wakati wabunge wa upinzani wakileta vurugu bungeni kumzuia waziri w nishati na madini, Simbachawene alipokuwa akisoma muswada w mfut na gesi nilimsikia mbunge wangu Tundu Lisu akilopoka huku akisema namnukuu "kamwambieni Obama hatutaki gesi yetu" kwanza kabisa nilishangaa kwa mbunge wangu huyu ambaye kitaaluma ni mwanasheria na wakili maarufu hapa nchini kuvunj taratibu za bunge kwa kuropoka na kuzomea kiasi cha kumfanya spika ashindwe kufanya kazai yake na kuahirisha bunge.
nikawa najiuliza zaidi na zaidi kuwa je wana singida mashariki na ikungi kwa ujumla je tulikosea kumchagua Lissu? maana muda mwingi Lissu amekuwa akipenda kuendesha malumbano ndani ya bunge na miongozo ambayo haina maslahi na wana ikungi,
ikiwa mbunge wangu Lissu anauchungu na rasilimali za nchi mbona huna uchungu na posho na kiinua mgongo ambacho mmepandishiwa kutoka milioni 94 mpaka milioni 230, mbona hatukusikii kulaani mamilioni hayo ya kiinua mgongo kama kweli una uzalendo wa kupinga ufisadi?
Lissu mbunge wangu kama unauchungu na rasilimali za wsatanzania vipi mabilioni ya ruzuku yz chadema au sio kodi ya watanzania ambayo tumewahi kusikia wakubwa wakikopeshana na kuyatafuna rejea ripoyti ya CAG
Lissu mbunge wangu tukiangalia miaka mitano hii hakuna chocjote cha maana alichofanya hususani hapa ikungi, maji shida, barabara ndio usiseme alitushawishi kugoma kuchangia maabara sasa tunajuata shule za jimboni kwetu hazina maabara kama wenzetu leo tunajuata kwanini tulimsikikliza.
Pia mbunge wangu Lissu mbona umeshindwa kujibu hoja ya matumizi mabovu ya mfuko wa jimbo ambayo yalitolewa na mbunge mwenzio tena wa huku huku singida kuwa unatafuna bila huruma mfuko wa jimbo.
Mwisho kabisa tunasikitika kuwa na mbunge wa aina ya Lissu ambayo miaka mitano imepita hakuna cha maana kilichofanyika huku jiomboni kwake amekuwa mbunge wa malumbano badala kutuletea maendelea wananchi waje lakini siyo mbaya kwa kuwa mbio za sakafuni huishia ukingoni nawe umefika ukingoni tutakutana october