Mhe. Mengi ondoa tangazo la kulazimisha ngono ITV

Mbwambo

JF-Expert Member
Nov 25, 2008
625
93
Nina uchungu mkubwa kuona kwamba mheshimiwa Mengi anakubali kutangazwa tangazo lakulazimisha ngono litangazwe kwenye kituo chake cha itv.

Mheshimiwa , mimi nakuamini kwamba una heshima na unapenda uelemeishe jamii sambamba na kusadia jamii katika michango mbali mbali ya maendeleo yao. Na sikuamini kuona umetoka kupewa tuzo kubwa sana hivi karibuni ambalo unastahili lakini unakubali jamii yako ya kitanzania ifedheheshwe kwa tangazo la kulazimisha ngono. Kweli watu wengi tumejisikia vibaya sana kwamba kweli jamii imeelimishwa au watoto na vijana wamefundishwa jinsi wazazi wao wanavyolazimishana kufanya tendo hilo? Kweli linatolewa tena kwenye vipindi vya taarifa za habari ambapo sisi walala hoi hatuna tv zetu wenyewe na watoto zao wenyewe hivyo inapokuja taarifa ya habari saa mbili mimi nakosa raha na ninashindwa hata kuondoka nitaona wapi taarifa ya habari?

Nakuomba mheshimiwa Mengi ondoa tangazo hilo haliwasaidii watoto na vijana wa kitanzania
ninakuheshimu sana na ninapenda sana itv kuliko tv zingine
naamini utaliondoa kwa busara zako nyingi ulizo nazo
asante na mungu akubariki
 
Nina uchungu mkubwa kuona kwamba mheshimiwa mengi anakubali kutangazwa tangazo lakulazimisha ngono litangazwe kwenye kituo chake cha itv.

Mheshimiwa , mimi nakuamini kwamba una heshima na unapenda uelemeishe jamii sambamba na kusadia jamii katika michango mbali mbali ya maendeleo yao. Na sikuamini kuona umetoka kupewa tuzo kubwa sana hivi karibuni ambalo unastahili lakini unakubali jamii yako ya kitanzania ifedheheshwe kwa tangazo la kulazimisha ngono. Kweli watu wengu tumejisikia vibaya sana kwamba kweli jamii imeelimishwa au watoto na vijana wamefundishwa jinsi wazazi wao wanavyolazimishana kufanya tendo hilo? Kweli linatolewa tena kwenye vipindi vya taarifa za habari ambapo sisi walala hoi hatuna tv zetu wenyewe na watoto zao wenyewe hivyo inapokuja taarifa ya habari saa mbili mimi nakosa raha na ninasindwa hata kuondoka nitaona wapi taarifa ya habai?

Nakuomba mheshimiwa mengi ondoa tangazo hilo haliwasaidii watoto na vijana wa kitanzania
ninakuheshimu sana na ninapenda sana itv kuliko tv zingine
naamini utaliondoa kwa busara zako nyingi ulizo nazo
asante na mungu akubariki

Ndugu yangu katika ulimwengu huu watoto huwezi ukawaficha haya masuala na ukaamini hawatafahamu hilo Tangazo hata wao pia linawahusu maana nao ni wanandoa watarajiwa. Miaka ya sasa ni tofauti kabisa na miaka ya zamani tulikuwa tunadanganywa kwamba watoto hutolewa chini ya mwamba Mkubwa na tulikuwa tunaamini mpaka tukiwa na Umri wa miaka 10+. Leo hii mdanganye mtoto ujinga huo atakuchora tuu maana anafahamu fika ili mtoto azaliwe lazima watu wawili wa jinsia tofauti wajamiiane.
 
Ndugu yangu katika ulimwengu huu watoto huwezi ukawaficha haya masuala na ukaamini hawatafahamu hilo Tangazo hata wao pia linawahusu maana nao ni wanandoa watarajiwa. Miaka ya sasa ni tofauti kabisa na miaka ya zamani tulikuwa tunadanganywa kwamba watoto hutolewa chini ya mwamba Mkubwa na tulikuwa tunaamini mpaka tukiwa na Umri wa miaka 10+. Leo hii mdanganye mtoto ujinga huo atakuchora tuu maana anafahamu fika ili mtoto azaliwe lazima watu wawili wa jinsia tofauti wajamiiane.

teh teh teh duuu mkubwa umenikumbusha mbali sana .Watoto tulidanganywa sana aiseee
 
Hata mi najiskia vibaya sana nionapo tangazo hilo pembeni yuko Mkwe, mtoto, mume yani ni aibu na utovu wa nidhamu wa hali ya juu sana, TUSIENDELEE KUFUMBIA MACHO MMOMONYOKO HUU WA MAADILI.
 
Ndugu yangu katika ulimwengu huu watoto huwezi ukawaficha haya masuala na ukaamini hawatafahamu hilo Tangazo hata wao pia linawahusu maana nao ni wanandoa watarajiwa. Miaka ya sasa ni tofauti kabisa na miaka ya zamani tulikuwa tunadanganywa kwamba watoto hutolewa chini ya mwamba Mkubwa na tulikuwa tunaamini mpaka tukiwa na Umri wa miaka 10+. Leo hii mdanganye mtoto ujinga huo atakuchora tuu maana anafahamu fika ili mtoto azaliwe lazima watu wawili wa jinsia tofauti wajamiiane.

.
Akili za namna hii ndizo zilizoshusha miaka ya kuishi ya binadamu mpaka sasa wastani wa kuishi wa baazi ya nchi umefikia miaka 35 kutoka 900 ya kina Adamu.
Kwa nini tukubali kuwa waovu? Uovu ni mambo mema ambayo mtu anafahamu kuwa anapaswa kufanya, lakini hata hivyo hafanyi. Tunafahamu kuwa kuna haki ya kuwalinda watoto wetu na masuala ambayo hawapaswi kuyafahamu kwa ujuzi wake kabla ya wakati wao yaani umri unaoruhusu. Mojawapo ya mambo hayo ni suala la mahusiano ya ngono. Ni kweli kwamba kuna vipindi ambavyo tunawalinda watoto wetu wasivifuatilie katika Tv. Sasa hata taarifa ya habari tuwahami wasifuatilie? Maana ndiko mlikopeleka hili tangazo lisiloheshimu mila na utamaduni wetu sisi waafrika tuwapo na familia zetu zilizochanganyikana.
Kingine ni Uasi. Uasi ni mambo ambayo tunafahamu hatupaswi kufanya lakini hata hivyo tunayafanya. Sii kweli kwamba Mengi na ITV hawajui kuwa hawapaswi kujjadili ama kuashiria ashki za kingono mbele ya under age. Hivyo kutekeleza vitendo hivyo kwa Mengi na Tv yake mbele ya under age ni uasi. Ni uasi kwa mila zetu, ni uasi kwa tamaduni yetu na ni uasi kwa ulinzi wa watoto wetu. Maana yake kuliweka tanzazo hili ndani ya mda wa Taarifa ya habari ni nini?
.
 
Back
Top Bottom