Miaka 50 ya Uhuru-Walimu 2 tangu 1976

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
773738251.JPG
Mwalimu Mkuu akitoka kwenye ofisi yake​



Shule ya Msingi Kitete iliyopo katika kata ya Uchindile, Tarafa ya Mlimba wilayani Kilorombero mkoani Morogoro yenye walimu wawili tu na wanafunzi 29.

Shule ilianzishwa mwaka 1976. Ipo zaidi ya kilomita 150 kutoka Kilombero mkoani Morogoro na kilomita zaidi ya 125 kutoka Mafinga, mkoani Iringa.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Idd Mdaba anasema tangu ahamishiwe katika shule hiyo mwaka 2008 kwa ahadi kwamba angehamishiwa shule nyingine baada ya miaka mitatu, amekuwa akifundisha mwenyewe wanafunzi wa madarasa yote yaliyopo katika shule hiyo, “Hata hivyo nashukuru mzigo huo umepungua mwezi mmoja tu uliopita baada ya kuletewa mwalimu mwingine mmoja kutoka wilayani Geita ,” alisema huku Mwalimu huyo Juma Deke akidai kujutia uamuzi wa kuomba uhamisho kutoka Geita ili ahamie mkoani kwake Morogoro kwani hakujua kama angepangiwa shule kama hiyo.

Alisema mbali na shule hiyo kutokuwa na vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ofisi ndogo ya mwalimu na madarasa yake matatu yaliyopo, hayajasakafiwa chini na kuta zake, hakuna madirisha na milango na yote kwa ujumla wake yana madawati yasiozidi 20.

Mdaba alisema mazingira hayo yameifanya shule hiyo kukosa wanafunzi wa darasa la kwanza, la tatu na la tano hadi la saba hivi sasa baada ya waliopaswa kuwa wanafunzi wa madarasa hayo kutosajiliwa mwaka wa kwanza wa masomo yao ya darasa la kwanza.

Picha zaidi kuhusu shule hii, tembelea blogu ya Lukwangule (chanzo cha habari na picha ni Frank Leonard).

source: Wavuti - Habari
 
773738251.JPG
Mwalimu Mkuu akitoka kwenye ofisi yake​



Shule ya Msingi Kitete iliyopo katika kata ya Uchindile, Tarafa ya Mlimba wilayani Kilorombero mkoani Morogoro yenye walimu wawili tu na wanafunzi 29.

Shule ilianzishwa mwaka 1976. Ipo zaidi ya kilomita 150 kutoka Kilombero mkoani Morogoro na kilomita zaidi ya 125 kutoka Mafinga, mkoani Iringa.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Idd Mdaba anasema tangu ahamishiwe katika shule hiyo mwaka 2008 kwa ahadi kwamba angehamishiwa shule nyingine baada ya miaka mitatu, amekuwa akifundisha mwenyewe wanafunzi wa madarasa yote yaliyopo katika shule hiyo, "Hata hivyo nashukuru mzigo huo umepungua mwezi mmoja tu uliopita baada ya kuletewa mwalimu mwingine mmoja kutoka wilayani Geita ," alisema huku Mwalimu huyo Juma Deke akidai kujutia uamuzi wa kuomba uhamisho kutoka Geita ili ahamie mkoani kwake Morogoro kwani hakujua kama angepangiwa shule kama hiyo.

Alisema mbali na shule hiyo kutokuwa na vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ofisi ndogo ya mwalimu na madarasa yake matatu yaliyopo, hayajasakafiwa chini na kuta zake, hakuna madirisha na milango na yote kwa ujumla wake yana madawati yasiozidi 20.

Mdaba alisema mazingira hayo yameifanya shule hiyo kukosa wanafunzi wa darasa la kwanza, la tatu na la tano hadi la saba hivi sasa baada ya waliopaswa kuwa wanafunzi wa madarasa hayo kutosajiliwa mwaka wa kwanza wa masomo yao ya darasa la kwanza.

Picha zaidi kuhusu shule hii, tembelea blogu ya Lukwangule (chanzo cha habari na picha ni Frank Leonard).

source: Wavuti - Habari

sasa huyu mwalimu si atakatwa na mabati kama ikitukea purukushani ktk ofisi
angalia meza yake na dawati lilivyo chakaa,panya wanaonekana ktk picha wakizunguka huku na kule

Hivi kweli serikali imeshindwa kununua ama kuchukua zile faniture zinazobadilishwa ktk maofisi ya serikali kama kwa waziri mkuu,Raisi ama Makamu wa Raisi na kuwapelekea hawa walimu ambao ndio wanao tuandalia vijana wetu
 
Wapi mbunge wa Kilombero Papa ABDUL MTETEKETA...AWIJEE BAMBO...AU NAKASHINA ...Kazi kweli kweli.Kwanza kufika hapo Uchindile sio mchezo..Mnnnhhhh
 
Wapi mbunge wa Kilombero Papa ABDUL MTETEKETA...AWIJEE BAMBO...AU NAKASHINA ...Kazi kweli kweli.Kwanza kufika hapo Uchindile sio mchezo..Mnnnhhhh

WE ACHA TU
mwakashina hayupo,na wala haoni hayo na nasikia huwa anakwenda kuongea na wanachi maeneo hayo lakini wapiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii,kidole na macho
 
Back
Top Bottom