Michango imezidi RC

Michango imezidi RC

Umeongea ukweli mtupu alafu unashangaa mapadri wanaishi kitajiri sana majumba yao ni mazuri wanaendesha magari makali wanavaa vizuri kula vizuri kutibiwa hospitali kali nk wakati asilimia 80 ya hao waumini wafia dini ni masikini wa kutupwa mtu wewe kama wewe hujui hata familia yako kama wana bima ila ndo wa kwanza kimberembere kuchangisha bima ya mapadri zako. Unaambiwa akili za kuambiwa changanya na zako


Sent from my iPhone using JamiiForums
Sure wanataka wenyewe wawe na bima wakati asilimia kubwa ya waumini wao haziwezi kunilipia bima. Na kwenye matumizi yao utasikia milioni 200 zimetumika kununua funiture na kuweka A. C kwenye nyumba za mapadri hakuna ata senti inayorudi kwenye jamii.
 
Kwa muda mrefu Catholic Churches nchini zilikuwa zinafadhiliwa na mashirika mengi tajiri ya Kikatoliki.

Sasa misaada hiyo imekoma maana makanisa ni mengi.

Kwa makanisa ya KKKT hali hii wamesha zoea, kuikubali, na kuendelea na michango mikubwa na mingi inayolijenga kanisa.

Mkristo jiulize hao wamissionari wslifikaje huku kwetu?
Ni kwa kutumia pesa za sadaka za wengine huko walikotoka.

Ni ukweli usiopingika kuwa sasa wamechoka, msimamo wao makanisa duniani wajitegemee, hii ni pamoja na vijana wengi Europe, Marekani na wafadhili wengine, kuiasi dini.
Hivyo hata huko makanisa yana sinyaa.
Huko Marekani na Uingereza Makanisa yanageuzwa ofisi, bar na studios au hata night clubs.

Kijana endelea kujitolea kadri uwezavyo ili Neno la Mungu liendelee kuhubiriwa duniani kote.
Shida haipo kwenye kujitoa. Shida ipo kwenye kupangiana kiasi cha kutoa.
 
Ukiamka mara sijui tengeneza nini, ukihema mara sijui bima ya kina nani, ukikohoa mara zaka yani ni shida, imefikia kipindi watu tunapangiana kwamba kila familia ni LAZIMA ITOE LAKI KADHAA Bila kujali kipato chache.. Huu ni utumwa na unyonyaji wa mchana kweupe.Nachokiona watakatifu (mapadre na viongozi wadini) wanataka kuishi kitakatifu zaidi na kwa anasa huku kwa kutumia jasho la waumini.shida sana itabd watu waanzishe dini za familia.
"Mtu Hutoa Kama Vile Ameazimia Moyoni Mwake”

Badala ya kutaja kiasi hususa cha pesa, Paulo alipendekeza tu kwamba ‘kila mmoja atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake’ katika siku ya kwanza ya juma. (1 Wakorintho 16:2) Kwa kupanga na pia kutenga kando kiasi fulani kwa ukawaida, Wakorintho hawangehisi kwamba wanashurutishwa kutoa michango yao, wala hawangeitoa kwa sababu ya msisimuko tu wakati Paulo alipofika. Kila Mkristo angeamua kibinafsi ni kiasi gani angetoa, kulingana na ‘alichokuwa ameazimia moyoni mwake.’—2 Wakorintho 9:5, 7.

Wakorintho walihitaji kupanda kwa wingi ili wavune kwa wingi. Paulo hakusema lolote kuhusu kutoa kupita uwezo wa mtu. ‘Sikusudii iwe vigumu kwenu,’ Paulo akawahakikishia. Michango ‘ilikubalika hasa kulingana na alicho nacho mtu, si kulingana na kile ambacho mtu hana.’ (2 Wakorintho 8:12, 13; 9:6) Katika barua fulani aliyoandika baadaye, mtume alionya: “Ikiwa yeyote hawaandalii kitu . . . wale walio washiriki wa nyumbani mwake, ameikana imani naye ni mbaya zaidi kuliko mtu asiye na imani.” (1 Timotheo 5:8) Paulo hakuwahimiza watu watoe kwa njia iliyovunja kanuni hiyo.

Inafaa kuona kwamba Paulo alisimamia ukusanyaji wa ‘mchango kwa ajili ya watakatifu’ waliokuwa na uhitaji. Maandiko hayasemi popote pale kwamba Paulo au mitume wengine walipanga michango itolewe au walipokea fungu la kumi ili kugharimia huduma zao wenyewe. (Matendo 3:6) Paulo alishukuru daima kwa zawadi ambazo watu walimpelekea, naye alikuwa mwangalifu asiwatwike ndugu zake “mzigo ulemeao wenye gharama.”—1 Wathesalonike 2:9; Wafilipi 4:15-18.
 
Kwani mfano ukienda kusali na kutoka bila kuchanga watakuzuia kwenda tena Jumapili ijayo

Sent using Jamii Forums mobile app
Utasali tu, tatizo hii michango inadaiwa huku kwenye jumuiya. Nanusipoitoa inamaaana ata huduma za kanisani hutapata maana jumuiya ndo zinatunza hzo kumbukumbu
 
Sasa kama kutoa ni moyo s utajiri kwanini wafosi hadi wakuambie familia ya mzee fulan mtatoa laki, mara bima ya mapadre, mara mchango kwa ajili ya nini na wakati huo huo wanapga biashara, maana wana bank, wana redio, wana tv, wanahospitali wana shule na huko kote hupati huduma kama huna hela

Sent using Jamii Forums mobile app
Bima ya mapadre?? kanisa katoliki si lina mahospital dunia nzima? wanahitaji bima ya nini sasa
 
Ukiamka mara sijui tengeneza nini, ukihema mara sijui bima ya kina nani, ukikohoa mara zaka yani ni shida, imefikia kipindi watu tunapangiana kwamba kila familia ni LAZIMA ITOE LAKI KADHAA Bila kujali kipato chache.. Huu ni utumwa na unyonyaji wa mchana kweupe.Nachokiona watakatifu (mapadre na viongozi wadini) wanataka kuishi kitakatifu zaidi na kwa anasa huku kwa kutumia jasho la waumini.shida sana itabd watu waanzishe dini za familia.
mkuu jaribu kusoma roman empire ndio utaelewa catholic nini hasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa muda mrefu Catholic Churches nchini zilikuwa zinafadhiliwa na mashirika mengi tajiri ya Kikatoliki.

Sasa misaada hiyo imekoma maana makanisa ni mengi.

Kwa makanisa ya KKKT hali hii wamesha zoea, kuikubali, na kuendelea na michango mikubwa na mingi inayolijenga kanisa.

Mkristo jiulize hao wamissionari wslifikaje huku kwetu?
Ni kwa kutumia pesa za sadaka za wengine huko walikotoka.

Ni ukweli usiopingika kuwa sasa wamechoka, msimamo wao makanisa duniani wajitegemee, hii ni pamoja na vijana wengi Europe, Marekani na wafadhili wengine, kuiasi dini.
Hivyo hata huko makanisa yana sinyaa.
Huko Marekani na Uingereza Makanisa yanageuzwa ofisi, bar na studios au hata night clubs.

Kijana endelea kujitolea kadri uwezavyo ili Neno la Mungu liendelee kuhubiriwa duniani kote.
Umeeleza vema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza inabidi ujiulize kama mungu yeye ndio aliumba vitu vyote kwanini mumuchangie hela zote hizo?

Sent from my SM-G950F using Tapatalk
 
Nilijua ni huku niliko mimi tu kumbe kila mahali,yaani kwa hapa nilipo wanakuangalia biashara au kazi uliyonayo then unapangiwa kiasi unachopaswa kutoa,na hiyo inaanzia huku kwenye jumuiya.Wengi wanaacha kusali na wapo wanaohama madhehebu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom