Michango imezidi RC

Michango imezidi RC

mchango wa mtoto yesu, kanisa katoriki lina vitega uchumi vingi sana ila naona kuna watu wanataka tushindane na haya makanisa yalioyoanzishwa siku hizi imefikia kuna watu wanaogopa kwenda kanisani kwa kuogopa kudhalilika kwa kutotoa michango
 
Duuuh jpm kagusa mpaka misikiti na makanisa ?

Wakati ule issue kama bima za mapadre ilikuwa anafuatwa fisadi fulani anamaliza kila kitu
Sasa hivi utaanzaje kumfuata yeye mwenyewe anataka achangiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiamka mara sijui tengeneza nini, ukihema mara sijui bima ya kina nani, ukikohoa mara zaka yani ni shida, imefikia kipindi watu tunapangiana kwamba kila familia ni LAZIMA ITOE LAKI KADHAA Bila kujali kipato chache.. Huu ni utumwa na unyonyaji wa mchana kweupe.Nachokiona watakatifu (mapadre na viongozi wadini) wanataka kuishi kitakatifu zaidi na kwa anasa huku kwa kutumia jasho la waumini.shida sana itabd watu waanzishe dini za familia.
Duh, nilikuwa ninataka kuhamia huko toka kkkt sababu ya michango, sasa ngoja nianze fikiria TAG.
 
Kwa muda mrefu Catholic Churches nchini zilikuwa zinafadhiliwa na mashirika mengi tajiri ya Kikatoliki.

Sasa misaada hiyo imekoma maana makanisa ni mengi.

Kwa makanisa ya KKKT hali hii wamesha zoea, kuikubali, na kuendelea na michango mikubwa na mingi inayolijenga kanisa.

Mkristo jiulize hao wamissionari wslifikaje huku kwetu?
Ni kwa kutumia pesa za sadaka za wengine huko walikotoka.

Ni ukweli usiopingika kuwa sasa wamechoka, msimamo wao makanisa duniani wajitegemee, hii ni pamoja na vijana wengi Europe, Marekani na wafadhili wengine, kuiasi dini.
Hivyo hata huko makanisa yana sinyaa.
Huko Marekani na Uingereza Makanisa yanageuzwa ofisi, bar na studios au hata night clubs.

Kijana endelea kujitolea kadri uwezavyo ili Neno la Mungu liendelee kuhubiriwa duniani kote.
hao wamissionari ndio usiwataje ni washenzi tu walikuja kusaidia Afrika kutawaliwa mbona sasa hivi huko kwao ndio wanaunga mkono ushoga uliokatazwa na maandiko matakatifu
 
Toa kwa kadri ya uwezo wako. Halafu sadaka na zaka ya kweli inanzia ndani ya familia yako, ndugu na jamii inayokuzunguka
Haingii akilini familia yako inakosa huduma ndugu, majirani na jamaa zako wanakufa kwa njaa na maradhi wewe ukobusy na michango ya kanisa. Aysee hutaenda mbingu
 
hao wamissionari ndio usiwataje ni washenzi tu walikuja kusaidia Afrika kutawaliwa mbona sasa hivi huko kwao ndio wanaunga mkono ushoga uliokatazwa na maandiko matakatifu
Wewe unaongelea sasa, mimi nimeonglea miaka 150 iliyopita.
 
Kwanza inabidi ujiulize kama mungu yeye ndio aliumba vitu vyote kwanini mumuchangie hela zote hizo?

Sent from my SM-G950F using Tapatalk
Kuna kitu kinaitwa blind faith, waamini wa dini hawajiulizi zaidi ya wanachofundishwa na dini zao.

Huo uninga niliacha
 
(Kwanza na declare interest mimi ni mkatoliki)

Shida hapa naona ni IMANI tu. Wengi tuna imani haba!

Ni nani kati yetu anayetoa kama zaka sehemu ya kumi ya kipato chake cha mwaka? Kwa nini tunatoa pungufu?

Sadaka, zaka na michango mingine haijawahi kuwa ya lazima (i.e. hakuna adhabu kwa kushindwa kutoa) katika Kanisa. Pamoja na kuweka viwango kama sehemu ya administration, lakini bado hakuna adhabu kwa kushindwa kufikia viwango elekezi.
Lakini pua tujiulize, itakuwaje kama wakatoliki wote hatutaki kuchangia ujenzi wa makanisa yetu, hatutaki kuchangia harakati za kueneza injili kwengineko, hatutaki kutoa zaka, hatutaki kuwahudumia mapadri na watoa huduma wengine? Ni nani tunataka agharamie mambo hayo? Na wewe kama mkatoliki wajibu wako ni nini kwa kanisa na uinjilishaji?

Na kwa kweli hakuna dini ama dhehebu ambalo hakuna michango au majitoleo kabisa. Ukiona hakuna muchango ujue kuna watu wachache wanajitolea pakubwa kwa niaba ya wengine....but hiyo sio sustainable. Na angalau Kanisa Katoliki linaendeshwa kitaasisi na pesa tunazotoa zinaonekana katika majengo, miradi na huduma za kijamii. Huwezi hata linganisha madhehebu mengi mengine...ambayo Kanisa ni almost mali ya mtu mmoja na familia yake!

Kuna watu wapo tayari kulipia gesti sh40,000 na kulipa malaya hata sh50,000....lakini mwambie mchango wa ujenzi wa kanisa! Na mifano mingi mingine inayofanana na hiyo!

Wenzetu walikuwa tayari kutoa hata watoto wa pekee kama sadaka kwa Mungu......itakuwa sisi tunaotoa pesa tu!
 
Ukiamka mara sijui tengeneza nini, ukihema mara sijui bima ya kina nani, ukikohoa mara zaka yani ni shida, imefikia kipindi watu tunapangiana kwamba kila familia ni LAZIMA ITOE LAKI KADHAA Bila kujali kipato chache.. Huu ni utumwa na unyonyaji wa mchana kweupe.Nachokiona watakatifu (mapadre na viongozi wadini) wanataka kuishi kitakatifu zaidi na kwa anasa huku kwa kutumia jasho la waumini.shida sana itabd watu waanzishe dini za familia.
Watu kama nyinyi ndio mnaokwamisha maendeleo Na mnataka kufanyiwa kila kitu...bora hata Roman Na Lutheran Church walao waumini huona kile wachangiacho ni kwa manufaa ya kanisa kuliko kwenye baadhi ya makanisa kiroho ambapo waumini huchangia miradi ya wenye kanisa wachungaji nk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutoka 23:15
Kutoka 34:20
Kumbukumbu la Torati 16:16

Umtolee Mungu kiwango ambacho ni size yako ila sio kiwango cha dharau kwa Mungu...
Meneja mzima mzima, afisa mzima mzima unapeleka 200 kweeeeeli?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom