GE2025 Mhuni Hasusiwi uchaguzi

GE2025 Mhuni Hasusiwi uchaguzi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
29 okt ndio tutazungumza lugha moja. Jana si leo, Maandishi Tz hayafuatwi. Kama katiba yenyewe inakiukwa mchana kweupeeeee, itakuwa hizo fomu za maadili. Na jana si leo, dunia inakwenda haraka sana. Wanajitambua hawa kuliko unavyofikiria wewe.

Acheni Utapeli.
 
Napenda uelewe kitu kimoja: Kwa mwanasiasa yeyote anayepatikana kwa kuchaguliwa na wanachi hata kama ni mgombea pekee akashindana na kivuli (Mfano wakati wa Mwl Nyerere). Na ikafahamika kuwa yeye kapata 40% na kivuli kikapata 60%. Na kwenye kutangaza wakapindua hizo namba, mwanasiasa huyo hatakuwa na raha katika uongozi wa kipindi chake chote.

Kwa hiyo mimi naamini kuwa matokeo ya hizi chaguzi, hata kama CCM watafoji, lakini huko ndani wanaambiana ukweli. Kuwa mwenzetu tumekutetea kwa nguvu zote, lakini ulipata 40%. Hizi namba ndio zinawafanya CCM wabadilike.


Njaa imeingia mpaka huko. Wameanza kupambana wenyewe kwa wenyewe maana njaa haina adabu
 
Wananchi wa Zanzibar hawajawahi kupiga kura kwa wingi kuiondoa CCM kule, ila bado CCM inafaulu kukimbia na masanduku ya kura?
Ni kweli na uko sahihi. Ila Tanganyika ina karibu ya wananchi zaidi ya milioni 55. Kwa hiyo ni kazi kweli kweli kufoji uchaguzi Tanganyika kama zaidi ya 60% wakasema No. Utakubaliana nami kuwa kwa bahati mbaya CCM bado inakaubaliwa kwa takriban 50% kwa Tanganyika tofauti na Zzibar.
 
Ninaamini ACT wame-focus kwenye kampeni ya "Oktoba tunalinda kura" hili ni jambo lao.
Sijibizani na CHADEMA. Ninachosema tujadili dhana hizi 2 kwa faida ya Taifa.

Kwa mfano: Ndugu Polepole katika mazungumzo yake amekuwa muwazi kuwa yeye hakubaliani na NO REFORM NO ELECTION kwa vile kauli hiyo haina mashiko. Akaendelea kwa kusema, haoni utekelezaji wa kauli hiyo utafanywa vipi na wanachama na watanzania wameelimishwa faida, hasara kwa Taifa.
Haoni au hataki kuona? Mbona liko wazi na very simple, ukihamasisha watu wasiende kupiga kura inamaanisha nini? Haina mashiko kivipi?
 
#MHUNI HASUSIWI UCHGUZI - Tuseme usemi huu ni joke ya mwaka na NO REFORM NO ELECTION ndio habari ya mjini, Swali hivi huko nyuma CHADEMA imewahi kususia uchaguzi? Kama jibu ni yes, ilipata nini?

Shida mnahangaika na CHADEMA. Kususia inatoka wapi?. Mmemchukua mgombea urais kutoka kwa wahuni halafu mnadai muhuni hasusiwi.
 
Nathamini mchango wako. Ila kuna wengine wanaamini kuwa uchaguzi upo na hata wengine toka CHADEMA. Hawa wamelazimika kutafuta majukwaa mengine na kuomba ridhaa yakugombea nafasi tofauti kupitia vyama hivyo.

Kugombea hakuleti uhalali wa uchaguzi kufanya.
 
Project ya Mchengerwa na Abdul, watu watawashangaza mwaka huu.

Utapeli hauna nafasi kwa sasa.

Sasa nyie mnakiri mnaenda kushindana na mhuni na sio uchaguzi unatarajia nini?
 
Ni kweli na uko sahihi. Ila Tanganyika ina karibu ya wananchi zaidi ya milioni 55. Kwa hiyo ni kazi kweli kweli kufoji uchaguzi Tanganyika kama zaidi ya 60% wakasema No. Utakubaliana nami kuwa kwa bahati mbaya CCM bado inakaubaliwa kwa takriban 50% kwa Tanganyika tofauti na Zzibar.
Watanzania hatudanganyikia, ACT ni kibaraka wa CCM.
 
Ninaamini ACT wame-focus kwenye kampeni ya "Oktoba tunalinda kura" hili ni jambo lao.
Sijibizani na CHADEMA. Ninachosema tujadili dhana hizi 2 kwa faida ya Taifa.

Kwa mfano: Ndugu Polepole katika mazungumzo yake amekuwa muwazi kuwa yeye hakubaliani na NO REFORM NO ELECTION kwa vile kauli hiyo haina mashiko. Akaendelea kwa kusema, haoni utekelezaji wa kauli hiyo utafanywa vipi na wanachama na watanzania wameelimishwa faida, hasara kwa Taifa.

..Polepole amekubaliana na No Reforms No Election na amependekeza yawepo mazungumzo ya kitaifa ya wadau wote kabla ya uchaguzi.

..Pia amemtaka Mama Samia amuachie Tundu Lissu ili aweze kushiriki ktk mazungumzo hayo ya kitaifa.

..Hapo nyuma Polepole alikuwa anacheza na maneno tu lakini kwa ujumla anataka marekebisho kabla ya uchaguzi.
 
Punguza ujinga wewe chawa. Nimekureply wewe?. Peleka uccm wako kwa Samiah.
Angalia reply zako huna hoja, siku zote mfinyu wa mawazo na akili anakimbilia kutusi..... Unaongea vitu hujui usije hapa na half baked information. And fyi Mimi sio ccm ila nachukia watu wanaoongea vitu wasivyovijua kama wewe. Unaamka na mihemko hujui hata siasa imeendaje
 
Kwenye hili, tupo pamoja kwani hata mimi namlaumu kukimbilia Urais badala ya kutetea jimbo lake la Kisesa.
Hata ACT wenyewe wamechemka, sijui kwanini hili hawakuliona. Hapo nimemdharau Mpina, alifaa sana kugombea ubunge.

ACT hawajachemka, yeye ndie aliechemka. ACT walihaitaji mtu mwenye credibility ya kisiasa katika hiyo nafasi kwa ajili kusaidia muamko kwenye kampeni. Ila viongozi wao wakubwa wote waliingia kwenye majimbo. kwahiyo yeye kaja ku cover nafasi waliokua wanaumisha kichwa kuijaza.
 
Back
Top Bottom