AFRIKA KWETU
Member
- May 21, 2013
- 29
- 8
Mke wa Rais wa Marekani Bi. Michelle Obama, amepata usumbufu wa kurekebisha kigauni chake kifupi na chepesi kutokana na hali ya upepo iliyotawala katika maeneo mengi ya jiji la Dar es Salaam. Haya yametokea katika uwanja wa ndege wa Mwl. Julius K. Nyerere wakati wa mapokezi ya Rais Obama uwanjani hapo. Michelle alionekana kukoswa utulivu kwani wakati wote mikono yake ilionekana kushughulikia uvutaji wa kigauni chake na kukirekebisha ili kikae sawa. Aidha, Michelle alionekana kuwa na kazi ya kuukabili upepo kwa kusimama katika mwelekeo utakaomsaidia kuikwepa aibu iliyokuwa inaelekea kumpata. Wakati huohuo, mwenyeji wake Mama Salma Kikwete alionekana kujiamini muda wote kwani kama ilivyo kawaida yake, alijisetiri ndani ya vazi lake la tenge la ukweli.