Mhe. Rais Magufuli, usikubali Usalama wa Taifa kudhalilika

From Sir With Love

JF-Expert Member
Sep 13, 2010
2,076
3,797
Pole na Majukumu ya ujenzi wa Taifa Mhe. Rais

Nina ushauri mdogo kwako kama kiongozi wangu wa Nchi, na nishukuru mitandao ya kijamii kunipa hii fursa.

Naomba nijikite kwenye swala la "MTU MMOJA" kumtolea bastola Mhe. Nape siku alipokuwa akutane na waandishi wa habari.

Nilikuelewa ulivyosema huyo "MTU MMOJA" sio serikali, Kosa lake lisiwe kosa la serikali nzima. Nakubaliana na wewe asilimia mia moja. Ikiwezekana abebe lawama, kama vile Cleophace Simon alivyobeba lawama kule Iringa.

Kuna picha zinazunguka kwenye mitandao ya kijamii, zikionyesha wale vijana, waliokuwa wanamwomba Mhe. Nape arudi kwenye gari. Mengi yamesemwa, na mengi yatasemwa. "Vijana wetu" wanafanya kazi ngumu sana, na zingine zinawaingiza matatani kwa kujulikana kirahisi na kwa kitu ambacho kingezuiwa.

Kuna madoa kama matatu, ambayo yatakumbukwa na wananchi, kuhusiana na idara. Ni vizuri haya matukio yakawa case studies kwenye masomo.

Mosi ni swala la Ulimboka, pili ni kifo cha ofisa usalama wa taifa, Ndugu Peter Tyenyi kufia kwenye kisima cha maji pale kijitonyama na sasa swala la "MTU MMOJA" kutoa bastola mchana kweupe na kumtishia aliyekuwa Waziri wako wa habari.

USHAURI:

1. Ni vizuri unapopewa briefings za kila siku ukumbushie "vijana wetu" kufanya kazi kwa ueledi ili wananchi wasiwe na dhana potofu.

2. Kazi ya kumwomba Mhe. Nape arudi kwenye gari, ingefanywa na mtu mwenye umri mkubwa na utashi ungetumika. Waswahili wanasema mtu mzima dawa.

3. Mwaka 2011 ulipokuwa Waziri wa Ujenzi, kuna tetesi zilienea unataka kujiuzulu. Lakini baadaye hizi habari zilikanushwa. Nimekumbushia hilo kwa sababu, ungemuita Mhe. Nape, uongee naye na haya yote yasingetokea. Pamoja na hayo naheshimu uamuzi wako.

Naomba nimalizie Mhe. Rais kwamba, kuna wakati huwa tunawapa chai watoto wetu kwenye vikombe vya glasi. Ukiona mwanao amedondosha "glasi" mara mbili au tatu, basi mbadilishie kikombe na umpe cha "udongo". La sivyo Mhe. Rais utagombana na marafiki zako watakapo mwagiwa chai na mwanao kwa sababu hawezi kuhimili kutumia glasi.

Nikutakie kazi njema.

Ni mimi mwananchi wa kawaida.
 
Hao vibaka wa Bashite lazima washitakiwe
Daudi, yameshapita, tumpe Rais wetu ushauri. Ukitaka kumkosoa Mhe. Magufuli mweleze kwa upole.

Haiba ya Rais, ni ya wale watu ambao wanapenda kitu kifanyike na kionekane.
Wakiamua kitu, wameamua. Na ili watengue waliyoyasema, lazima waamue wenyewe. La sivyo, kuwaambia kwa ustaarabu ndiyo jawabu.
 
Enzi zetu ukisikia usalama wa taifa unaanza kuimagine huyo bwana atakuwaje!
Walikuwa hawaonekani kizembe!

Kama hawa waliotumwa na bashite wanaotoa bastola kwenye tako la kushoto nao ni usalama wa taifa.......Basi tumuombe Mungu tu atulinde lasivyo tumekwisha!

Inaonekana ni watupu kabisa kichwani
 
kuna wakati huwa tunawapa chai watoto wetu kwenye vikombe vya glasi. Ukiona mwanao amedondosha "glasi" mara mbili au tatu, basi mbadilishie kikombe na umpe cha "udongo". La sivyo Mhe. Rais utagombana na marafiki zako watakapo mwagiwa chai na mwanao kwa sababu hawezi kuhimili kutumia glasi.

Atakujibu mtoto anakua,ana uhuru wa kuvunja vikombe,huna mamlaka ya kunishauri to that extent,watch it!!
 
Enzi zetu ukisikia usalama wa taifa unaanza kuimagine huyo bwana atakuwaje!
Walikuwa hawaonekani kizembe!

Kama hawa waliotumwa na bashite wanaotoa bastola kwenye tako la kushoto nao ni usalama wa taifa.......Basi tumuombe Mungu tu atulinde lasivyo tumekwisha!

Inaonekana ni watupu kabisa kichwani
Ila Ngushi, sijasema ni usalama wa taifa. Usininukuu.

Lakini pia aliyetoa bastola, hakuamriwa kufanya hivyo.
 
kuna wakati huwa tunawapa chai watoto wetu kwenye vikombe vya glasi. Ukiona mwanao amedondosha "glasi" mara mbili au tatu, basi mbadilishie kikombe na umpe cha "udongo". La sivyo Mhe. Rais utagombana na marafiki zako watakapo mwagiwa chai na mwanao kwa sababu hawezi kuhimili kutumia glasi.

Atakujibu mtoto anakua,ana uhuru wa kuvunja vikombe,huna mamlaka ya kunishauri to that extent,watch it!!
Mkuu una bonge la sense of humor
 
Hatua zimeshachukuliww si lazima uambiwe ni hatua gani
Nafarijika kusikia hivyo. Japo kuna watu tofauti duniani.

Kuna mtu anapenda kazi ya field na mwingine kazi ya ofisini

Kumrudisha mtu ofisini wakati huwa anafanya vizuri field, utakuwa hujamtendea haki.
 
Usalama wa taifa mi jeshi kama yalivyo majeshi mengine utofauti wao hawavai uniform/combat ingawa wanazo(nenda kijito nyama). Hivyo suala la uzalendo sijui siasa linakuja baadae, wakishapewa order lazima itekelezwe maelezo baadae.

Utaratibu wa utekelezaji kwa ndio changamoto maana hawapaswi kuonekana.

Alichokifanya yule dogo naweza kusema ni sawa na kumpa mtoto chai kwenye kikombe cha bati na yeye bila kuangalia mazingira akanyanyua ma kuweka mdomoni. Watch it....
 
Back
Top Bottom