Miaka 10 Kawe Barabara ni mitaro ya maji, Gwajima okoa jahazi

Miaka 10 Kawe Barabara ni mitaro ya maji, Gwajima okoa jahazi

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
17,547
Reaction score
28,494
Kwa miaka 10 aliyokaa Halima Mdee kuwakilisha jimbo la Kawe, maendeleo ya miundombinu ya kijamii ni kama hakuna.
Barabara chache sana za kuunganisha maeneo zimejengwa.

Nimeishi jimbo ka Kawe zaidi ya miaka 20 baada ya kuhamia huku toka Temeke.
Hali ya jimbo la Kawe inatisha.
Tunahisi Mdee aidha hawezi kazi yake kushawishi serikali kuleta hayo maendeleo muhimu ya miundombinu ya barabara, au tu kwamba hafai.

Kwa muda wote huo sijamwona huku mitaani akipita kusikiliza kero kubwa za wananchi hususan barabara.

Huwa narudi Temeke, Tandika na Kijichi na huwezi kuamini.
Barabara mpya maeneo hayo ni zaidi ya kilometa 100, na zinapita hadi uchochoroni.

Tatizo lipo kwa mwakilishi wetu, Halima Mdee.
Tusichague vyama tuchague mtu awezaye kuleta maendeleo ya barabara.
Watu wasichague kwa mazoea, chagua Gwajima tupate mabadiliko na maendeleo.
Hata waliomchagua Trump si kwamba wanampenda, wamemchagua kwa maslahi ya maendeleo yao.

Wana Kawe tuwe strategic, chagua Gwajima.
 
Kheri James na mjomba wake wamesema hadharani kuwa usipochagua CCM maendeleo hawaleti na la kuwafanya hatuna.

Mwaka huu tunawajibu kuwa Rais, Mbunge na Diwani watatoka upinzani na maendeleo yatakua kwa wote.
 
Kheri James na mjomba wake wamesema hadharani kuwa usipochagua CCM maendeleo

Hawa letu na la kuwafanya hatuna.
Mwaka huu tunawajibu kuwa Rais, Mbunge na Diwani watatoka upinzani na maendeleo yatakua kwa wote.
Dawa yao hawa wapuuzi ni mfumo unaopendekezwa na Chadema tu. Yaani hela za jimbo husika zifanye maendeleo kwenye jimbo husika. Ndo mana wanabwabwaja ujinga tu humu Eti mbunge atoke kwa sababu Kuna barabara mbovu wakati mbunge wala hajengi barabara na wanakusanya fedha za walipa kodi wanaenda kujenga viwanja vya kimataifa vijijini kwao Chato huko!
 
Kheri James na mjomba wake wamesema hadharani kuwa usipochagua CCM maendeleo hawaleti na la kuwafanya hatuna.

Mwaka huu tunawajibu kuwa Rais, Mbunge na Diwani watatoka upinzani na maendeleo yatakua kwa wote.
Ni kujidanganya kuwa ukichagua upinzani maendeleo yatakuja.
Kawe ni mfano dhahiri.
Halima yupo pale kama picha, hanyanyui mdomo kutetea maendeleo ya barabara kwa miaka 10 sasa.
 
Maendeleo huletwa na serikali inayokusanya kodi , hayaletwi na pesa za mbunge .
Kawaambie hivyowana Kawe, Halima ameshindwa kuiamsha Serikali jimboni Kawe.Gwajima nina uhakika ataiamsha Serikali.
 
Kwa miaka 10 aliyokaa Halima Mdee kuwakilisha jimbo la Kawe, maendeleo ya miundombinu ya kijamii ni kama hakuna.
Barabara chache sana za kuunganisha maeneo zimejengwa.

Nimeishi jimbo ka Kawezaidi ya miaka 20 baada ya kuhamia huku toka Temeke, hali ya Kawe inatisha.
Tunahisi Mdee aidha hawezi kazi yake kushawishi serikali kuleta hayo maendeleo muhimu ya miundombinu ya barabara, au tu kwamba hafai.

Kwa muda wote huo sijamwona huku mitaani akipita kusikiliza kero kubwa za wananchi hususan barabara.

Huwa narudi Temeke, Tandika na Kijichi na huwezi kuamini.
Barabara mpya maeneo hayo ni zaidi ya kilometa 100, na zinapita hadi uchochotoni.

Tatizo lipo kwa muwakilishi wetu, Halima Mdee.
Tusichague vyama tuchaguemtu awezaye kuleta maendeleo ya barabara.
Watu wasichague kwa mazoea, chagua Gwajima tupate mabadiliko na maendeleo.
Hata waliomchagua Trump si kwamba wanampenda, wamemchagua kwa maslahi ya maendeleo yao.

Wana Kawe tuwe strategic, chagua Gwajima.
kazi ya mbunge ni kujenga barabara?
 
Back
Top Bottom