Mbuge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA Mhesimiwa John Mnyika ameeleza chazo cha kukosekana mara kwa mara kwa maji ya bomba katika maeneo ya Ubungo hadi Kimara, wakati bomba kuu la maji linapita maeneo hayo hayo. Mheshimiwa Mnyika amesema chanzo ni uozo wa kiutendaji uliopo katika Mamlaka ya Maji safi na maji taka DAWASCO, eneo la Kimara hadi Ubungo kwa kula njama na wafanyabiashara wa maji wenye malori hivyo kuzuia au kufunga maji katika maeneo hayo ili kuleta uhaba wa maji wa kujitakia na baadae wafanya biashara hao wa maji kuvuna mapesa ya chee kwa kuuza maji kwa bei ya juu sana.
Tayari baada ya kuligundua hilo Mheshimiwa John Mnyika amefanya juhudi za makusudi zilizopelekea meneja wa DAWASCO anaeshughulikia eneo hilo kutimuliwa kazi. Pia Mheshimiwa Mnyika ameitaka EWURA kudhibiti kikamilifu bei ya maji kwa mtumiaji wa kawaida. Amesema EWURA imeshikia bango bei za mafuta tu na kusahau bei za maji. Ambayo ni huduma ya lazima tena ni ya kila siku kwa kila mwanadamu.
Tayari baada ya kuligundua hilo Mheshimiwa John Mnyika amefanya juhudi za makusudi zilizopelekea meneja wa DAWASCO anaeshughulikia eneo hilo kutimuliwa kazi. Pia Mheshimiwa Mnyika ameitaka EWURA kudhibiti kikamilifu bei ya maji kwa mtumiaji wa kawaida. Amesema EWURA imeshikia bango bei za mafuta tu na kusahau bei za maji. Ambayo ni huduma ya lazima tena ni ya kila siku kwa kila mwanadamu.