Pima mwenyewe
JF-Expert Member
- Nov 20, 2012
- 891
- 237
Kweli alie shiba amkumbuki mwenye njaa . Albino wanauawa na polisi inavamiwa eti usalama
Tumieni ubongo kufikiri nasi moyo mkuu
Sasa rafiki hebu tufikiri kidogo; wauza viungo vya binadamu ni polisi ama jamii tunayoishi nayo? Hebu fikiria wauzaji wengine ndugu zetu tunaishi nao na tunawafichia uovu kisa eti tutalogwa? Sasa hivi huyu polisi yeye bila msaada wa jamii anawaibuaje hao waovu kama wewe tu unayeishi nao huwatambui? Kuna kitu kinachoitwa Polisi jamii, je uliwahi kukisikia? Kama ndiyo umeshiriki vipi wewe mwenyewe maana mtandao wake unafika hadi uliko wewe? Kama hujawahi kusikia unadhani shida nini? Wewe unajishirikishaje kwenye forum za maendeleo ya kijijini, kata, tarafa na Wilaya? Hivi unahudhuria vikao vingapi vya ngazi ya jamii uliyopo wewe au umewaachia wazee tu? Jamani hebu tufanye audit ya akina nani huhudhuria forum za maendeleo ngazi za chini zaidi! Kama hatujitokezi kushiriki mambo ya msingi huko kwa wananchi na kutwa kushinda jf kushabikia basi yawezekana hata fursa hatuwezi kukutana nazo. Jitafakari