Katika hali ya wahadhiri vyuo vikuu kuendelea kuwatumia wanachuo kama sehemu ya kutimizia haja zao na kuonyesha umaarufu wao,sasa umeingia sura mpya baada ya Mwalimu mmoja(jina tunalo)wiki iliyopita kujipambanua kama member wa Royal families na kuwadharau Wahadhiri wenzake kuwa wanawafundisha ujinga wanafunzi huku akijisahau na kumtaja hata mkuu wake wa kitengo ambaye wanachuo hao wanamheshimu kwa ufundishaji uliotukuka.Haikuishia hapo,aliendelea ku kuwadharau wanafunzi wanaosoma kozi tatu za Utawala wa umma,siasa na uhusiano wa kimataifa kuwa hawana pa kwenda kwa kuwa wamekuwa wakijidai kuwa wanajua kujenga hoja.Mhadhiri huyu aliendelea kuwaeleza wanazuoni hao kuwa anawachukia mno na ana mtazamo hasi dhidi yao,hakuishia hapo akaendelea kuwaeleza kuwa watafeli mno watake wasitake huku akiwapa matokeo ya test zao na kuwapiga 0 karibia darasa zima.Wakadhani kamaliza,akaendelea kuwaeleza kuwa walijiunga chuo wakiwa wachanga(huku zaidi ya nusu ya darasa wakiwa wanamzidi umri).Baada ya mhadhara huo,wanazuoni hao hawakuridhika na hoja hizo na inasemekana wameanza taratibu za kulishughulikia suala hilo na wengi wamejipanga kumkataa hata kama management itashinikiza kuendelea naye.