Mhariri Tanzania daima kanunuliwa?

ukisoma mtanzania ya leo utashangaa sana, inamshambulian dr mwakyembe na kumuwekea maneneo mdomoni, hali wakijua kuwa hata slaa ambaye nikatibu mkuu wa chadema alishasema kuwa mwakyembe hana maslahi na wala halazimiki kutangaza maslahi ambayo hana

Gazeti la RAI lilianza hivihivi,Je Mbowe umeuza gazeti na tuhamie magazeti mengine?
 
Mlalahoi, kwanini tunaconclude kuwa kanunuliwa? why cant we say that he has a different opinion from the "majority"? I for one, do not believe anything Mwakyembe says in this saga especially after it was revealed that he is also fighting to enrich himself in the power generating business. Absalom anaweza kuwa naye amegundua hadaa ya Sitta na Mwakyembe na kwa kung'amua kuwa hawa watu hawana nia njema basi akaamua kusema aichosema.

Hivi tunataka tuseme kuwa TANESCO hawana utaalamu wa kugundua mitambo mizuri na mibovu? Kama wao wameona kuwa mitambo ya Dowans ni suruhisho la muda la matatizo ya umeme, kwanini sisi ambao hatuna utaalamu wowote katika eneo hilo tunasema kuwa wamenunuliwa!! Mwakyembe na Sitta ni wanasheria! Shelukindo hana utaalamu wowote wa umeme na hawajasema ni wapi wametoa hiyo thesis kuwa mitambo ya DOWANS haiwezi kuzalisha umeme tunaohitaji kwa muda huu. Na tusisahau kuwa mitambo ya DOWANS ingenunuliwa ingekuwa kwa ajili ya "emergencies" na sasa giza tumeanza kuliona.

Bwana Jobo, mtu anaweza kununuliwa au kuwa na different opinion lakini thats not a big issue here. Mkuu unaonekana upo biased kwa kuwa unaipenda opinion ya kununua mitambo. lakini lazima ukubaliane na nguvu ya pesa kuwa inaweza kutu twist katika mwelekeo wowote tu.
TANESCO wanunue mitambo mipya hata kwa mkopo, kama walivyonunua ile iliyojengwa na watsila pale jirani. wanaweza.
umesema TANESCO wanautaalamu wa kugundua mitambo? toka lini? hawa TANESCO unaowaongelea wamechangia kiasi kikubwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa hivi, ya ununuzi wa vitu vibovu mf. nyaya, transformer nk. Wangekuwa na akili hiyo na ya kuweza ku project mahitaji ya umeme, suala la umeme lingekuwa historia. we cannot trust this people any more. mtazamo wao umekuwa mara nyingi ni wa ubinafsi. Mungu ibariki Tanzania.
 
Gazeti la RAI lilianza hivihivi,Je Mbowe umeuza gazeti na tuhamie magazeti mengine?

Du mkuu unafuata content au unamfuata Mbowe? Ni udhaifu wa wa Tanzania kuwa washabiki wa watu badala ya issues ndio maana katika sakata hili la Dowans vifuata upepo wengi wamechanganyikiwa sana. Chamsingi tuangalie issues jamani kama hazitufai tuachane nazo kama zinatufaa tuzichukue na si kufuata upepo mara Mbowe mara Mwakyembe mara Rostam mara yule kwani hawa ni binadamu na huwezi kutabiri kesho watachukua msimamo gani. Cha msingi watu waache uvivu wa kufikiri na kuchambua mambo badala yake wahoji kila kitu bila kujali ni nani anaye kisema.
p.s nasoma magazeti yote bila kujali ni nani mmiliki ila nachambua hoja na kubaki na msimamo wangu mwenyewe so awe kauzwa au kanunuliwa si biashara yangu ila anachokiandika ndio biashara yangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom