Miaka zaidi ya 10 Baada ya Janga la Kikwete bado Watanzania hatujui tunataka Rais mwenye Sifa zipi!

Hili suala linaniumiza sana kichwa kila napofikiri. Mwaka 2005 nlikuwa nikifanya masomo yangu udsm wakati ambao kila kona vijana walikuwa na heka heka katika harakati za kuchagua rais.

Nakumbuka sana walivyokuwa wamejawa na kimuhemuhe cha kumchagua ndugu kikwete awe rais wa tanzania. Nlikuwa nikipenda kuwauliza vijana wenzangu na wasomi wa miaka hiyo.

Kwa nini hasa walipenda kumchagua kikwete kuwa rais? Majibu waliyotoa yalichoma moyo wangu kwa kiasi kikubwa sana.nliugua na kusononeka kutokana na majibu haya.
1. Ni kijana mwenzetu
2. Huwa anaenda klabu
3. Anaingia mpirani kutizama mpira na sisi
4. Anapenda sana kula bata
Wale walitoka bush wakaenda mbali zaidi na kusema ni hendisamu.

Nliukunyata moyo kwa masikitiko,majonzi na huzuni kubwa. Yaani Dr Salim A. Salim alionekana hafai. Hakuna aliyemfikiria kwa sababu hizi? Iliumiza sana moyo wangu. Tuliyokuja kuyapata Mungu mwenyewe anajua.

Ni mwendawazimu tu ambaye atamchukia magufuli na kumpenda kikwete. Ni mwendawazimu na pia mpumbavuh. Ashakum si matusi. Unawezaje leo kumchukia magufuli ukasema unampenda kikwete?

Ilhali magufuli anatokana na kile alichofanya kikwete? Ni wangapi tunakumbuka hata wapinzani walisema sasa anatakiwa apatikane rais dikteta?maana tulishachoka na kucheka cheka na nyani tukaishia kuvuna mabua?

Mungu aliwajaalia watanzania kuwa wasahaulifu na wanafiki sana.nadhani katika afrika kma si duniani watanzania ni watu wanafiki hawajawahi kutokea.ni hawa leo wanaomtetea patel,rugemalila na manji

Lakini ni hawa miaka kadhaa iliyopita walikuwa wakisema kwa uovu watu hawa. Ni watanzania hawa hawa ambao wanasema wanamtaka membe awe rais.katika watu wote...membe? Huyu huyu aliyekuwa akiandikwa kwa kashfa nyingi humu JF?

kikwete aliharibu dhana nzima ya Urais tanzania. Akaleta Urahis. Urais ukaonekana ni kitu Rahis. Ni muda wa kutembea dunia nzima kuomba omba...na watu kweli kama watoto wamfuatavyo baba hawakuona thamani ya kazi au kusoma.

Walidumbukia kwenye utumiaji na uuzaji wa madawa ya kulevya.ikawa ajira rasmi kabisa.kwani ninani asiyefaham ajira hii ilivyotajirisha wakubwa kwa wadogo? Wenye vyeo na wasio na vyeo?

Ni kipindi ambacho kuiba mali au pesa ya umma ilikuwa ishara ya ujanja na mafanikio.na wezi wapo mpaka leo waliogawana pesa za watanzania.huku rais wao akisema akiwakamata nchi itayumba.kauli ya hovyo kupata kusemwa na mtu ambaye tumempa dhamana ya urais.

Miaka zaidi ya 10 baada ya kupitwa na janga hilo bado watanzania hatujui tunataka rais wa namna gani.wanakuja watu kusifia kuwa flani anafaa kuwa rais sababu ni mpole, hana makuu,mnyenyekevu, mtanashati n.k

Ni wazi bado vijana wengi na hta wazee ukiwauliza mnataka rais wa namna gani wasijue. Watakosa sifa au watataja tena sifa za majanga mengine ya kitaifa hapa nchini.watanzania tunasahau sana.

Pengine kwa umbumbumbu au kwa kutumika na baadhi ya watu. Na katika hili tumeweza hata kuondoa Unyeti wa taasisi ya urais.now every tom,dick and harry thinks can be a president.

Tuliona mwaka 2015 watu wa hovyo hovyo bila hofu waliamua kuchukua form za kugombea urais.katiba inaruhusu lakini hii haimaanishi sasa watudharau kiasi hiki.waamini kuwa upumbavuh tuliokuwa nao mwaka 2005 na kuendelea nao mpaka leo upo.

Tufikie hatua tuwaheshimu watanzania.msilete watu wa hovyo hovyo kuwapigia debe kutaka wawe marais wa nchi hii mama ya tanzania.

Nasisitiza tuheshimiane.kuna mjanga hayaepukiki kama mvua,ukame,njaa,tetemeko na kimbunga.lakini la kuchagua rais kilaza hilo ni la kujitafutia.tusifanye tena majaribio.

"Nakulilia tanzania, unajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye choyo"
Ashmkum si matusi ndugu yangu una laana ya ukoo wako yaani makubwa aliyo yafanya kikwete huyaoni?? mabarabara, zahanati, michezo na burudani,kukua kwa uhusiano wa kimataifa, ukuzaji wa demokrasia vyoooote hivi unaona ni upuuzi??? unakuja unatukana watu wanaomuona Kikwete ni bora kwa wakati wake!!!!
we jamaa usijitoe ufahamu kabisa ebu angalia maamuzi machache anayo yaamua Rais wetu na impact yake kwanza pitia ishu ya korosho, ndege, thamani ya Tsh yetu na kuanguka kwa makampuni mengi then uniambie kwa maamuzi haya Je huyu ni BORA kuliko JK???
NB: tumia akili kutafakari na si mihemko au Tumbo
 
Mleta mada umetembelea kwenye chaki vizuri sana, makosa yalianza kwenye mchakato wa urais kweny kipind cha Mkapa wakt anamaliza muda wake. Laiti kile kijiti angepatiwa Dr. Salim Ahmed Salim hakika tusingekuwa na uozo huu tulionao. Mimi namlaumu Ben na Hendisamu kwa haya yote waliyotuachia wameyataka wao
Japo Jpm kidogo huwez mlinganisha na aliyepita.
Imefika wakati nimeamua kuamini kuwa watanzania rais aliyepo madarakani hatumpendagi.
Atayefuata ajiandae kuchukiwa na watanzania na haijalishi wa chama kipi.
 
Mleta mada umetembelea kwenye chaki vizuri sana, makosa yalianza kwenye mchakato wa urais kweny kipind cha Mkapa wakt anamaliza muda wake. Laiti kile kijiti angepatiwa Dr. Salim Ahmed Salim hakika tusingekuwa na uozo huu tulionao. Mimi namlaumu Ben na Hendisamu kwa haya yote waliyotuachia wameyataka wao
Japo Jpm kidogo huwez mlinganisha na aliyepita.
Mkuu umeongea vizuri,lakini kwa Salim kosa halikuwa la Mkapa.
Salim ilikuwa awe rais baada ya Nyerere.Wakati Mel aliamini kea dhati kwamba Salim atakuwa rais,Watu ndani ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM na hasa kutokana Z'bar waliamini kuwa mchannganyiko was damu,na hasa yenye muonekano was kiarabu,hauwezi kutawala Tena Tanzania.
Hivyo watu wakagangamaa,na kumduwaza Mel,hatimaye,Mwinyi akawa rais kea kigezo kwamba alikuwa makamu ws Kwanza was rais,na.rais wa Zanzibar.
 
Nawe umetoa maoni yako. Kwa upeo wako wala siwezi kukulaumu ndo maana hata kwa maneno uliyotumia unadhihilisha una tatizo kubwa kuliko ambavyo huwa nadhani. I am so blessed kiasi kwamba naon maisha kwangu hayana taabu. Na ikitokea siwezi mlaumu mtu yeyote.

Wazazi wangu nawashukuru wamenifundisha maisha na kunipatia elimu ambayo hii hunisaidia niweze jadiliana na watu wa kila aina hata aina yako pia... Maana JF unapotaka kujiunga hawaulizi utimamu wa akili au elimu. Na inasaidia maana hata wewe umeweza comment kitu na kikasomeka kama hivi.😁😁😁


Ashmkum si matusi ndugu yangu una laana ya ukoo wako yaani makubwa aliyo yafanya kikwete huyaoni?? mabarabara, zahanati, michezo na burudani,kukua kwa uhusiano wa kimataifa, ukuzaji wa demokrasia vyoooote hivi unaona ni upuuzi??? unakuja unatukana watu wanaomuona Kikwete ni bora kwa wakati wake!!!!
we jamaa usijitoe ufahamu kabisa ebu angalia maamuzi machache anayo yaamua Rais wetu na impact yake kwanza pitia ishu ya korosho, ndege, thamani ya Tsh yetu na kuanguka kwa makampuni mengi then uniambie kwa maamuzi haya Je huyu ni BORA kuliko JK???
NB: tumia akili kutafakari na si mihemko au Tumbo
 
MAWAZO HURU HUHITAJIKA SANA UNAPOTAKA KUJADILI KITU.

JAKAYA KIKWETE KAMA RAIS WA AWAMU YA NNE HAKUWA NA TOFAUTI SANA NA MARAIS WOOTE WALIOPITA KATIKA TAIFA HILI, TUSITAKE KUDANGANYANA NA KUWA WANAFIKI.. TOKA HII NCHI IMEPATA UHURU MPAKA AWAMU YA NNE HAKUNA RAIS ALIYEWAHI KUFANYA MAAJABU HAPA TUSIDANGAYANE, TOKA AWAMU YA KWANZA MPAKA YA NNE KILA MTU ALIFANYA SEHEMU YAKE AMBAPO SIONI TOFAUTI SANA..TENA HUWEZI KUFANANISHA UTAWALA WA KIKWETE NA ULE WA BEN NA MWINYI TUACHE UNAFIKI HAPA KWA KIASI FULANI JK ALIFANYA KITU TUACHE UNAFIKI..

Sijui labda kwa sababu nilikulia ktk utawala wa Jakaya Kikwete....

Ndiyo kipindi Nilichoona barabara za lami zinajengwa...

Lakini ndicho kipindi cha JK (2005 - 2015) pia ambapo aliiua kabisa sekta ya Usafiri wa Anga na Reli...


Kiuchumi jamaa (Kikwete) kidogo alikuwa afadhali. Aliachia fedha sana kuzunguka mikononi mwa watu....

Huyu aliyepo Pombe Magufuli, fedha (uchumi) unamilikiwa na watu wachache..... kikundi kidogo ndani ya CCM na Serikali yao...

Hili ni tatizo kwa kweli
 
Nawe umetoa maoni yako. Kwa upeo wako wala siwezi kukulaumu ndo maana hata kwa maneno uliyotumia unadhihilisha una tatizo kubwa kuliko ambavyo huwa nadhani. I am so blessed kiasi kwamba naon maisha kwangu hayana taabu. Na ikitokea siwezi mlaumu mtu yeyote.

Wazazi wangu nawashukuru wamenifundisha maisha na kunipatia elimu ambayo hii hunisaidia niweze jadiliana na watu wa kila aina hata aina yako pia... Maana JF unapotaka kujiunga hawaulizi utimamu wa akili au elimu. Na inasaidia maana hata wewe umeweza comment kitu na kikasomeka kama hivi.😁😁😁
tunasema wembe ni ule ule, kipimo utakachompimia mwenzako ndicho utakachopimiwa..... mzee gudume vumilia tuu ndo maisha yalivo :cool::cool:
 
Sijui labda kwa sababu nilikulia ktk utawala wa Jakaya Kikwete....

Ndiyo kipindi Nilichoona barabara za lami zinajengwa...

Lakini ndicho kipindi cha JK (2005 - 2015) pia ambapo aliiua kabisa sekta ya Usafiri wa Anga na Reli...


Kiuchumi jamaa (Kikwete) kidogo alikuwa afadhali. Aliachia fedha sana kuzunguka mikononi mwa watu....

Huyu aliyepo Pombe Magufuli, fedha (uchumi) unamilikiwa na watu wachache..... kikundi kidogo ndani ya CCM na Serikali yao...

Hili ni tatizo kwa kweli
ukimlinganisha na huyu ni bora Jk mzee wala si kidogo afadhali
 
Mleta mada umetembelea kwenye chaki vizuri sana, makosa yalianza kwenye mchakato wa urais kweny kipind cha Mkapa wakt anamaliza muda wake. Laiti kile kijiti angepatiwa Dr. Salim Ahmed Salim hakika tusingekuwa na uozo huu tulionao. Mimi namlaumu Ben na Hendisamu kwa haya yote waliyotuachia wameyataka wao
Japo Jpm kidogo huwez mlinganisha na aliyepita.
Kama mnaruhusu siasa chafu na za kijinai ndani na nje ya chama basi kumpata rais anayetakiwa na watanzania ni ndoto. Tutaendelea muwapata marais tuliopangiwa na fisi wachache.
 
Imefika wakati nimeamua kuamini kuwa watanzania rais aliyepo madarakani hatumpendagi.
Atayefuata ajiandae kuchukiwa na watanzania na haijalishi wa chama kipi.
kuchukiwa na kupendwa ni sehemu ya umaarufu either wa kisiasa au kivyovyote ila kwa hiki kinachoendelea ni MAUMIVU ya moyo kwakua hawarusiwi kuyatoa zaidi ya nyuma ya keyboard na button za simu, pia panamkakati wa kushughulikiwa na huku pia (Lugola press) yaani tuwe taifa la mabubu. sijui ni bomu gani hili linaandaliwa
 
Maendeleo ya kwanza kwa binadamu ni uhuru wake, hivyo magufuli haamini kwenye haki za binadamu na uhuru wake hafai kabisa kuwa rais

Magufuli ameongeza umasikini nchini badala ya kuupunguza

Magufuli ameongeza deni la taifa maradufu bila kujua hizo pesa anakopa na kupeleka wapi ikiwa kila miradi mikubwa tunaambiwa ni fedha zetu za ndani

Magufuli hapambani na ukosefu wa ajira nchini

Magufuli anatengeneza nchi ambayo imegawanyika kiitikadi za kisiasa tofauti na kipindi cha Kikwete ambapo hali angalau ilikuwa siyo mbaya kama sasa

Kwa kifupi magufuli ni bomu haswa kuliko Kikwete, huyu hafai hata kuwa mkuu wa familia

Mnaomchukia Kikwete na kumuona magufuli ni bora ni wajinga sana maana hamjui shida ambazo Watanzania wanazipata awamu hii kuliko awamu ya Kikwete

Kikwete alikuwa mbovu sana ila kwa huyu Magufuli ni bora ya Kikwete

Ni sawa na kufananisha jambazi na kibaka ambapo ni bora kibaka kuliko jambazi, maana jambazi yeye hana utu yuko tayari kuua ili mambo yake binafsi yaende

Rais asiye heshimu misingi ya katiba na sharia zake alizoapa kuzilinda na bado unamuona anafaa kuwa rais ni bora ukawahi matibabu ya akili kabla ya hali kuwa mbaya zaidi
Ukimtazama magufuli kisiasa na kiitikadi hutaelewa malengo ya magufuli kwa nchi hii..lakini haihitaji tochi..umesahau tuliambiwa kuna watu wakiwekwa ndani nchi itatikisika? Yaani waachwe tu wale mema ya nchi..usalama wa nchi ilikuwa kuwaacha hao wale wasaze wao na familia zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi sina cha kuvumilia....nadhani wewe ndo unahitaji kuvumilia.muda wangu wa kuvumilia uliisha mwaka 2015. Sasa naishi kwa kujiachia na furaha. Naamini huko mbeleni wengi watatia akili. Lakini pia malezi hata huko nyuma yaliharibika ndo kikatokea kizazi hiki kilichopo sasa ambacho ni moja ya athari za kipindi kile.

tunasema wembe ni ule ule, kipimo utakachompimia mwenzako ndicho utakachopimiwa..... mzee gudume vumilia tuu ndo maisha yalivo :cool::cool:
 
Ukimtazama magufuli kisiasa na kiitikadi hutaelewa malengo ya magufuli kwa nchi hii..lakini haihitaji tochi..umesahau tuliambiwa kuna watu wakiwekwa ndani nchi itatikisika? Yaani waachwe tu wale mema ya nchi..usalama wa nchi ilikuwa kuwaacha hao wale wasaze wao na familia zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kazi ya serikali ni kupambana na ukuaji wa uchumi kwa wananchi wake, je, toka magufuli ameingia ikulu amefanikiwa kwa kiwango gani kupunguza umasikini nchini?

Magufuli amefanikiwa kwa kiwango gani kupunguza tatizo la ajira nchini?
 
Mimi sina cha kuvumilia....nadhani wewe ndo unahitaji kuvumilia.muda wangu wa kuvumilia uliisha mwaka 2015. Sasa naishi kwa kujiachia na furaha. Naamini huko mbeleni wengi watatia akili. Lakini pia malezi hata huko nyuma yaliharibika ndo kikatokea kizazi hiki kilichopo sasa ambacho ni moja ya athari za kipindi kile.
ungekua hapa nchini na hizi ngonjera zako angalau ningekuelewa..... ila nikujuze tuu binafsi sina shida nipo hapa HOME tz nakula maisha kama kawa na tunatobozaa tuu kwa sababu mimi ni born town kitambo...kikubwa tunataka jamaa ashaurike tuu kwakua majority wanaumia.
 
chuse tbr kwanza ni dhahiri kuwa hufahamu dini yangu. Ukinidhibitishia dini yangu ntashukuru. Sijajua Dr Salim A Salim ni Dini gani ambaye binafsi nliona ni mtu anayefaa kuliko kikwete.simchukii kikwete. Na dini yake mimi binafsi hainihusu hata kidogo.ila pia hainizuii kusema mabaya yake. Hali kadhalika kwa zitto na dau.

Kuna watu wa hovyo ambao nmewahi waandika. Nmewahi kumwandika ndugai,nmewahi mwandika makyembe, nmewahi mwandika mwiguru,nmewahi mwandika polepole... Hawa nmewaandika kwa kuwakosoa.nmekuwa nikikataa kata kata membe kuwa rais wa tanzania.sifaham dini yake.mana hiniuhusu.na hao wengine wote Sifahamu dini zao na pia hazinihusu.

Katika huu uzi sijasema nani anafaa nmesema watanzania tuwe serious.ikiwa nawe utaona kikwete au zitto anasemwa kwa sababu ya dini yake basi unaidhalilisha dini husika.maana sijamsema mchungaji au sheikh.ikiwa wewe unazifaham dini zao kwa majina yao ni sawa.

Tumefikia hatua tunatetea watu sababu ya dini zao.tunawasema watu sababu ya dini zao.dini zao ni zipi? Za kizungu na kiarabu? Zinakuaje zao? Mi sijui. Lakini naamini kama tukitoka nje ya box la dini tunaweza fikiria vizuri zaidi.

Nashukuru kuwa siku zote sifungwi na dini wala chama. Naandika ninachoamini...ndo maana nmewahi andika msema mbowe kwa makosa yake

NACHUKIA MATENDO NA MANENO YA WANASIASA WA HOVYO BILA KUJALI DINI,KABILA,RANGI WALA VYAMA VYAO VYA SIASA.
Kikwete ndie Raisi peke yake aliyeing'arisha Tanzania kimataifa,Tanzania ulikuwa haijulikani katika Armani ya Dunia.

Kikwete alileta fursa nyingi kwa Watanzania lakini Watanzania kushindwa kuzitumia,mfano Tanzania walipewa nafasi ya kuingia katika sio la Marekani,wafanyabiashara wakubwa wa Marekani wenye asili ya Kiafrika nakumbuka walifanya mkutano wao pale Arusha,ile ilikuwa fursa kwa wafanyabiashara wa Kitanzania..

Je Magufuli kaipeleka wapi Tanzania kimataifa?Je Watanzania wamepata fursa gani za kiuchumi na kimaendeleo tangu Magu aingie madarakani
 
Huwezi ukatuambia JK alikuwa wa hovyo kuliko Ben ukiwa na mawazo huru kichwani pasipo kuwa na chuki yeyote..

Huwezi ukatuambia Nyerere na Mwinyi walikuwa ni bora halafu ukatuambia JK alikuwa wa hovyo pasipo chuki yeyote..

Tunaposema fulani alikuwa wa hovyo kwenye nafasi fulani bila shaka tunamajibu kuna fulani alitumikia nafasi hiyo kwa ubora wa hali juu.. Toka uhuru Tanzania chini ya CCM haikuwa kupata Rais bora kwa kuangalia vigezo vyenye umuhimu kwenye nafasi ya Urais, Nyerere tunampa tu heshima kama mzee wetu lakini ukweli pasipo unafiki alishindwa kufanya yale ya muhimu kwa maendeleo ya Taifa zaidi ya kujijengea heshima binafsi na ndoto za kuwa Rais wa Africa kwa kufanya yale yenye manufaa ya kisiasa kwake..

Ya awamu ya pili na ya tatu kila mtu timamu anayajua tena afadhali ya huyo Mzee Mwinyi maana alikabidhiwa nchi ikiwa na hali mbaya lakini Ben hapana tusiwe wanafiki JK anastahili credit kubwa sana vs waliomtangulia..

Hivi unafahamu JK alijenga KM nyingi za barabara kuliko Marais wote waliomtangulia ukiunganisha, hivi unafahamu JK aliacha MW nyingi za umeme kuliko waliomtangulia ukiunganisha, idadi ya vyuo vikuu vilivyojengwa, hospitali kubwa za rufaa Benjamini mkapa dom na mloganzila na taasisi ya moyo KWELI UNAMUITA HUYU WA HOVYO..
JK ni Raisi bora kutokea Tanzania baada ya Mzee ruksa ambae aliitoa Tanzania katika kiza alichorithi kutoka kwa Baba wa Taifa J.k Nyerere,afadhali Nyerere alikiri mwenyewe kuwa nchi ilimshinda,msema kweli mpenzi wa Mungu
 
Kazi ya serikali ni kupambana na ukuaji wa uchumi kwa wananchi wake, je, toka magufuli ameingia ikulu amefanikiwa kwa kiwango gani kupunguza umasikini nchini?

Magufuli amefanikiwa kwa kiwango gani kupunguza tatizo la ajira nchini?
Kuwajengea watu miundo mbinu ni njia ya kupunguza umaskini, kuwapelekea watu umeme ni kupunguza umaskini..ajira si lazima ikuguse wewe..na ajira si lazima apate unayemjua..ila ajira zinatangazwa na watu wanapata ajira serikalini..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwajengea watu miundo mbinu ni njia ya kupunguza umaskini, kuwapelekea watu umeme ni kupunguza umaskini..ajira si lazima ikuguse wewe..na ajira si lazima apate unayemjua..ila ajira zinatangazwa na watu wanapata ajira serikalini..

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona unacheza na maneno tu lakini hakuna mahala umejibu hoja zangu
 
Hapa ndugu umeingia kijanja kwa kwa gia ya kumponda kikwete ili umpe credit jiwe ,ambaye kwa miaka hii mitatu ameonyesha hafai kabisa ,somo ambao hata ccm wenyewe na waliompigia debe Mkapa na kikwete wanajuta nalo ni kwamba sio kula anayeshinda kura za maoni anafaa kuwa rais .MTU aliyeshindwa kuajiri toka 2015 ,ambapo wapi waliostaafu ,kufa na vyeti feki ,pengo linazibwa na nani ? umeshindwa hata kujiuliza upungufu wa wafanyakazi wote hao ufanisi wa kazi serikali utakuwa uleule ? sekta binafsi kaiua kwa kutoa kodi kubwa na kuwafungia watu biashara kwa mikurupuko ambao kumepoteza mapato ,kaharibu mahusiano ya kimataifa ,kaharibu mahusiano na wawekezaji ,kashindwa kuongeza mishahara ,bandari ya DSM kukimbiwa na wafanyabiashara ,watu kutekwa , kuuawa ,kufunga kwenye viroba ,kuminya demokrasia na haki za binadamu ,halafu wewe mataga gudume unamsifia na kumponda aliyewapa nafuu watanzania ,unamsifia aliyeharibu mzunguko wa pesa watu wanataabika halafu wewe unamsifia kabisa .
GuDume sio mtu makini. Mambo yote haya watu wanalalamika kutwa kukicha yeye haoni. Maelfu ya watu wamepoteza ajira kwa sababu ya biashara kufungwa na makampuni kupunguza watu, benki zaidi ya nane zimecollapse (ajira nyingi hapa zimepotea), wawekezaji wamefunga biashara na kukimbiza mitaji nje. Sitaki kuzungumzia mateso na dhuluma nyingine.Pamoja na mapungufu ya utawala wa Kikwete, hatukuumia kiasi hiki. Wewe Gudume nimekudharau sana, halafu unavyojifanya philosophical! Pimbi mkubwa.
 
Back
Top Bottom