Mhe. Rais Dkt. Magufuli Hongera, Mkutano wa Paris. Ushauri wangu

duocore

Member
Aug 27, 2012
55
4
Natoa hongera zangu kwa Mhe. Dkt. John Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni siku chache tangu aapishwe katika nafasi hiyo na mabadiliko yameanza kuonekana.

Hivi sasa kuna mkutano wa kimataifa unaendelea huko Paris kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi. Mhe. Rais nchi yetu pamoja na kuanza kupata athari za mabadiliko ya tabia ya nchi lakini bado mungu ametujalia kupata mvua kwa kiasi.

Mimi kwa mtazamo wangu hatujafikia kiwango cha kupata athari kubwa (significant) kwa kiasi hicho. Mhe. Rais kwa utashi wa kisiasa ulionao nashauri kwa mvua kidogo tunazozipata viongozi katika maeneo yao wapande miti kwa kasi.

Pia tutumie nguvu kazi iliyopo magerezani kama sehemu ya kurekebisha tabia ya wafungwa kulitumikia taifa wa kupanda miti, kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Pia Mhe. Rais suala la mrahaba unaotolewa na makampuni mbalimbali kama Corporate Social Responsibility imekuwa ni kama hisani wakati ni suala la lazima.

Nakutakia utekelezaji mwema wa kazi za kuwatumikia wananchi wa Tanzania. Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania:lock1:

Magufuli Hoyeee!!
 
Yababa weeeeeeeeeeeee, aiiiiiiiiiiiiiiii! ataongea nini? Atatumia lugha gani? Rais wangu ni lowasa time will tell.
 
Yababa weeeeeeeeeeeee, aiiiiiiiiiiiiiiii! ataongea nini? Atatumia lugha gani? Rais wangu ni lowasa time will tell.

Wew kweli ni litoto na fisadi...unamtaja nani hapo juu....ivii urais unazani unapewa kama pipi dukani...
 
Yababa weeeeeeeeeeeee, aiiiiiiiiiiiiiiii! ataongea nini? Atatumia lugha gani? Rais wangu ni lowasa time will tell.

Yarabi toba! Lowassa ndiyo kitu gani tena jamani hapa Tanzania? Ni aina ya kontena la Bakhresa au nini vile?
 
Lowasa ni rais wa fb whatsapp na twitter, Rais wa Watanzania ni John Pombe Magufuli!!

Ni kweli kabisa Myao wa Kaskazini maana kuna watu bado wanaota Lowassa kuwa rais na ndio maana wameona aibukie kwenye mwili wa marehemu Mawazo huku wakifanya show na spare tyre yake Sumaye. Tume wakamata pabaya maana hawajui kwamba ni siku chache tu zimebaki hao mabwana zao wataumbuliwa. God bless Magufuli, God bless Tanzania.
 
Hakuna La Maana Hko Paris ,makomeo Ame2mia Akili Kutokwenda ,pia Amesave Pesa ,hko Viongoz Watakula Na Kunywa Tu ,maana Wachafuz Wakubwa Wa Mazingira Hawatak Kuacha, Usa, China. Angekuwa Mkwele Angekwenda Wiki 2 Kabla Ya Mkutano. Na Ukizngatia Shambuliz Walojishambulia Wafaransa Wenyewe Na Kuanza Kulaumu Waislam ,Hapo Ndo Shda Nyngne ,Pia Ugaidi Huo Ungetokea Katika Nchi Zetu Wazungu Wangeambizana Hakuna Kusafir Kwenda Afrika! Lakn Haitashangaza Kuona Viongoz Wa Afrka Wemejaa Hko Kanakwamba Nawao Wanaviwanda Vinavyochafua Mazingira , Si Kwamba Mkutano Huo Ni Mbaya Sanaaa Mmh
 
Yababa weeeeeeeeeeeee, aiiiiiiiiiiiiiiii! ataongea nini? Atatumia lugha gani? Rais wangu ni lowasa time will tell.
ha ha ha ha
raisi wako ndo yule alisema kuna teknolojia ya kutengeneza mvua:bump2:kuna watu ni wajinga lakin wengine ni wajinga zaidi
 
Kama moja ya kinga dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi, inabidi nchi iwekeze katika kuhifadhi chakula cha kutosha.

Nakumbuka kuna wakati Pinda alikwenda Poland na aliongelea suala la kujenga maghala ya chakula hasa nafaka. Kwa usalama wa nchi, ni vyema Tanzania ikajenga grain reserves za kutosha. lengo linaweza kuwa kuhifadhi nafaka za kutosha kutumia miaka mitano kukabili dharula au janga lolote.

Kuna faida nyingi kufanya hivyo. Kwanza kuwapa soko la ukahika wakulima wetu kwa kipindi hicho. Pili, kutokuwa na haja ya kuagiza nafaka nje ikitokea ukame. Tatu, kuweza kuziuzia nchi ambazo zitahitaji nafaka hizo siku za usoni.

Japan walifanya mambo kama hayo baada ya vita kuu ya pili. Ule mchele maarufu kama kitumbo ulikuwa unatoka kwenye hifadhi kama hizo.
 
Hakuna La Maana Hko Paris ,makomeo Ame2mia Akili Kutokwenda ,pia Amesave Pesa ,hko Viongoz Watakula Na Kunywa Tu ,maana Wachafuz Wakubwa Wa Mazingira Hawatak Kuacha, Usa, China. Angekuwa Mkwele Angekwenda Wiki 2 Kabla Ya Mkutano. Na Ukizngatia Shambuliz Walojishambulia Wafaransa Wenyewe Na Kuanza Kulaumu Waislam ,Hapo Ndo Shda Nyngne ,Pia Ugaidi Huo Ungetokea Katika Nchi Zetu Wazungu Wangeambizana Hakuna Kusafir Kwenda Afrika! Lakn Haitashangaza Kuona Viongoz Wa Afrka Wemejaa Hko Kanakwamba Nawao Wanaviwanda Vinavyochafua Mazingira , Si Kwamba Mkutano Huo Ni Mbaya Sanaaa Mmh
Jamani hamkufahamu alichokiandika mtoa mada au mmekurupuka?

Mtoa mada ametaja tu, Mkutano wa Paris na kuoanisha na ushauri wake kwa Raisi Pombe wa magufuli.

Mkutano wa Paris unahusu uhifadhi wa mazingiza ili kukabiliana na athari za mabadiliko tabia nchi.

Mtoa mada hakutaka Magufuli aende Paris wala Tokyo.

Wazo la kupanda miti ni wazo zuri. Ile siku ya 9 desemba itumike kufanya usafi na kupanda miti.
 
wafungwa kweli watumike kupanda miti na kufanya usafi, siyo kula kodi zetu bure bure tu
 
Hakwenda Paris! Kama ni wengine, saa hizi ametinga huko na msafara wa watu 20 eti kuzungumzia mazingira! Kama namsikia: " "Two southand years from now we will be dead if..." Mungu aiepushie TZ jinamizi lile tena.
 
Asante ndugu kwa kutoa ufafanuzi wa hoja yangu kwa mheshimiwa Dkt. Magufuli. Kimsingi hapa tulipofikia tumempata mchapa kazi. Kwa mtazamo wangu bado hatujafikia pahala pa kuanza kusingizia suala la mabadiliko ya tabia ya nchi. Bado tuna nafasi ya kufanya mabadiliko kwa kuangalia pia hatua tunazopitia kuelekea maendeleo, sera pamoja na mikakati mbalimbali. Hili ni pamoja na viongozi wetu wa Afrika kupata sauti kwa mataifa ya magharibi juu ya uharibifu wa tabaka la hewa ukaa. Kwa pamoja tunaweza kupaza sauti zetu. Kama nilivyooleza awali fursa bado ipo kwa nchi yetu kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi bila kuhitaji fedha za kigeni
 
Back
Top Bottom