Mhe Sitta, Utaweka wapi sura yako?

Mhe Sitta, Utaweka wapi sura yako?

Pamoja na UKAWA kuwa ni wa vyama vya upinzani, lakini katika hili wameonyesha kidogo uzalendo wa kupigania maoini ya wananchi.

Inaelekea huelewi nini maana ya vyama vyama vya upinzanini na umuhimu wake katika demokrasia. Ni katika hizo juhudi za vyama vya upinzani ndio tumepata uamuzi wa kusitishwa baraza hili la katiba. Nachelea kusema kuwa changamoto ya hao wengine uliowataja ilikuwa ndogo sana au kutokuwepo kabisa!!
 
Sijaelewa Oktoba4 wanakula hela za bure tu, hii ni nn nyie TCD? Huu ni Ufisadi bhana. Ina maana wakikutana watajadili nini tena au wataanza upya. Maswali ni mengi kuliko majibu
 
Ni kweli Sita aliingizwa mkenge,mkuu wa kaya ndiye chanzo cha sakata lote hili,na sasa watu wanampongeza kwa kitu ambacho alijua mwisho wa siku kitakwama na yeye ndiye mkwamuaji,watanzania fungueni macho
Ni kawaida ya ccm kutengeneza tatizo halafu wakijidai kulimaliza sisi wananchi tunawapigia makofi - eti serikali sikivu!!!!
Tuachane na huu ujinga
 
Imekuaje leo mwanaCCM unakubaliana na UKAWA au hii sredi kuna mtu ameandika kwa niaba yako?

Mkuu nchi hii ni yetu sote wana CCM, CHADEMA, CUF,NCCR,Saa ya Ukombozi etc

Politics ni give and tske, na kwa suala la Katiba Mpya checks and balances lazima zitokane na katiba iliyo bora.

Kutngeneza katiba ya watu fulani ni hatari kwa uhai wa utaifa.
 
Umepewa nafasi ya kufanya uchaguzi na kupata wajumbe wapya kwa bmk lijalo. Ni juu yako kuwaondoa hao waliopindisha mawazo ya wananchi na kuweka ya kwao. Hii ni fursa nzuri - tuitumie.
Usisahau pia kuwa tutakuwa na rais mwingine ambaye si lazima aje na mawazo kama ya JK. Kumbuka mbunge mmoja aliwahi kusema " anayeshikila nguvu za dola (instruments of power) ndiye mwenye uwezo wa kusema katiba mpya iwepo na ikawa au sitaki katiba mpya na ikawa. Alitoa mfano wa Afrika ya kusini

Ni sawa mkuu, lakini tutakapo urejea tena(resume) huu mchakato tutaanzia kwenye hatua gani? Ya kura ya maoni ama ya majadiliano tena bungeni?

Ikiwa tutaendelea na kura ya maoni, huoni kwamba tutaenda kukipigia kura kitu ambacho hakijatokana na maoni ya wananchi?Si UKAWA watakuwa wapuuzi wote kususia vikao vya BMK, then washiriki kwenye mchakato huo mwishoni!
Na ikiwa tutaanza na mijadala upya si tutakuwa tumechezea bure pesa za wavuja jasho wa nchi hii bila ya matunda tarajiwa?

Tutafakari kwa kina suala hili.
Ningeiona busara kama BMK lingesitishwa mara moja baada ya kutolewa maazimio ya kikao cha majadiliano kati ya TCD na Rais wa nchi.
 
Pigo siyo kwa Sitta maana yeye alipewa maelekezo kasimamie moja, mbili, tatu.........hicho kikundi kilichotoa maelekezo ya mpaka Raisi afungue Bunge baada ya Rasimu kuwasilishwa na kufutilia mbali tovuti ya Tume ingefaa hiyo majina yao yawekwe wazi ili Watanzania wawafahamu.

Mimi wa kwanza ni Waziri wa Katiba na Sheria - Asha Rose Migire, Tovuti iko wizarani kwake

Asha Rose Migiro anakesi ya kujibu hapo. Hafai kuwa kiongozi wa wananchi pengine apewe uongozi wa kikundi change cha magamba.
 
Back
Top Bottom