Mheshimiwa John Mnyika: What is Plan C


Sheria ya Tanzania hairuhusu mtu mwengine yoyote kuuza umeme reja reja isipokuwa Tanesco. Kwa hiyo hata TANESCO ikipatiwa mafuta haitajalisha nani katoa kiasi gani, akiwasha umeme TANESCO itabidi usambazwe kwa wote na kama ukidumu kwa nusu saa tu kutokana na demand ya kukidhi eneo lote, tutashindwa kuwadhibiti.

Bado hatujafika hasa kwenye solutions mkuu, hebu tufikiri tena
 

Mkuu tatizo miradi ya 10% imekuwa mingi sana na ishaonekana kuwa Tanesco ndipo mahali pekee ambako ten percent zinafanya kazi
So hatutaambiwa tatizo ni nini na bado dharura zitaendelea kuwepo mpaka mwisho na wala hakuna wa kutuambia kiini cha tatizo ni nini
Mpakka watakapolimaliza shirika ndio tutakuja kujua kuwa kumbe tatizo lilikuwa hili
 
...INATOSHA SASA.kilicho muafaka ni kuunganisha nguvu zetu wanyonge na kuwashikisha adabu,kuwatoa kabisa madarakani,tuanze upya!

Kwahiyo mkuu huamini kabisa kwamba unaweza ukatumia non-violence na ukapata results bora zaidi kuliko kwa kutumia nguvu.., kwahiyo mi naona njia nzuri na rahisi (ambayo pia haiwezi ikawa mis-qouted) kama vurugu ni kuonyesha maovu ya hawa waliomadarakani na wananchi wenyewe watawaondoa madarakani (yaani jamii nzima itasema imechoka)... kuliko watu wachache wakipinga wata-spin kwamba hawa jamaa ni wapenda fujo na baba na bibi zetu vijijini wataamini...

By the way kwahiyo unasema tukae gizani mpaka pale tutakapowaondoa madarakani
 

Indeed hapa siongelei sisi kuanza kuuza umeme, hapana sababu kwanza hii itakuwa ngumu sababu inabidi tutumie transmission za tanesco

Pia ni kwamba hata kama tukiweza kuwapa wananchi wote umeme kwa masaa mawili (it does not matter) itakuwa symbolic kwamba wananchi waliweza kujipatia umeme wenyewe kwa siku moja..., Hivyo basi hadithi za viongozi kwamba haiwezekani au hii kazi ni ngumu sana itakuwa haipo...

Point yangu sio kwamba wananchi tuanze kutajirika kwa kufanya competition na Tanesco..., bali ni tuangalie ni wapi tumekwama ili tuone kama tunaweza kupanyoosha..

Sababu mpaka sasa ni kwamba kila mtu individually inamcost zaidi, pia am sure kama mkiongea na Tanesco kwamba tunachangia hapa ili huu umeme huende kwenye line za industrial areas sidhani kama watakataa au Generator kubwa la ku-supply mtaa mzima na excess inayobaki kuwauzia tanesco (kumbuka hapa tutakuwa hatuuzi reja reja)
 
Plan c tukazichukue hela za nshimbo south kwanza zen mkweere atupishe kwa nguvu ya umma
 

when.........................?
 

Mkuu hizi ndoto zitaisha lini
Muda wa kuchukua hatua ni sasa
Mwaka tuoka wachaguliwe unakatika na hatuna lolote la kujivunia na ndo tunazidi kudidimia zaidi na zaidi
Tusubiri mpaka lini
Malalamiko tumeshatoa mpaka yamepitiliza na hatuoni kama kuna suluhisho
Bado tuu tuendelee kulalamika
 


Nilichokusudia kukueleza ni kuwa, mfano watu 30 kwenye industrial area wamechangia lakini wengine 10 hawakutaka kufanya hivyo. Umeme ukizalishwa na TANESCO hakuna atakaeweza kuwazuwia hao wafanya biashara wasio changia kutumia umeme huo. Na itatagemea wasiochangia wana demand kubwa kiasi gani pia. Ikiwa demand yao ni kubwa, gharama za umeme kwa siku kwako wewe inaweza ikawa ni ile ile tu.

Usisahau kuzingatia kuwa hela yako uliyochangia haitaweza kurudi hadi watu walipe bills zao pia.

Sipo kukuvunja moyo lakini nakupa reality ya hali ilivyo.

Hilo la kuiuzia umeme Tanesco uliobakia unaongozwa na sheria za feed in tariff ambazo as far as I know sheria inawaruhusu kununua umeme kutoka tu kwa vyanzo vyenye a certain minimum production, chini ya hapo sheria haiwaruhusu kununua (Na ndio maana mtu mwenye solar panel umeme wake hawezi kuiuzia tanesco, au mwenye bio-fuel generator nyumbani)

Tunaweza kuanza kwa kulazimisha Tanesco kushusha viwango vyao vinavyolazimika kwa feed in tariff kwanza
 

Mkuu niko na wewe, there is no way we can pull ourselves out without forcing plan A to work. the question is how.....need a guide
 

Mhh nadhani haujanipata Gaijin hapa mimi ninaongelea short term solution na sio kwamba iwe the way to go.., bali ni symbolic.., na kama Tanesco wanaweza kununua au kukopa vyombo vya kuzalishia pengine basi na sisi wanajamii tunaweza tukawakopa mafuta yetu (pesa zetu) na watu wataendelea kulipia according to their meters na hapo wanajamii tunaweza kuidai Tanesco in the near future au tuka-minize tulichowakopa kwenye usage yetu... (mfano I we owe you 20,000/= our bill normally is 100/= a month therefore we owe you 200 months of service)

Lakini all in all in the long run huenda hii ikawa expensive solution lakini the first thing ni kuonyesha we can (as symbolic)... na hata kama kuwashauri Tanesco wapunguze feed in Tariff who is better to do... kama sio viongozi wetu..,
 

Mkuu jua kwamba unapoongea hata suala la kuchangia mafuta unaongelea asilimia 14 tuu ya watumiaji wa umeme
Sio watanzania wote wanafaidika na huo umeme unausemea na sio wote watakuwa tayari kufanya hilo unalotaka
Tunalotaka ni kujua kuwa uwezekano wa kuwa na uhakika wa umeme kwa watanzania wengi kwa pamoja na usambazaji uwafikie walengwa wengi na ndio hapo hilo la kwako unaweza kulisema
Ila kusemea asilimia 14 ya watanzania wafanye hilo unalolitaka mkuu n i pagumu sana
 
VoiceOfReason

Nilikuwa nakuonyesha hali kisheria ilivyo hata kama unataka Tanesco izalishe umeme kwa dakika tano. Ili usije ukakwama baina ya theories and practices.

Mfumo wa kumkopesha Tanesco na kukulipa labda service is a very complex system which practically is difficult to run

Juu ya hivyo iwapo ni kwa ajili ya kuonyesha as symbolic tu, hakuna kinachoshindikana, japokuwa ingekuwa Mimi Tanesco ningetumia vipengele vyote vya sheria vilivyopo kuzuwia hilo kutokea. Nisingeweza kuruhusu kutokeasymbolic tu at my expense.
 
duh, miaka 50 ya uhuru bado tunajadialiana kuhusu umeme (unaopatikana kwa wachache ca 20% ya watanzania), baada ya hapo tunahamia kwenye majadialiano ya uhaba wa sukari.
 
<br />
<br />
Hakuna haja ya kusubiri,wakati ni sasa na ninaamini hawataweza ku spin dhima ya uamuzi huo mgumu,tayari wananchi wamechoka...Wamechoshwa na ugumu wa maisha na sarakasi za hao tunaowaita viongozi wetu.Huku vijijini watu wamepigika mbaya wanasubiri kipenga kipulizwe,waingie mtaani!Kuwachangisha ni kuzidi kuwaongezea maumivu.
 

Ni kweli asilimia kubwa sana ya Tanzania haina umeme (na hapo tunahitaji long term solution.., sio kutatua tatizo la muda mfupi) lakini kwa sasa tupo on total blackout hata wale wachache ambao huwa wanapata umeme sasa hivi hawana umeme kwahiyo swali ni tunafanya nini kwa short term solution..? (sababu uchumi upo at a standstill)

long term hatuna njia bali ni kuwa-force Serikali iliyomadarakani ili ielekeze kodi zetu panapofaa ili tuweze kupata miradi ya maada na sio hii ya kuziba ziba inayofanyika sasa
 
<br />
<br />
Hatupaswi kuendelea kuweka makalio yetu chini na kuendelea kulalamika...Tumenung'unika sana,tumelalamika sana,sasa inatosha.Hatuna haja ya kuendelea tena kuumiza makoo yetu wala kuzidi kutia mikono mifukoni mwetu tukitafuta shilingi dhaifu (ambayo hata hivyo imekuwa adimu kwa wengi)ili eti tufanye jambo la mfano kwa watawala.Ni muda muafaka wa kutumia nguvu yetu ili kuleta mabadiliko chanya kwa ustawi wa taifa letu!
 

Kumbuka hapa Adui sio Tanesco bali ni serikali ambayo inaingilia kazi za Tanesco..., hivyo sababu hii itakuwa a political move as well as kuwawajibisha wenye serikali kwamba what they are doing is not good..., waache Tanesco wakatae ndipo hapo tutawaambia wananchi kuwa sisi wenyewe tumejaribu kusaidia lakini Tanesco/Serikali wamekataa..., alafu tuone kama hawa-sway the other way au serikali kuamka kutoka kwenye usingizi wao...
 

Mkuu wanasubiri waingie mitaani lini na kipenga atakipiga nani..?, kumbuka mpaka hivi sasa unachangishwa kwa kutumia either generator au kushindwa kufanya shughuli zako sababu hakuna umeme... (you are paying heavily already) kwahiyo labda nikuulize swali.. Je kuingia mitaani is it the only solution?..., na system ilivyo mbovu hivi sasa unaweza ukamtoa Kenge na Kumuweka Mamba (the all system is corrupt, na inahitaji massive changes)
 

Ndo maana nasema we need another step now hapa tulipo na tulilofanya linatutosha na tukiendeela na hali hii sioni kama kuna suluhisho na wala hatuna viongozi wenye utashi wa kutatua hali hii
TUnahitaji sasa solution ya hili tulilo nalo na sio kulalamika tena maana tutalalamika wee mpaka tutakuwa kama kasuku
 

tutaipata wapi au wapi inauzwa tukainunue kama mvua ya Lowassa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…