Serikali kwa ujumla kwa ushirikiano wanaowapatia katika kutatua matatizo yanayowakabili.
 
Ngoma nzito fainali Daraja la Kwanza

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:35 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0






FAINALI za Ligi Daraja la Kwanza zinatarajiwa kuendelea tena kesho kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga ambapo Villa Squard itamenyana na Prisons Mbeya.

Timu tisa ndizo zinazoshiriki ligi hiyo na timu nne za juu ndizo zitakazopanda daraja na kucheza Ligi Kuu msimu wa 2011/2012.

Mpaka sasa JKT Oljoro na wenyeji Coastal Union ndizo zilizopanda Ligi kuu baada ya JKT kufikisha pointi 15 na Coastal 13.

Kabla ya mechi ya kesho Villa ina pointi 11 na Prisons ina pointi nane, hivyo endapo Villa itashinda mechi ya kesho itafikisha pointi 14 na kuishusha Coastal katika nafasi ya pili.

Nafasi ya tatu inashikwa na Rhino ya Tabora yenye pointi 11 pia lakini ikiwa tayari imeshamaliza mechi zake.

Hata hivyo Coastal bado ina mechi moja mkononi dhidi ya TMK United ambayo iko nafasi ya pili kutoka chini ikiwa na pointi sita.

Aidha mechi nyingine itakayochezwa kesho ni kati ya Moro United dhidi ya Morani FC. Moro ina pointi 10 na ikishinda mechi yake ya leo dhidi ya Morani inayoshika mkia itafikisha pointi 13 sawa na Coastal Union.

Hata kama Coastal Union itafungwa mchezo wake wa mwisho dhidi ya TMK United na ikazidiwa uwiano wa mabao na Moro United, bado itapanda daraja kwa sababu timu ya kwanza itakuwa JKT Oljoro, ya pili Villa Squard ambayo itakuwa na pointi 14 kama ikiifunga Prisons na ya tatu Moro United kama ikiifunga Morani.

Lakini kama Villa Squard ikifungwa na Prisons yenye pointi nane zote zitakuwa na pointi 11 na kisha Moro ikafungwa na Morani na Coastal ikafungwa na TMK, Polisi Moro ikaifunga JKT Oljoro, timu zitakazopanda daraja zitakuwa ni JKT Oljoro, Coastal Union, na Polisi Moro na timu ya nne itategemea kati ya Villa, Prisons na Rhino ambazo zote zitakuwa na pointi 11.

Polisi Moro ina pointi tisa baada ya juzi kuifunga Prisons na ina mechi moja dhidi ya JKT Oljoro ambayo kama ikishinda itafikisha pointi 12 ambazo kupanda kwake daraja kutategemea na moja kati ya Moro United au Villa ziboronge mechi zao za mwisho.

 
Wanachama Yanga wazodoana

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:30 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0








BAADHI ya wanachama wa Yanga wamesikitikia kitendo cha wanachama wenzao kuitisha mkutano leo huku Taifa likiwa kwenye maombolezo ya waathirika wa mabomu ya Gonga la Mboto.

Zaidi ya watu 20 wamefariki na 100 wamejeruhiwa kutokana na milipuko ya mabomu kutoka kambi ya Jeshi ya Gongo la Mboto yaliyotokea mwanzoni mwa wiki hii na watoto kadhaa kupoteana na wazazi wao.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana zinadai kuwa wanachama wa Yanga Temeke wanatarajia kukutana leo lengo likuwa kuzungumzia hatima ya kujiondoa kwa mfadhili wao Yusuf Manji na suala la kutoelewana kwa Mwenyekiti Llyod Nchunga na Makamu wake Davis Mosha.

Akizungumza kwenye ofisi za gazeti hili mwanachama mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alisema kwa kipindi hiki hadhani kama ni wakati muafaka wa kuitisha mikutano.

"Hatukatai ndio Mwenyekiti wetu na Makamu wake wana tofauti, lakini kesho (leo) sio mahali pake pa kulifanya hilo, sasa hivi watu wapo maombolezo, hili lililotokea ni janga la kitaifa, inafaa tuwe na roho za imani jamani,"alisema.

Mfadhili wa Yanga Manji alitangaza kujiondoa kwenye klabu hiyo hali ambayo imewagawa wanachama wa klabu hiyo, wengine wakisema mfadhili huyo aondoke na wengine wakimtaka arudi.

Aidha mwanachama huyo aliyeongozana na wenzake 10 alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa wamegudua mkutano huo pia una lengo la kumchafua Makamu Mwenyekiti Mosha.

"Sisi tunajua kuna watu wana hila, wanataka kwenye mkutano huo wamchafue Mosha kwamba hana elimu na hawezi kuongoza Yanga, sasa hapo tunajenga tunabomoa, kila siku tunasema Makamu na Mwenyekiti wapatane, leo wanaibuka watu wanaanzisha zogo,"alisema.

Gazeti hili lilimtafuta Nchunga kutaka kujua kama kweli mkutano huo utakuwepo leo hasa baada ya kudaiwa kuwa yeye ndio atakuwa mgeni rasmi, lakini simu yake ya mkononi iliita bila mafanikio.

Lilipomtafuta Makamu Mosha, alisema hana taarifa za mkutano huo. "Ninachoweza kusema ni kwamba mimi kama Makamu Mwenyekiti sina taarifa za mkutano huo wa Temeke kesho (leo), na hilo suala la kunijadili kwamba sina cheti cha kidato cha nne... halina ukweli lakini siwezi kumzuia mtu kuzungumza vile anavyodhani katika kichwa chake,"alisema.
 
TFF yaahidi kulipa madeni

Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:25 Imesomwa na watu: 20; Jumla ya maoni: 0



Habari Zaidi: Azam yapania kuishusha Yanga
Wasanii wahamasishwa kusaidia waathirika wa mabomu
Taswa FC yapigwa jeki
Polisi Arusha yaongoza netiboli Morogoro
Wenye ulemavu waandaliwa tamasha
Ngoma nzito fainali Daraja la Kwanza
Wanachama Yanga wazodoana
TFF yaahidi kulipa madeni
Kamati ya sakata la Kaijage yakamilisha uchunguzi
Ligi Tanzania mbovu-Fifa
Coastal Union yarejea Ligi Kuu Bara
Ray afagilia filamu yake mpya
Kalunde kujitambulisha mikoani
Kamuzora kuzikwa leo Bukoba
Ligi ya Taifa moto Morogoro
Kamati Tamasha la Pasaka kusaidia waathirika Gongo la Mboto
Simba kidali po, Yanga yatamba
JKT Oljoro yaingia Ligi Kuu, Villa yaona mlango
Toto yatibua hesabu za Simba
Yanga kumalizia hasira kwa Kagera

Habari zinazosomwa zaidi: Balaa lingine kwa Chenge
Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
‘Housigeli' anataka kuniharibia ndoa
Vatican yamvua jimbo Askofu
Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema kuwa muda mfupi ujao litazilipa hoteli zote ambazo zilitoa huduma ya malazi kwa timu zilizoshiriki Michuano ya Kombe la Chalenji mwishoni mwa mwaka jana.

Akizungumza na HABARILEO Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah ‘Ngeta' alisema kuwa zoezi la kuwalipa litafanyika hivi karibuni na kuzitaka hoteli hizo kuwa na subira.

Ngeta alisema kuwa kulikuwa na sababu mbalimbali zilizopelekea kucheleweshwa kwa malipo hayo na kuongeza kuwa kwa sasa kila kitu kipo sawa.

Alisema, kuna baadhi ya hoteli ambazo zimekuwa zikifuatilia malipo hayo ambayo ni ya kiwango tofautitofauti.

Bila ya kutaja kiwango cha fedha ambacho TFF inadaiwa, Ngeta alisema kuwa anatambua usumbufu unaoweza kuwa umejitokeza kwa kucheleweshewa malipo yao hayo.

"Ni kwamba karibia kila kitu kitaenda sawa na pia ifahamike kuwa zipo hoteli nyingi ambazo tulizitumia kuwahifadhi wachezaji hawa na pia kila moja itakamilishiwa taratibu zake za malipo," alisema Angetile.

Februari 18 Maofisa kutoka hoteli za Wanyama na Johannesburg zilizopo Sinza walikuwa wakilalamika kucheleweshewa malipo yao hayo.

Bila ya kutaka kutaja majina yao na kiasi wanachodai waliliambia gazeti hili kuwa wamekuwa wakifuatilia malipo hayo kwa muda katika ofisi hizo za TFF.

Hoteli takribani 11 zilitumika kuhifadhi timu kutoka nchi 11 zilizoshiriki michuano hiyo iliyochukua siku 14 karibia kila timu ilikuwa na watu 23.


 
TFF yaahidi kulipa madeni

Imeandikwa na Evance Ng’ingo; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:25 Imesomwa na watu: 20; Jumla ya maoni: 0


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema kuwa muda mfupi ujao litazilipa hoteli zote ambazo zilitoa huduma ya malazi kwa timu zilizoshiriki Michuano ya Kombe la Chalenji mwishoni mwa mwaka jana.

Akizungumza na HABARILEO Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah ‘Ngeta’ alisema kuwa zoezi la kuwalipa litafanyika hivi karibuni na kuzitaka hoteli hizo kuwa na subira.

Ngeta alisema kuwa kulikuwa na sababu mbalimbali zilizopelekea kucheleweshwa kwa malipo hayo na kuongeza kuwa kwa sasa kila kitu kipo sawa.

Alisema, kuna baadhi ya hoteli ambazo zimekuwa zikifuatilia malipo hayo ambayo ni ya kiwango tofautitofauti.

Bila ya kutaja kiwango cha fedha ambacho TFF inadaiwa, Ngeta alisema kuwa anatambua usumbufu unaoweza kuwa umejitokeza kwa kucheleweshewa malipo yao hayo.

“Ni kwamba karibia kila kitu kitaenda sawa na pia ifahamike kuwa zipo hoteli nyingi ambazo tulizitumia kuwahifadhi wachezaji hawa na pia kila moja itakamilishiwa taratibu zake za malipo,” alisema Angetile.

Februari 18 Maofisa kutoka hoteli za Wanyama na Johannesburg zilizopo Sinza walikuwa wakilalamika kucheleweshewa malipo yao hayo.

Bila ya kutaka kutaja majina yao na kiasi wanachodai waliliambia gazeti hili kuwa wamekuwa wakifuatilia malipo hayo kwa muda katika ofisi hizo za TFF.

Hoteli takribani 11 zilitumika kuhifadhi timu kutoka nchi 11 zilizoshiriki michuano hiyo iliyochukua siku 14 karibia kila timu ilikuwa na watu 23.


 
Ligi Tanzania mbovu-Fifa

Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 18th February 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 587; Jumla ya maoni: 0






SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (FIFA) limesema haliridhishwi na Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara kwani haina kiwango bora.

Kauli hiyo ilitolewa na mwakilishi wa Fifa katika nchi za Kusini mwa Afrika, Ashford Mamelody wakati wa ufungaji semina ya siku tano iliyowashirikisha viongozi wa klabu zinazoshiriki ligi hiyo pamoja na maofisa habari na viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Alisema ligi hiyo haina mvuto na kuongeza kuwa inatakiwa kuongezwa hamasa zaidi kwani sio ligi yenye msisimko kama ambavyo ingetakiwa.

Alieleza kuwa ili Tanzania iweze kushiriki fainali za Kombe la Dunia ikiwa pamoja na Kombe la Afrika ni vyema ikawekeza zaidi katika ligi hiyo.

Kwa mujibu wa kigogo huyo wa Fifa kama Ligi Kuu ikiwa bora inaweza kutoa wachezaji wengi wa kucheza katika klabu kubwa za nje ya nchi, ambao wataisaidia timu ya Taifa.

Naye Rais wa TFF Leodegar Tenga akizungumza kwenye ufungaji huo, alikubaliana na changamoto alizozitoa Mamelodi na kufafanua kuwa ligi hiyo inatakiwa kuwekewa hamasa zaidi.

Alisema inatakiwa kuwa ligi yenye nguvu na msisimko zaidi ya ilivyo sasa.

Akizungumzia makubaliano waliyofikia katika semina hiyo, alisema kila klabu inayoshiriki ligi hiyo iwe na ofisi pamoja na kufanyiwa ukaguzi wa mara kwa mara.
 
Kamati ya sakata la Kaijage yakamilisha uchunguzi

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th February 2011 @ 23:00 Imesomwa na watu: 20; Jumla ya maoni: 0








KAMATI maalumu iliyopewa kazi ya kuchunguza sakata la kugoma kupigwa kwa nyimbo za taifa katika mechi kati ya timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars na Morocco imeshakamilisha kazi hiyo.

Sakata hilo lilitokea Oktoba mwaka jana katika mechi hiyo ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika 2012 ambapo wimbo uligoma kuchezwa wakati Rais Jakaya Kikwete akiwa tayari ameshuka jukwaani kwa kusubiria wimbo huo.

Kitendo hicho ndicho kilichomlazimu Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodegar Tenga kuunda Kamati itakayochunguza chanzo cha sakata hilo.

Kamati hiyo inaongozwa na Mwanasheria Hamidu Mbwezeleni ambaye aliliambia gazeti hili kuwa tayari Kamati yake imeshakamilisha kazi hiyo.

"Kamati yangu imeshamaliza kazi iliyotumwa na Rais Tenga na muda wowote kuanzia sasa itakuwa tayari kuzungumza na waandishi wa habari kuutaarifu uma kitu gani kilitokea mpaka Rais akadhalilika kiasi kile,"alisema.
 
Spanish La Liga Roundup, Feb. 19


storypage_APlogo_01.png




PRINT RSS

67 comments »

Updated Feb 19, 2011 5:54 PM ET
Real Madrid provisionally moved to within two points of league leader Barcelona by beating Levante 2-0 on Saturday.
Karim Benzema scored Madrid's sixth-minute opener after a great individual effort from Angel Di Maria, and Ricardo Carvalho sealed the win four minutes before halftime.
Scores | Fixtures | Table | Stats Scores | Fixtures | Table | Stats Scores | Fixtures | Table | Stats Scores | Fixtures | Table | Stats Scores | Fixtures | Table | Stats Scores | Fixtures | Table | Stats

Madrid's 12th victory in as many games at Santiago Bernabeu stadium increases the pressure on Barcelona to beat Athletic Bilbao on Sunday.
The win also extended coach Jose Mourinho's nine-year unbeaten run at home. The last time the former Chelsea and Inter Milan manager lost at his home ground was when FC Porto fell to Beira Mar 3-2 in February 2002.
With the first leg of its Champions League round of 16 match against Lyon set for Tuesday, Mourinho rested midfielder Xabi Alonso, defender Pepe and striker Emmanuel Adebayor, who came on late as a substitute. Goalkeeper Antonio Adan also made his first start in Spain's top division with Madrid captain Iker Casillas serving a one-game suspension.
Even though Madrid had routed Levante 8-0 in their last meeting in the Spanish capital in the Copa del Rey, Levante had drawn with Madrid in their first league fixture and won the second leg of their Copa del Rey match, making the minnow one of just three teams to beat Mourinho's squad this campaign.
Luis Garcia's team had also won a club record three straight games, but Madrid quickly banished any thoughts of an upset.
Benzema, who had lost his spot in the starting 11 with Adebayor's arrival in January, wasted little time in putting Madrid ahead when Di Maria dribbled through three defenders before crossing for the France striker to redirect into goal.
Cristiano Ronaldo grazed the top of the goal with a header in the 16th, and Levante goalkeeper Gustavo Munua made two excellent saves from shots by Di Maria and Benzema in the 22nd and 24th as the hosts pressed to put the game away.
But it was center back Carvalho who slid unmarked into the six-yard box to stab home Ronaldo's free kick after Di Maria had provoked a foul on the left edge of the box.
Munua denied Madrid a third goal with back-to-back saves from a header by Ronaldo and a hard volley by Benzema in the 65th.
Ronaldo kept firing away, but Munua was there to block the Portuguese forward's two clear attempts late in the contest.
Earlier, Valencia drew 0-0 with Sporting Gijon.
After a disappointing draw with Schalke in the Champions League midweek, Valencia dominated possession but could not convert any chances to be held scoreless for the first time at Mestalla stadium this season.
"It is true we were not fresh," Valencia coach Unai Emery said. "We did not move the ball enough and we did not have precision in our one-on-one situations."
Valencia remained undefeated in 10 games, but is only three points clear of fourth-place Villarreal.
Sporting, which last week ended Barcelona's league-record winning streak of 16 games with a 1-1 draw, has only lost once in six weeks.
Valencia's top goal scorer, Aritz Aduriz, injured his ankle in the second half and Brazilian striker Jonas Goncalves, who joined the team in the winter transfer window, debuted for Valencia as his substitute.
Later, Atletico Madrid tries to break its four-game losing streak in its trip to Zaragoza.
Also on Sunday, it's: Getafe vs. Racing Santander, Villarreal vs. Malaga, Almeria vs. Deportivo La Coruna; Osasuna vs. Espanyol, and Sevilla vs. Hercules.
Mallorca is at Real Sociedad on Monday to close round 24.
 
Saturday, February 19, 2011​
Week 24​

Mestalla
Expand
expandInfo.jpg


0 : 0
Final




Match Stats | Match Trax
Goals
yellow-card.gif
(56') Mehmet Topal
Cards
greenArrow.gif
(55') Roberto Soldado
redArrow.gif
Alejandro Domínguez

greenArrow.gif
(69') Pablo Hernández
redArrow.gif
Juan Manuel Mata

greenArrow.gif
(79') Gonçalves Oliveira
redArrow.gif
Aduriz

Substitutions Mate Bilić (72')
greenArrow.gif

Gastón Sangoy
redArrow.gif


Nacho Novo (83')
greenArrow.gif

De las Cuevas
redArrow.gif


José Ángel (89')
greenArrow.gif

Diego Castro
redArrow.gif



Santiago Bernabéu
Expand
expandInfo.jpg


2 : 0
Final




Match Stats | Match Trax
goal.gif
(7') Karim Benzema
goal.gif
(41') Ricardo Carvalho
Goals
yellow-card.gif
(31') Sergio Ramos
yellow-card.gif
(58') Lassana Diarra
Cards Felipe Caicedo (45')
yellow-card.gif

Sergio Ballesteros (83')
yellow-card.gif

greenArrow.gif
(76') Mesut Özil
redArrow.gif
Kaká

greenArrow.gif
(76') Emmanuel Adebayor
redArrow.gif
Ángel Di María

greenArrow.gif
(85') Fernando Gago
redArrow.gif
Karim Benzema

Substitutions Jefferson Montero (61')
greenArrow.gif

Xisco Muñoz
redArrow.gif


Stuani (72')
greenArrow.gif

Felipe Caicedo
redArrow.gif


Lois (79')
greenArrow.gif

Xavi Torres
redArrow.gif



La Romareda
Expand
expandInfo.jpg


0 : 1
Final




Match Stats | Match Trax
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom