Mhe Vincent Nyerere kutikisa mkoa wa Mara

Mhe Vincent Nyerere kutikisa mkoa wa Mara

Lai Otieno

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
311
Reaction score
90
Habari zilizotufikia muda sio mrefu kutoka Musoma Mjini nikuwa Mhe Vincent J Nyerere(Mb)wa Musoma mjini anatarajiwa kufanya ziara jimboni kwake kukaguwa miradi mbali pamoja na kufanya mikutano mtatu mikubwa jimboni Musoma mjini Mhe Vincent pia anatarajiwa kufanya mikutano mbali mbali mkoani pamoja na kanda ya ziwa ziara hiyo itanza atakvyo maliza ziara ya jimboni kwake..
 
big up sana makamanda,mapambano yanaendelea!
 
Mapambano ndiyo kwaanza yanaanza.
Safi sana kamanda nyerere jr.
 
Mwambie aingie na vijijini kabisa! Kule wanakoamini rais wa tanzania bado ni nyererd!
 
Kamanda Mara kwetu, Tafadhari kwa heshima na taadhima na kwa niaba ya wapenda mabadiliko wote wa Jimbo la Serengeti Mara, tunamwomba Mhe.Vincent Nyerere kwa kuwa ndiye Mlezi wa Jimbo letu la Serengeti tunamhitaji afanye ziara huku Jimboni kwetu hususani maeneo ya Vijijini ambako ndiko kuna wapigakura wengi wanaotuunga mkono.

Mfano Wananchi wa Kata za Nyansurura, Kisaka, Machochwe, Rung'abure, Kebancha, Nyamoko, Kitunguruma, Kisangura na baadhi ya maeneo ya Vijiji vilivyoko kandokando ya Hifadhi ya Serengeti kama vile Merenga n.k, Wananchi wa maeneo hayo wanamhitaji Mhe.Vicent wakiamini kabisa kwamba yeye ndiye anayeweza kuwafikishia Kilio chao kwa viongozi wa juu, tofauti na Mbunge wa sasa wa CCM ambaye Serikali ya Chama chake imebariki zoezi la Operation tokomeza iliyowaua ndugu zao bila hatia, huku ikiwafukuza kwenye ardhi yao ya tangu enzi za mababu zao mpaka leo ili kuwapisha wanyama wa porini.

Kwa tafsiri nyingine ni kwamba, Mbunge huyu wa Jimbo hili Stephen Kebwe, yeye na Chama chake wameamua kwa upamoja wao, kuwathamini wanyama wa porini wapate mahali pa kuishi kuliko wananchi ambao ndio wapigakura waliompa huyu Kebwe nafasi ya kuwa Mwakilishi wao, lakini amewasaliti na kupotea kabisa Jimboni, na amekwenda kuishi Dar Es Salaam, hivyo anatarajiwa kurudi tena nyakati za Uchaguzi mwaka kesho.

Mhe.Vicent Nyerere,
Kwa kuwa Wana-Serengeti wameonyesha Moyo wa hali ya juu wa kutuunga Mkono, ni wakati mwafaka sasa wa sisi kama Chama kuwa karibu nao ili kuwasikiliza kero zao ana kwa ana, ni muda mrefu sana Wakazi wa maeneo tajwa hapo juu wamekuomba uwafikie kwenye maeneo yao.

Hivyo tunaomba uitikie wito wao sasa na uweze kuwafikia Wakazi wa Serengeti ndani ya Ratiba ya ziara zako.
Naamini wananchi hawa watapata faraja sana ya kufikiwa na Mbunge wa Chama chao wanachokiunga mkono, tena Mbunge ambaye ni mmoja ya wana-ukoo wa Baba wa Taifa Mwl.Nyerere.

Ahsante sana, ni matumaini yetu Viongozi na Wanachama wa Chadema Serengeti kuwa, mara upatapo ujumbe huu utaufikiria namna ya kuitikia wito wa wapigakura wetu.

Na;
Katibu Mwenezi Chadema,
Kata ya Nyansurura,
Francis Garatwa,
Mugumu, Serengeti,
0767881009/0785881009.
06/07/2014.
 
Last edited by a moderator:
Kamanda Mara kwetu, Tafadhari kwa heshima na taadhima na kwa niaba ya wapenda mabadiliko wote wa Jimbo la Serengeti Mara, tunamwomba Mhe.Vincent Nyerere kwa kuwa ndiye Mlezi wa Jimbo letu la Serengeti tunamhitaji afanye ziara huku Jimboni kwetu hususani maeneo ya Vijijini ambako ndiko kuna wapigakura wengi wanaotuunga mkono.

Mfano Wananchi wa Kata za Nyansurura, Kisaka, Machochwe, Rung'abure, Kebancha, Nyamoko, Kitunguruma, Kisangura na baadhi ya maeneo ya Vijiji vilivyoko kandokando ya Hifadhi ya Serengeti kama vile Merenga n.k, Wananchi wa maeneo hayo wanamhitaji Mhe.Vicent wakiamini kabisa kwamba yeye ndiye anayeweza kuwafikishia Kilio chao kwa viongozi wa juu, tofauti na Mbunge wa sasa wa CCM ambaye Serikali ya Chama chake imebariki zoezi la Operation tokomeza iliyowaua ndugu zao bila hatia, huku ikiwafukuza kwenye ardhi yao ya tangu enzi za mababu zao mpaka leo ili kuwapisha wanyama wa porini.

Kwa tafsiri nyingine ni kwamba, Mbunge huyu wa Jimbo hili Stephen Kebwe, yeye na Chama chake wameamua kwa upamoja wao, kuwathamini wanyama wa porini wapate mahali pa kuishi kuliko wananchi ambao ndio wapigakura waliompa huyu Kebwe nafasi ya kuwa Mwakilishi wao, lakini amewasaliti na kupotea kabisa Jimboni, na amekwenda kuishi Dar Es Salaam, hivyo anatarajiwa kurudi tena nyakati za Uchaguzi mwaka kesho.

Mhe.Vicent Nyerere,
Kwa kuwa Wana-Serengeti wameonyesha Moyo wa hali ya juu wa kutuunga Mkono, ni wakati mwafaka sasa wa sisi kama Chama kuwa karibu nao ili kuwasikiliza kero zao ana kwa ana, ni muda mrefu sana Wakazi wa maeneo tajwa hapo juu wamekuomba uwafikie kwenye maeneo yao.

Hivyo tunaomba uitikie wito wao sasa na uweze kuwafikia Wakazi wa Serengeti ndani ya Ratiba ya ziara zako.
Naamini wananchi hawa watapata faraja sana ya kufikiwa na Mbunge wa Chama chao wanachokiunga mkono, tena Mbunge ambaye ni mmoja ya wana-ukoo wa Baba wa Taifa Mwl.Nyerere.

Ahsante sana, ni matumaini yetu Viongozi na Wanachama wa Chadema Serengeti kuwa, mara upatapo ujumbe huu utaufikiria namna ya kuitikia wito wa wapigakura wetu.

Na;
Katibu Mwenezi Chadema,
Kata ya Nyansurura,
Francis Garatwa,
Mugumu, Serengeti,
0767881009/0785881009.
06/07/2014.

kwani hujui Dr kebwe ni waziri hivyo anawahudumia watanzania wote? Hapo Serengeti kuna ofisi ya naibu waziri wa afya? Pambanua mambo kama kiongozi. Siyo unaandika ushabiki unajidhaulisha
 
Last edited by a moderator:
kwani hujui Dr kebwe ni waziri hivyo anawahudumia watanzania wote? Hapo Serengeti kuna ofisi ya naibu waziri wa afya? Pambanua mambo kama kiongozi. Siyo unaandika ushabiki unajidhaulisha

Mkuu umukurya punguza kuchanganya viroba na konyagi ndani ya Gongo utalewa vibaya sana, kwani kwa akili yako mgando unaamini kwamba mtu akiwa Waziri/Naibu Waziri ndo jukumu la kuwahudumia Wananchi Jimboni linakwama?

Kwani huyo Kebwe alianza lini kuwa Naibu Waziri, au umekurupuka toka usingizini, pima mawazo yako kwanza kabla ya kutuchafulia hali ya hewa humu ndani
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom