Mhe. Rais Magufuli, Anza na Kusaini Hati za Wote Waliohukumiwa Kifo, Wanyongwe Haraka Haraka Mpaka..

Mhe. Rais Magufuli, Anza na Kusaini Hati za Wote Waliohukumiwa Kifo, Wanyongwe Haraka Haraka Mpaka..

Yale Mashati yako ya PPRA huna hata ya akiba unipe na Mimi mojawapo? Nayapenda sana Mkuu japo naona yote ni XXL wakati Mimi ni ' Kimbaumbau ' tupu.
Há ha! , sio PPRA, ni PPR.
zile shati ni uniform za ile ofisi.
P.
 
paschal ungekuwa wewe mfano uko gerezani na umehukumiwa kunyongwa ,halafu nje kuna debate inaendelea unyongwe Au usinyongwe, nadhani ungeelewa na kwa akili yako ungekubali bora unyongwe ,ila sikufichi kuna waliohukumiwa kunyongwa bado wanaamini IPO Siku wataachiwa huru, inahitaji uvae uhusika then ndo utoe mchango wako
Mkuu Durant, please take time kanisome kwenye bandiko langu hili.
Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo

Adhabu ya Kifo: Jee kweli bado inahitajika?

Paskali
 
ha! we inakufaidisha nini..?
halafu mbona umekomalia au una lako jambo..
ingelikuwa mmoja wa ndugu yako yuko kwenye hilo kundi ungejisikiaje.. haya mambo hayahitaji haraka wengine humo usikute wamebambikiwa na wewe unasapoti tu.

kwa maamuzi ya mkulu jinsi yalivyo mi naomba apunguziwe baadhi ya madaraka maana tutaisoma kwelikweli
Pasco sounds satirical.
 
Yule aliyekutwa na hatia ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini Bagenyi vipi, maana tulisoma hapa jf kwamba amehukumiwa kunyongwa hadi kufa.
 
Ukitulia ukatumia busara na akili utaelewa paskali ana maana gani
Kuna tofauti kubwa kati ya wivu na usongo
 
Uthubutu katika ishu hii si jambo dogo, sidhani kama utekelezaji wake ni mwepesi kama unavyodhani mkuu.
 
acha upunda ndugu fanya lile lililo halali...naona unalalama lalama tu hapa mbona utuambii kuwa huyo aliekamatwa china pia alipeleka sumu ili wenzie wafe,ukiburi wako ndo umauti wako utachezea tanzi tu.
mtu akikosea suluhisho sio kumuua, ukiona wewe unashabikia mtu afe ujijue kuwa sio sawa na wanadamu wengine, una roho ya ukatili. subiri watoto wako au ndugu zako waje wafanya makosa yanayosababisha kunyongwa hadi kufa ndio utaona uchungu wake. kwasasa hauwezi kuelewa kitu hadi yakukute ndugu. every human being is to be given a second chance, kama Mungu angekuwa anaua kila anayefanya makosa hata wewe hapo ungeshauawa zamani sana kwasababu haupo salama. umefanya madudu mangapi tangu umezaliwa hadi leo, yale ya sirini...lakini Mungu amekuacha hai hadi leo...worse enough pamoja na kupata neema ya kuishi bado unashabikia mwanadamu mwenzio auawe. ndizo roho za watu walio wengi siku hizi. badilika.
 
Mi nimekuelewa vizuri sana Pascal.
Uandishi wako ni wa fasihi ya hali ya juu sana
 
Pasco, are you serious? Unataka wanyongwe ama unataka JPM asaini? Kuna uzi mwingine pia umejaribu kusema kuwa huruma ya JK ni udhaifu hasa kwa kutopenda watu wanyongwe! Kwa Mantiki hiyo Nyerere alikuwa dhaifu sana kwa kuwa aliidhinisha unyongwaji muuaji wa rafiki yake Dr. Kleruu na Mkapa pia alikuwa dhaifu zaidi kwa kuwa hakuidhinisha unyongwaji. Madikteta wote wanashabikia unyongwaji na kwa kweli ni wauaji!
Nilimsikia Nyerere katika hotuba yake moja akieleza kwanini hakupenda wakosaji waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa wanyongwe. Alisema kuwa mkosaji huyu amehukumiwa kunyongwa kwa kuwa alimuua mtu. Na hilo ni kosa kubwa sana lenye adhabu ya kiwango kikubwa sana. Alisema, "Mimi nikiruhusu kuwa mkosaji huyu anyongwe, maana yake na mimi nafanya kosa lile lile alilofanya! Aliua mtu na mimi naruhusu kuwa auwawe kwa hiyo tuko sawa hapa. Wote ni wauaji. Sheria si kigezo kwa kuwa sheria hizi tumetunga sisi, na kwakweli mwenye ruhusa ya kuuondoa uhai wa mtu ni yeye aliyeuweka ambaye ni Mwenyezi Mungu!" Pia alitoa sababu nyingine kuwa mtu akiua mtu, taifa limepoteza raia mmoja. Tukiruhusu aliyeuwa naye auwawe maana yake taifa linapata hasara ya watu wawili. Lakini pia nani aliyewahi kuonja mauti akarudi ili atuambie kuwa adhabu ya kumuua mtu inalingana na kosa lake la kuumuua mtu?
Huenda huo ndio ulikuwa udhaifu wa Nyerere na ndio udhaifu(?????) wa Kikwete! Ila mimi naamini kuwa kumsamehe mtu ni moja ya evidence za maturity. Mtu dhaifu hawezi kumsamehe mtu. Ni mtu mjasiri tu na mkomavu wa nafsi ndiye anayeweza kusamehe. Ni ngumu sana kwa mwanaume mdhaifu kumsamehe mkewe anapokosea. Ni mwanaume mkomavu tu ndiye awezaye! Tabia za kulipiza kisasi, ubabe, kutumia nguvu badala ya hoja, kuamrisha badala ya kujadiliana na kutumia nguvu ya ushawishi, kuzira, kulalamika, kusingizia wengine, kutokuwajibika n.k. zinaonyesha kuwa mhusika ni dhaifu kwa ndani na kwa nje ana compplement udhaifu huo na udikteta. Kikwete hakuwa dhaifu!!!
Comment nzur sana mungu akubariki
 
Hayo ya chini tu ndio
Pasco, are you serious? Unataka wanyongwe ama unataka JPM asaini? Kuna uzi mwingine pia umejaribu kusema kuwa huruma ya JK ni udhaifu hasa kwa kutopenda watu wanyongwe! Kwa Mantiki hiyo Nyerere alikuwa dhaifu sana kwa kuwa aliidhinisha unyongwaji muuaji wa rafiki yake Dr. Kleruu na Mkapa pia alikuwa dhaifu zaidi kwa kuwa hakuidhinisha unyongwaji. Madikteta wote wanashabikia unyongwaji na kwa kweli ni wauaji!
Nilimsikia Nyerere katika hotuba yake moja akieleza kwanini hakupenda wakosaji waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa wanyongwe. Alisema kuwa mkosaji huyu amehukumiwa kunyongwa kwa kuwa alimuua mtu. Na hilo ni kosa kubwa sana lenye adhabu ya kiwango kikubwa sana. Alisema, "Mimi nikiruhusu kuwa mkosaji huyu anyongwe, maana yake na mimi nafanya kosa lile lile alilofanya! Aliua mtu na mimi naruhusu kuwa auwawe kwa hiyo tuko sawa hapa. Wote ni wauaji. Sheria si kigezo kwa kuwa sheria hizi tumetunga sisi, na kwakweli mwenye ruhusa ya kuuondoa uhai wa mtu ni yeye aliyeuweka ambaye ni Mwenyezi Mungu!" Pia alitoa sababu nyingine kuwa mtu akiua mtu, taifa limepoteza raia mmoja. Tukiruhusu aliyeuwa naye auwawe maana yake taifa linapata hasara ya watu wawili. Lakini pia nani aliyewahi kuonja mauti akarudi ili atuambie kuwa adhabu ya kumuua mtu inalingana na kosa lake la kuumuua mtu?
Huenda huo ndio ulikuwa udhaifu wa Nyerere na ndio udhaifu(?????) wa Kikwete! Ila mimi naamini kuwa kumsamehe mtu ni moja ya evidence za maturity. Mtu dhaifu hawezi kumsamehe mtu. Ni mtu mjasiri tu na mkomavu wa nafsi ndiye anayeweza kusamehe. Ni ngumu sana kwa mwanaume mdhaifu kumsamehe mkewe anapokosea. Ni mwanaume mkomavu tu ndiye awezaye! Tabia za kulipiza kisasi, ubabe, kutumia nguvu badala ya hoja, kuamrisha badala ya kujadiliana na kutumia nguvu ya ushawishi, kuzira, kulalamika, kusingizia wengine, kutokuwajibika n.k. zinaonyesha kuwa mhusika ni dhaifu kwa ndani na kwa nje ana compplement udhaifu huo na udikteta. Kikwete hakuwa dhaifu!!!
Para ya mwisho tu ndio umevuruga. Otherwise nami niungane nawe Kunyongwa hapana! Kwani adhabu ya Kifungo tu ninaiona ni adhabu kubwa mnoooo kubwa mno. Just imagine uko ndani na unapewa vitu vyoote- Chakula kizuri, mahali pazuri pa kulala, unaoga vizuri lakini tu huruhusiwi kutoka hapo ulipo. Ni adhabu kubwa mno kwa ulimwengu huu ulioo unaitoa kwa wahalifu, sasa kwa nchi zetu adhabu mara mbili kutokuwa na uhuru na sehemu za wafungwa si nzuri jamani adhabu ya kifungo ni adhabu tosha.
 
Jino kwa jino....Mh. rais wetu mpendwa na kipenzi cha Mungu ayasign tu ili hao wahalifu wanyongwe....namuunga mkono rais wangu.
 
Nafikri si busara sana kuendelea kumshushia hadhi rais mstaafu. yake yamepita
 
ha! we inakufaidisha nini..?
halafu mbona umekomalia au una lako jambo..
ingelikuwa mmoja wa ndugu yako yuko kwenye hilo kundi ungejisikiaje.. haya mambo hayahitaji haraka wengine humo usikute wamebambikiwa na wewe unasapoti tu.

kwa maamuzi ya mkulu jinsi yalivyo mi naomba apunguziwe baadhi ya madaraka maana tutaisoma kwelikweli
Suala si ndugu yake kuwemo kwa wanaosubir kunyongwa. Suala ni je huyo ndg alifanya nini. Kuna makosa haki pekee anayoweza kupewa mhusika ni kumpunguza dunian. Hatar kubwa imekuwa ni mfumo wetu wa kutoa haki na ushahid usio na shaka.
 
unawaagiza wenzako watimize ahadi ya kunyonga haraka sana, wakati wewe unaogopa kusaini wa kwako wanyongwe na wengine ni kwa makosa ya mauaji na sio unga
 
Back
Top Bottom