Mh. Sugu: Rais wa Mbeya...?

Chipolopolo

JF-Expert Member
Feb 14, 2012
1,425
725
Mahali ni pale pale. Msafara uleule. Spidi ile ile ya mbio za mwenge. Wakati msafara wa Makamu wa Rais Dk. Mohammed Bilal ukipita eneo la Kabwe- Mwanjelwa Mbeya kuelekea mashariki ya jiji hili lenye changamoto kadhaa za kisiasa, baada ya muda mfupi msafara ukiwa umetokomea, zilisikika kelele za shangwe eneo hilo la Kabwe.

Gari likitembea kwa mwendo wa polepole huku likiwa linasindikizwa na kundi kubwa na vijana wakishangilia.Ndipo ilibainika kuwa aliyekuwa amezingirwa na kusababisha msururu wa magari kuwa mkubwa ni Mh. Joseph Mbilinyi aka Sugu.

Akiwa amevalia mawani ya makubwa ya jua, na kombati la CDM, alitumia dakika kadhaa kuwasalimia wananchi akiwa ndani ya gari kisha kuwaomba wamruhusu aendelee na safari. Akaruhusiwa kisha akaondoka.

Haikufahamika mara moja kwanini hakuambatana na ule msafara wa mbio za mwenge?
 
Huyu si yule RUGE B? kama huyu ndio Rais wa Mbeya, I can imagine watu wa Mbeya uwezo wao wa kufikiri ukoje!
 
Huyu si yule RUGE B? kama huyu ndio Rais wa Mbeya, I can imagine watu wa Mbeya uwezo wao wa kufikiri ukoje!

Mkuu siasa ni mchezo wa bahati nasibu pia. Watu wakichoka hatawakiwekewa kivuli na mtu, wanaweza kupigia kura kivuli ili kuonyesha kutoridhika kwao na yule aliyekuwepo. Watu wa Mbeya wanafikiri vizuri tu.Wanamaamuzi.
 
Kiongozi:Cha maana wamemaliza beef lao salama. Wasongembele.Nchi ni yetu sote.Tuijenge pamoja.
Mkuu Chipolopolo, heshima kwako; kimsingi mimi sikukerwa na muafaka wa SUGU na RUGE. Beef sio issue wala nini, na hata katika dini watu wanatakiwa wapatane. Kinachonikera, ni kuwa kuna unafiki, kwa nini mwafaka huu, ingawa una kila aina ya mlungula watu waunge mkono, wakati ule wa Wanzanzibar, ambao ulipoteza maisha ya watu wengi, waubeze? Huu ni Unafiki na Uzandiki!
 
Mkuu Chipolopolo, heshima kwako; kimsingi mimi sikukerwa na muafaka wa SUGU na RUGE. Beef sio issue wala nini, na hata katika dini watu wanatakiwa wapatane. Kinachonikera, ni kuwa kuna unafiki, kwa nini mwafaka huu, ingawa una kila aina ya mlungula watu waunge mkono, wakati ule wa Wanzanzibar, ambao ulipoteza maisha ya watu wengi, waubeze? Huu ni Unafiki na Uzandiki!

Mkuu PZion:Nmekusikia.Umechambua vizuri. Umeamsha hoja yenye changamoto nzuri:kwa kulinganisha muafa wa Sugu Ruge na ule wa CUF vs CCM Zanzibar!
 
Mkuu Chipolopolo, heshima kwako; kimsingi mimi sikukerwa na muafaka wa SUGU na RUGE. Beef sio issue wala nini, na hata katika dini watu wanatakiwa wapatane. Kinachonikera, ni kuwa kuna unafiki, kwa nini mwafaka huu, ingawa una kila aina ya mlungula watu waunge mkono, wakati ule wa Wanzanzibar, ambao ulipoteza maisha ya watu wengi, waubeze? Huu ni Unafiki na Uzandiki!
Usikubali kwenye open forum kama hizi kichwa chako kionekane debe tupu, hakuna asiyependa muafaka lakini tatizo linakuja je muhafaka huo unaendana na kile ulichokuwa unakipigania? Seif Sharif Hamad huwezi kumfananisha na Raila Odinga wa Kenya, muhafaka wa kenye ni realy power sharing, lakini sio muafaka wa Zanzibar yule Maalim hana maamuzi yoyote ni sawa na karani tu.

Back to Sugu, wao na Ruge + Clouds Fm wana mambo yao ya kiburudani na hayahusiani na siasa, kama wamepatana wao muafaka wao sio wa Kitaifa ni kikundi tu flani kwa maslahi yao na si maslahi ya Taifa.
Utakuwa ni mzembe wa mwisho na mvivu wa kufikiri kutaka kufananisha issue ya Burudani na issue ya siasa. nitakushangaa sana.
 
Back
Top Bottom