GE2025 Mhuni Hasusiwi uchaguzi

GE2025 Mhuni Hasusiwi uchaguzi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
ACT - Wazalendo wamekuja na ujumbe muhimu sana "#MHUNI HASUSIWI KURA" na OKTOBA - LINDA KURA.
Ni jumbe kali sana. Napenda kuziwakilisha kwa NO REFORM NO ELECTION, ili tuzijadili hoja hizi mbili kwa kina.

Kwani ni takriban miezi 3 mpaka uchaguzi, hatujachelewa kwa jumbe moja au nyingine, meza inaweza kugeuzwa. Wakati wa maamuzi ni huu.
Kwani kuna chama kimesusia uchaguzi ?
 
..ACT wange-focus kwenye kampeni ya " Oktoba tunalinda kura. "

..kujibizana na Chadema kunawapunguzia nguvu ya kupambana na Ccm.
Si kujibizana, bali ni kujaribu kuelewa na kujadili idiolojia mbili tofauti. Kuona nje ya box ya kila upande, kwa mfano faida na hasara kwa nchi na watanzania kwa jumla.
Katika mjadala huu ni vizuri kutojikita sana kwenye vyama, bali kwenye idiolojia kwa mustakabali wa nchi na wananchi wake.
 
Inamaana wataanza kujitambua oktoba 29, Mpina ameshindwa kulinda jina lake huko kisesa, Ndo atalinda kula za Uraisi?

Watu sio wajinga bhana.
Kwenye hili, tupo pamoja kwani hata mimi namlaumu kukimbilia Urais badala ya kutetea jimbo lake la Kisesa.
Hata ACT wenyewe wamechemka, sijui kwanini hili hawakuliona. Hapo nimemdharau Mpina, alifaa sana kugombea ubunge.
 
subiri uone mambo ambayo akili ya mwanadamu haikuwa na uwezo wa kuyang'amua
Wakati/muda ndio mwalimu wa kweli. Tusubiri wote. Kama kutakuwa na wabunge upinzani zaidi ya 25, upande wa Mhuni hasusiwi kura utakuwa sahihi. Kama jumla ya wabunge upinzani watakuwa chini ya 25, NO REFORM NO ELECTION utakuwa sahihi.
 
Ninachowasihi ni kimoja: Vyote ni vyama vya upinzani, Tujadili kauli mbiu hizo mbili:
  • #MHUNI HASUSIWI UCHAGUZI
  • NO REFORM NO ELECTION
Tujadili kauli mbiu hizi kwa undani kwa manufaa ya vyama vyote viwili ACT na CHADEMA. Pengine tunaweza kuwashawishi ACT wafikiri mara mbili katika kuingia katika uchaguzi au wana ACT watujengee hoja ili pengine wanaweza kuwashawishi CHADEMA kubadili mawazo yao na kuingia ktk uchaguzi. Dirisha lipo wazi.
ACT wako sahihi kabisa. Ni suala la wapiga kura wote wa chadema na ACT kuunganisha nguvu ili kumuonyesha aliyeko madarakani kuwa hatakiwi.

Ni kupiga kura kwa wingi sana ili waogope
 
..ACT wange-focus kwenye kampeni ya " Oktoba tunalinda kura. "

..kujibizana na Chadema kunawapunguzia nguvu ya kupambana na Ccm.
Ninaamini ACT wame-focus kwenye kampeni ya "Oktoba tunalinda kura" hili ni jambo lao.
Sijibizani na CHADEMA. Ninachosema tujadili dhana hizi 2 kwa faida ya Taifa.

Kwa mfano: Ndugu Polepole katika mazungumzo yake amekuwa muwazi kuwa yeye hakubaliani na NO REFORM NO ELECTION kwa vile kauli hiyo haina mashiko. Akaendelea kwa kusema, haoni utekelezaji wa kauli hiyo utafanywa vipi na wanachama na watanzania wameelimishwa faida, hasara kwa Taifa.
 
ACT wako sahihi kabisa. Ni suala la wapiga kura wote wa chadema na ACT kuunganisha nguvu ili kumuonyesha aliyeko madarakani kuwa hatakiwi.

Ni kupiga kura kwa wingi sana ili waogope
Wananchi wa Zanzibar hawajawahi kupiga kura kwa wingi kuiondoa CCM kule, ila bado CCM inafaulu kukimbia na masanduku ya kura?
 
Ni slogan ya kipumbavu na kid kidhaifu mno, wamelinda mara ngapi wakafanikiwa? Kama CCM wenyewe kwa wenyewe wanaibiana kura hadi kuuwana, wewe ACT si watakunyonyoa kabisa.??
Napenda uelewe kitu kimoja: Kwa mwanasiasa yeyote anayepatikana kwa kuchaguliwa na wanachi hata kama ni mgombea pekee akashindana na kivuli (Mfano wakati wa Mwl Nyerere). Na ikafahamika kuwa yeye kapata 40% na kivuli kikapata 60%. Na kwenye kutangaza wakapindua hizo namba, mwanasiasa huyo hatakuwa na raha katika uongozi wa kipindi chake chote.

Kwa hiyo mimi naamini kuwa matokeo ya hizi chaguzi, hata kama CCM watafoji, lakini huko ndani wanaambiana ukweli. Kuwa mwenzetu tumekutetea kwa nguvu zote, lakini ulipata 40%. Hizi namba ndio zinawafanya CCM wabadilike.
 
29 okt ndio tutazungumza lugha moja. Jana si leo, Maandishi Tz hayafuatwi. Kama katiba yenyewe inakiukwa mchana kweupeeeee, itakuwa hizo fomu za maadili. Na jana si leo, dunia inakwenda haraka sana. Wanajitambua hawa kuliko unavyofikiria wewe.
Kamsikilize Muliro alivowajibu kwenye Ile interview yake aliyofanya
 
ACT - Wazalendo wamekuja na ujumbe muhimu sana "#MHUNI HASUSIWI KURA" na OKTOBA - LINDA KURA.
Ni jumbe kali sana. Napenda kuziwakilisha kwa NO REFORM NO ELECTION, ili tuzijadili hoja hizi mbili kwa kina.

Kwani ni takriban miezi 3 mpaka uchaguzi, hatujachelewa kwa jumbe moja au nyingine, meza inaweza kugeuzwa. Wakati wa maamuzi ni huu.

Formality itakamilika kwa vyovyote vile. Tukaamua kuipa jina tunalotaka.

Ila panapofuka moshi....sijui siku hizi, zamani tulikuwa tunasema pana moto.

Labda siku hizi pana maji baridi maana hii AI na technology ina mambo mengi
 
Back
Top Bottom