Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Mh. Zitto mnamo 27th November 2010 15:10 ulituandikia haya:
Nina nia njema ya kujua maendeleo na mafanikio ya jitihada zako kwa mwaka 2011 kwenye Rural Growth, Gas and Petroleum sub-sectors and Leadership Ethics.
Zitto
Mwaka 2010 - 2011 nimeamua kujikita kwenye Rural Growth, Gas and Petroleum sub-sectors and Leadership Ethics. Rural growth kwa ajili ya kusukuma nguvu katika cutting poverty levels vijijini. Bado ukuaji wa uchumi wa Taifa letu haufiki chini na hivyo hauendani kabisa na kupungua kwa umasikini. Ajenda hii imesahaulika sana sana. Baada ya kupata sheria mpya ya madini (bado ina mapungufu kidogo), napeleka nguvu kwenye kuhakikisha kuwa Gesi Asilia na Mafuta yanafaidisha nchi yetu. Lengo ni kusukuma kuwe na Sheria mpya ya Gesi na Mafuta ili kuepuka yaliyotukuta kwenye sekta ya Madini.
Nina muswada wa sheria nilioandika ili kubadili sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Serikali kukataa kuuchapisha. Ninadhamiria kuhakikisha kuwa muswada ninaurudisha Bungeni. Lengo ni kutenganisha Biashara na siasa kwa kuanzisha blind trusts. Pia lengo ni kufanya sheria ya maadili iwe effective na wananchi wawe na uhuru zaidi wa kukagua mali za viongozi wao.
Mambo mengine ni masuala ya chama mfano suala la Katiba mpya nk.
Nina nia njema ya kujua maendeleo na mafanikio ya jitihada zako kwa mwaka 2011 kwenye Rural Growth, Gas and Petroleum sub-sectors and Leadership Ethics.