Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,920
- 31,161
KILIPOKUWA kikiitwa chuo cha Uongozi wa Maendeleo kikitoa masomo ya ngazi ya stashahada, sifa za ubora wa taaluma na wahitimu wake zilisambaa ndani na nje ya nchi.
Miaka saba baada ya kujibadilisha na kuanza kutoa shahada, Chuo Kikuu cha Mzumbe kimekuwa katika wakati mgumu mbele ya macho ya jamii.
Jambo kubwa linalowatatiza baadhi ya watu ni kuwepo kwa taarifa za mara kwa mara kuwa chuo hicho kina wahadhiri wasio na sifa ya kufundisha ngazi hiyo elimu ya juu.
Mfano mzuri ni taarifa ya hivi karibuni iliyotoka katika gazeti moja la kila siku kuwa chuo hicho kina wahadhiri wakuu wanane ambao vyeti vya masomo yao vina walakini.
Taarifa hiyo iliongeza kusema kuwa vyeti hivyo ama ni feki au vilitolewa na vyuo visivyokuwa na ithibati au ubora unaokubalika kimataifa.
Hata hivyo uongozi wa chuo hicho kupitia Makamu Mkuu wake Prof. Joseph Kuzilwa, umeamua kuvunja ukimya na sasa unasema taarifa hizo si za kweli na zinalenga kuupotosha umma.
Hadithi ya vyeti feki
Hii si mara ya kwanza kwa chuo hiki kilichokuwa kinara wa kutoa watendaji wengi mahiri serikalini kukumbwa na kashfa ya kuwa na walimu wasio na sifa.
Miaka michache iliyopita uliibuka mjadala katika mtandao uliokuwa ukijadili kuwepo kwa walimu wa aina hiyo chuoni hapo na hata wahitimu feki, wengine wakiwa wanasiasa.
Hata hivyo Kuzilwa, licha ya kukiri kuwa tatizo hili lilikuwepo zamani hususan wakati wa enzi za kilichokuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo, kwa sasa anasema hakuna wahadhiri wa aina hiyo kama inavyosemwa na baadhi ya watu.
Akibainisha zaidi tatizo anasema hata wakati huo tatizo halikuwa walimu kuwa na vyeti feki bali lilikuwa wahusika kusoma na kupata shahada za uzamivu kutoka vyuo ambavyo havina ithibati au ithibati yake kutotambulika na mamlaka za kitaifa.
Anakiri kuwa wahadhiri wale walioshutumiwa licha ya kuwa na shahada za uzamili kutoka katika vyuo vinavyotambulika kimataifa, kwa makosa waliomba udahili wa kusoma shahada ya uzamivu katika vyuo ambavyo hawakujua hadhi yake kitaaluma.
"Mzumbe kiliwafadhili wahadhiri hawa kama ambavyo kilifanya kwa walimu wake wengine waliopata udahili katika vyuo vingine ndani na nje ya nchi katika kutekeleza mpango wake wa kuendeleza walimu," anasema.
"Ilionekana kuwa kwa kiasi kikubwa kutokea kwa tatizo hili kulichangiwa na kuzuka duniani kwa wimbi la mfumo wa masomo kwa njia ya masafa na njia ya mtandao ambapo mfumo wa ithibati yake haujakamilika."
Watuhumiwa washughulikiwa
Baada ya kuwepo kwa taarifa hizi Baraza la Ithibati la Elimu ya Juu, sasa inaitwa Kamisheni ya Vyuo Vikuu (TCU), mbali ya kuutahadharisha umma kuhusu kuwepo kwa vyuo visivyo na sifa vinavyotoa shahada ya uzamivu, liliuelekeza uongozi wa chuo kikuu Mzumbe kuwataka wahadhiri wale waombe udahili mpya katika vyuo vyenye sifa.
"Wahadhiri wote saba waliomba udahili katika vyuo vyenye ithibati inayotambulika. Kwa bahati mbaya wawili kati yao wametangulia mbele ya haki. Watano waliobakia wapo katika hatua inayoridhisha ya kukamilisha tafiti za tasnifu zao za shahada ya uzamivu na wanatarajia kuhitimu mwaka 2010", anaeleza
Aidha anapinga taarifa kuwa uongozi wa chuo uliwafutia au kuwanyanganya sifa wahadhiri hawa kama ilivyotangazwa katika baadhi ya vyombo vya habari kwa kuwa kitaratibu Mzumbe haina uwezo wa kumnyang'anya mtu sifa ya taaluma ambayo haikumpa.
"Seneti ya Chuo Kikuu Mzumbe ina mamlaka ya kunyang'anya sifa ambayo Chuo Kikuu Mzumbe imetoa. Baraza la chuo liliagiza kuwa sifa za udaktari wa falsafa za wahadhiri hao zisitumike katika nyaraka na shughuli za chuo mpaka hapo wahusika watakapohitimu katika sifa hiyo katika udahili huu mpya"
Hadhi ya chuo
Miongoni mwa mambo yanayoelezwa kukipaka matope chuo hiki ni pamoja na kuwepo kwa taarifa kuwa chuo hiki hakikufuata taratibu kilipokuwa katika mchakato wa kukipandisha hadhi ya kuwa chuo kikuu.
"Taratibu zote za kisheria na kiithibati zilifuatwa katika kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mzumbe na hivyo ni Chuo Kikuu halali kinachotambulika na mamlaka husika za kitaifa na kimataifa", anatetea Kuzilwa na kusisitiza:
"Kusema kuwa chuo hiki hakikufuata utaratibu wakati wa kuanzishwa kwake kuwa Chuo Kikuu ni kudharau mamlaka za kitaifa na kimataifa ikiwamo Kamisheni ya Vyuo Vikuu (TCU) na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"
Anasema walipata usajili wa muda baada ya kufanyika kwa tathmini ya awali na baadaye tathmini nyingine mbili zikafanyika na ilipofika mwaka 2006 walipewa usajili wa kudumu baada ya TCU kujiridhisha katika tathmini zao.
"Ilipofika mwaka 2006 tulipewa usajili wa kudumu baada ya TCU kujiridhisha katika tathmini zao na hata leo tuko tayari muda wowote kufanyiwa tathmini kuhusu uendeshwaji wa chuo chetu," anabainisha.
Ubora wa elimu na wahadhiri
Kwa sasa Mzumbe pamoja na uchanga wake kina wahadhiri 34 wenye sifa ya shahada ya juu ya falsafa walizosoma katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje na vinavyotambulika.
Wahadhiri wengne 44 wana shahada za uzamili na sasa wapo katika hatua mbali mbali za masomo ya shahada ya falsafa.
Kuhusu ubora wa elimu anasema chuo chake kinazingatia ubora wa elimu inayoitoa kwa kutoa fursa za masomo yenye ubora na zinazoendana na mahitaji ya soko kwa Watanzania.
"Tunatambua kuwa kuwepo kwa wahadhirin wenye ujuzi wa kufundisha na waliopata elimu bora na yenye viwango vya juu ni njia mojawapo ya kufikia azma hii," anafafanua.
Anasema katika kutimiza azma ya kuongeza ubora wa programu zake chuo chake kinashiriki kikamilifu katika kuweka na kufuata mfumo wa ubora kama ulivyopitishwa na Baraza la Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki (IUCEA). Hadi sasa kimeshafanyiwa ukaguzi mmoja wa nje.
Miaka saba baada ya kujibadilisha na kuanza kutoa shahada, Chuo Kikuu cha Mzumbe kimekuwa katika wakati mgumu mbele ya macho ya jamii.
Jambo kubwa linalowatatiza baadhi ya watu ni kuwepo kwa taarifa za mara kwa mara kuwa chuo hicho kina wahadhiri wasio na sifa ya kufundisha ngazi hiyo elimu ya juu.
Mfano mzuri ni taarifa ya hivi karibuni iliyotoka katika gazeti moja la kila siku kuwa chuo hicho kina wahadhiri wakuu wanane ambao vyeti vya masomo yao vina walakini.
Taarifa hiyo iliongeza kusema kuwa vyeti hivyo ama ni feki au vilitolewa na vyuo visivyokuwa na ithibati au ubora unaokubalika kimataifa.
Hata hivyo uongozi wa chuo hicho kupitia Makamu Mkuu wake Prof. Joseph Kuzilwa, umeamua kuvunja ukimya na sasa unasema taarifa hizo si za kweli na zinalenga kuupotosha umma.
Hadithi ya vyeti feki
Hii si mara ya kwanza kwa chuo hiki kilichokuwa kinara wa kutoa watendaji wengi mahiri serikalini kukumbwa na kashfa ya kuwa na walimu wasio na sifa.
Miaka michache iliyopita uliibuka mjadala katika mtandao uliokuwa ukijadili kuwepo kwa walimu wa aina hiyo chuoni hapo na hata wahitimu feki, wengine wakiwa wanasiasa.
Hata hivyo Kuzilwa, licha ya kukiri kuwa tatizo hili lilikuwepo zamani hususan wakati wa enzi za kilichokuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo, kwa sasa anasema hakuna wahadhiri wa aina hiyo kama inavyosemwa na baadhi ya watu.
Akibainisha zaidi tatizo anasema hata wakati huo tatizo halikuwa walimu kuwa na vyeti feki bali lilikuwa wahusika kusoma na kupata shahada za uzamivu kutoka vyuo ambavyo havina ithibati au ithibati yake kutotambulika na mamlaka za kitaifa.
Anakiri kuwa wahadhiri wale walioshutumiwa licha ya kuwa na shahada za uzamili kutoka katika vyuo vinavyotambulika kimataifa, kwa makosa waliomba udahili wa kusoma shahada ya uzamivu katika vyuo ambavyo hawakujua hadhi yake kitaaluma.
"Mzumbe kiliwafadhili wahadhiri hawa kama ambavyo kilifanya kwa walimu wake wengine waliopata udahili katika vyuo vingine ndani na nje ya nchi katika kutekeleza mpango wake wa kuendeleza walimu," anasema.
"Ilionekana kuwa kwa kiasi kikubwa kutokea kwa tatizo hili kulichangiwa na kuzuka duniani kwa wimbi la mfumo wa masomo kwa njia ya masafa na njia ya mtandao ambapo mfumo wa ithibati yake haujakamilika."
Watuhumiwa washughulikiwa
Baada ya kuwepo kwa taarifa hizi Baraza la Ithibati la Elimu ya Juu, sasa inaitwa Kamisheni ya Vyuo Vikuu (TCU), mbali ya kuutahadharisha umma kuhusu kuwepo kwa vyuo visivyo na sifa vinavyotoa shahada ya uzamivu, liliuelekeza uongozi wa chuo kikuu Mzumbe kuwataka wahadhiri wale waombe udahili mpya katika vyuo vyenye sifa.
"Wahadhiri wote saba waliomba udahili katika vyuo vyenye ithibati inayotambulika. Kwa bahati mbaya wawili kati yao wametangulia mbele ya haki. Watano waliobakia wapo katika hatua inayoridhisha ya kukamilisha tafiti za tasnifu zao za shahada ya uzamivu na wanatarajia kuhitimu mwaka 2010", anaeleza
Aidha anapinga taarifa kuwa uongozi wa chuo uliwafutia au kuwanyanganya sifa wahadhiri hawa kama ilivyotangazwa katika baadhi ya vyombo vya habari kwa kuwa kitaratibu Mzumbe haina uwezo wa kumnyang'anya mtu sifa ya taaluma ambayo haikumpa.
"Seneti ya Chuo Kikuu Mzumbe ina mamlaka ya kunyang'anya sifa ambayo Chuo Kikuu Mzumbe imetoa. Baraza la chuo liliagiza kuwa sifa za udaktari wa falsafa za wahadhiri hao zisitumike katika nyaraka na shughuli za chuo mpaka hapo wahusika watakapohitimu katika sifa hiyo katika udahili huu mpya"
Hadhi ya chuo
Miongoni mwa mambo yanayoelezwa kukipaka matope chuo hiki ni pamoja na kuwepo kwa taarifa kuwa chuo hiki hakikufuata taratibu kilipokuwa katika mchakato wa kukipandisha hadhi ya kuwa chuo kikuu.
"Taratibu zote za kisheria na kiithibati zilifuatwa katika kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mzumbe na hivyo ni Chuo Kikuu halali kinachotambulika na mamlaka husika za kitaifa na kimataifa", anatetea Kuzilwa na kusisitiza:
"Kusema kuwa chuo hiki hakikufuata utaratibu wakati wa kuanzishwa kwake kuwa Chuo Kikuu ni kudharau mamlaka za kitaifa na kimataifa ikiwamo Kamisheni ya Vyuo Vikuu (TCU) na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"
Anasema walipata usajili wa muda baada ya kufanyika kwa tathmini ya awali na baadaye tathmini nyingine mbili zikafanyika na ilipofika mwaka 2006 walipewa usajili wa kudumu baada ya TCU kujiridhisha katika tathmini zao.
"Ilipofika mwaka 2006 tulipewa usajili wa kudumu baada ya TCU kujiridhisha katika tathmini zao na hata leo tuko tayari muda wowote kufanyiwa tathmini kuhusu uendeshwaji wa chuo chetu," anabainisha.
Ubora wa elimu na wahadhiri
Kwa sasa Mzumbe pamoja na uchanga wake kina wahadhiri 34 wenye sifa ya shahada ya juu ya falsafa walizosoma katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje na vinavyotambulika.
Wahadhiri wengne 44 wana shahada za uzamili na sasa wapo katika hatua mbali mbali za masomo ya shahada ya falsafa.
Kuhusu ubora wa elimu anasema chuo chake kinazingatia ubora wa elimu inayoitoa kwa kutoa fursa za masomo yenye ubora na zinazoendana na mahitaji ya soko kwa Watanzania.
"Tunatambua kuwa kuwepo kwa wahadhirin wenye ujuzi wa kufundisha na waliopata elimu bora na yenye viwango vya juu ni njia mojawapo ya kufikia azma hii," anafafanua.
Anasema katika kutimiza azma ya kuongeza ubora wa programu zake chuo chake kinashiriki kikamilifu katika kuweka na kufuata mfumo wa ubora kama ulivyopitishwa na Baraza la Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki (IUCEA). Hadi sasa kimeshafanyiwa ukaguzi mmoja wa nje.