Mhe. Bashe tengua kauli...

Sidhani kama unajua unachokiongea. Mimi nilipata dv 2 form iv na form vi lakini ni mwalimu. Isitoshe walimu wengi wa sekondari ni wale wenye div I-III.
 
Kila mtu siku hizi anakosoa walimu hata kama hajui vigezo na majukumu ya mwalimu kwa ufasaha. Wengi wanadhani ile mtoto kufaulu nikujibu maswali kama nwalimu alivyo jibu. Wanajisahaulisha kuwa binadamu anautashi hivyo yampasa kutafakari. Nimeshuhudia vyuoni watu wakifanya discussions katika vikundi lakini ikitokea swali likatoka lenye mlengo unaoelekea kufanana na waliyojadili kuna watakao kosa kabisa kwakuandika kila kitu kama walivyojadiliana na kuna wengine watakao jiongeza nakugundua mlengo wa swali na watalipata. Ufahamu ni jambo ambalo kila mtu anakiwango tofauti na ni nadra sana mtu kufundishwa ufahamu. Ninachokiona kiona nikuwatwisha mzigo walimu usiokuwa wao,jamii isiyotayali kupokea na kujifunza hatimae kubuni njia zake kwakusaidiwa na nyenzo tofauti kama mwalimu, vitabu na mazingira halisi ya nje huyo hafai. Matokeo ya wanafunzi sio kama mgonjwa anae enda kutibiwa na kufanikiwa kwa dactari ni pale nafuu inapopatikana tena ndani ya mda mfupi.
Naamini kama vyuoni wanafunzi mitihani yao ingetungwa na chombo kingine nje ya yule aliyefundisha nakusahihiswa kwa mfumo huohuo,nakwambia pamoja na ukubwa wao,habari hii ya ufaulu vyuoni ingekuwa habari nyingine na uwepo wa ma PhD,na professors. 75% ufaulu unamtegemea mhusika ( mwanafunzi ) mwenyewe.
 
Sidhani kama unajua unachokiongea. Mimi nilipata dv 2 form iv
Kwa nini hukwenda form five? Mwaka gani na shule gani? Kama kuna wengine kama wewe wana sababu au wewe una sababu zako unazozijua wewe na ni WACHACHE- NEGLIGIBLE!
 
Nimesoma robo tu ya andiko lako, lakini nikajua kwa haraka haraka unaona dosari ya hoja za Mh Bashe. Kutoka moyoni, BASHE yuko SAHIHI. nampongeza kwa kujipambanua kuwa msema ukweli. Sina hakika chama kama kitamuona ni mbaya au la,lakini hoja zake ziko Kizalendo!
 
CCM watamfukuza! Hawataki ukweli
 
kwa hiyo walimu wenu walikuwa na ufaulu gani mkuu? walikuwa na division one tu?
 
Kwa nini hukwenda form five? Mwaka gani na shule gani? Kama kuna wengine kama wewe wana sababu au wewe una sababu zako unazozijua wewe na ni WACHACHE- NEGLIGIBLE!
mkuu usikariri vibaya. sio kila mwenye division one lazima aende form five. amka.
 
nn Einstein na billgate,?
Usilinganishe hao na Tanzania situation. Einstein alikataliwa kuwa lecturer kwa vile hakuwa na vigezo walivyokuwa wanavihitaji pale-passes, sio kuwa alikuwa na div 4 or zero! Hatujui Billgates background yake kwa nini alifeli! Kuna wanafunzi wana akili lakini hawasomi. Tulikuwa naye alikuwa na akili sana form 4 akafeli zero kabisa. Baba yake alikuwa afisa elimu Mtwara, akarudia form3 akapata div 1 form 4&6. Akasoma medicine Muhimbili with flying colours. Akaenda Zimbabwe etc... He is dead now-RIP.
 
Nadhani huyo ni mwalimu anajitetea. Kuna mzazi anaweza kukubali mtoto wake Na div one aende ualimu baadala ya kwenda fomu faivu
Anakosea, huwezi kuukana ukweli, kuna waalimu wangapi wa div one?
 
hii tabia ya kila mtu kuujua na kuukosoa uwalimu ni tatizo. kiujumla lengo la bashe lilikuwa jema ila kwenye kuwasilisha hoja yake imejaa ukakasi na imejaa udhalilishaji. kusema walimu ni chaka la watu waliofeli kiujumla sio sawa. je fani zingine huchukua watu wenye sifa zipi? je vipi polis? vipi uganga? hoja ya bashe imedhalilisha walimu kiukweli.
 
Kila secta inawatu wenye ufaulu tofauti,lakini naami kama ulipata certificate ina maana uli pasi. Swala sasa lingebaki ni grade ipi ya ufaulu inafaa kada ipi na kwanini? Je nikosa la nani kama waliruhusiwa kusoma? Je nikwakiwango gani( statistical data) hiyo grade imechangia kwa matokeo hayo?
NB: mwalimu anaefundisha darasa lenye watoto 50, harafu 2 wakaenda shule wanazoziita special, 8 wakaenda za kawaida je hapo mwalimu unamhukuje?
 
Hili swala la ufaulu mbona linatambulika tangu kitambo? Waliopata division one na two O'level huchaguliwa kwenda form five, na waliopata division three kombi zikakubali pia huchaguliwa moja kwa moja na nacte. Wale ambao kombi hazijakubali lakini wana credit tatu yaani "C" tatu husoma shule za private. Siku hizi huenda kufanya mitihani ya mchujo kwa ajili ya kusoma shule za english medium na zingine za private. Hali ipo hivyo hivyo kwa "A" level ingawa huyu anaweza kuchagua kusomea ualimu kwa ngazi ya degree. Sasa huyo mwanafunzi mwenye ufaulu wa division one, two na three mnayemtaka akasomee ualimu atapatikana wapi? Mbona mnataka kuficha ukweli ambao unafahamika tangu kitambo? Ni mfumo wa serikali ambao imejiwekea tangu siku nyingi. Hawa wenye division four ndiyo huenda kusomea ualimu na fani zingine kwa sababu hawakuchaguliwa kuendelea na shule moja kwa moja. Ngoja niishie hapa lakini walimu wengi ni wale wenye ufaulu wa division four ya point 28

Mshua.
 

Ndugu; ukiwa huna data nivizuri ukakaa kimya! One , two kwa uwalimu zimejaa . Nyie mnaonyooshea walimu vidole kwa nini mlipofaulu na hizo one za 7 na 3 hamkwenda uwalimu Kama mnaupenda sana kuukosoa?
 
ila waliofeli ndio waliokufanya ukajua kuandika kueni makini kwakile mnachotamka mcjemkapata laana bure
 
Ndugu; ukiwa huna data nivizuri ukakaa kimya! One , two kwa uwalimu zimejaa . Nyie mnaonyooshea walimu vidole kwa nini mlipofaulu na hizo one za 7 na 3 hamkwenda uwalimu Kama mnaupenda sana kuukosoa?
Soma kuna sabau kwa nini mtu wa div 1&2 anakwenda ualimu. Soma watu wametoa sabubu kwenye uzi huu! All in all ni wachache na wana sababu zao.
 
Ni ukweli ni sawa mtu akisema wabunge ni watu waliofeli au mafisadi au wala rushwa akilenga Sijui kubadili mfumo sidhani kama watamuelewa au utakuwa amewatendea haki.! Maana humo kuna watu makini pia kwa hiyo bora uende kwenye hoja kuliko kushambulia watu kwanza.
 
mkuu usikariri vibaya. sio kila mwenye division one lazima aende form five. amka.
Anakwenda wapi? Labda clinical officer very rare kwenye ualimu. Kuna ambao na mimi tunatoka kwenye familia masikini tunataka kusaidia familia, ni wachache!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…