Ndugu zangu wana JF natumaini mko wazima wa afya.
Leo Mheshimiwa Raisi ameonekana ni mzima. Kwa wale ambao walijipanga, walijiandaa au kutunza Pesa kwa ajiri ya kulewa na kuumwagilia moyo juu ya kifo cha Mheshimiwa Raisi, poleni sana kwa maana ya njia za Mungu sio za Binadamu.
Msife mioyo, nina ushauri juu ya hizo Pesa, mnaweza kuzitumia kwa namna nyingine mfano;
- Kuchangia yatima,
- kuongeza mitaji, ikiwa mitaji midogo,
- Au kuwatumia wazazi wafurahi msimu huu wa sikukuu,
- Kuwasaidia masikini ikifaa,
- Na shughuli zingine zinazofaa au zinazompendeza mungu.
La mwisho;
Tuombeane mwisho Mwema Ndugu na Dada zangu kwa maana sisi tu wasafiri humu ulimwenguni.