Vipi kuhusu Hawa Askari ambao wanaotuhumiwa kila siku kuua raia ?
Vipi kuhusu hao raia ambao wamekuwa wakifa wakiwa mikononi mwa Jeshi la Polisi katika Vituo vya Polisi ?? Nao hawamhusu?
Vipi hao mateka ambao baadhi yao wameokotwa wakiwa tayari wameuawa kinyama? Nao hawamhusu??
Akumbuke kwamba yeye binafsi akiwa Kama Mkuu wa nchi hii kwa mikono yake ndiye aliyewateua hao Viongozi wote wa Serikali hii iliyopo, wakiwamo na Wakuu wa Majeshi ambayo wa-Tanzania wanayatuhumu kwamba yamekuwa yakihusika katika kuwateka raia na kisha kuwaua. Matendo yote yanayofanywa na hao Watu Wateule wake ni sawa sawa kabisa kwamba ameyafanya yeye mwenyewe Mteuaji binafsi. Kushindwa kwa hao Watu ambao amewateua ndio kushindwa kwake yeye Mteuaji. Kwa hiyo kwa namna yoyote ile kamwe hawezi akajitenga na matendo mazuri au mabaya yanayofanywa na Wateule wake.
Aidha, hata tuhuma anazotupiwa za kuhusika na tukio la jaribio la mauaji ya Tundu Lissu kule Dodoma yeye pia tuhuma hizo zinamhusu Moja kwa Moja. Rais Magufuli siyo Mtuhumiwa pekee wa shambulizi lililofanywa dhidi ya Tundu Lissu, hata yeye pia anahusika kwa sababu Serikali ya 'MaguSami' (i.e. Magufuli+Samia) ndio iliyokuwa madarakani wakati ule tukio hilo lilipotokea.
Jana tarehe 28.9.2024 pale mkoani Ruvuma mh. Rais amesema yeye hajawahi kuua mtu labda sisimizi. Nimefurahi mno kusikia hivyo na imekua bora zaidi umekataa ukatili na unyama huo kwa kinywa chako. Hongera sana mama
Tatizo litakapokuja ni wale uliowaambia wajibu wala wasiogope.
Unawaambiaje wengine wajibu wakati wanaolalamika wanakatazwa kulalamika? Kama kweli unamaanisha kwamba watu wako wakusemee na wale wanaozuiya waambie wasiogope wawaachie walalamike. Hapo utakua ume balance mizania
Kwamaana nyingine turejee ule wimbo ...........waacha waandaneee.... ........ mbele kwa mbele
NB: Mimi siomwanachama wa chama chochote cha siasa
Kweli kabisa hajawahi kuua mtu labda Sisimizi .
Lakini pia hajawahi kujenga Daraja,barabara , bwawa la umeme katika eneo lolote la Tanganyika yeye kama Samia .
Cha ajabu kila barabara tunaambiwa kuwa amejenga yeye , madaraja amejenga yeye, mashule amejenga yeye. Mishahara ameongeza yeye . ,Hajawahi kukanusha hahusiki kujenga barabara yoyote wala Daraja kokote labda njia huko nyumbani kwake Kizimkazi.
Kama barabara zinajengwa kwa kodi za watu halafu anasema kuwa amejenga yeye iweje asilaumiwe zisipojengwa . Kama mauaji yakikomeshwa anaambiwa amekomesha mauaji basi hata yakitokea kwa sababu ya uzembe wa wateule wake na yeye kukaa kimya na kuwaacha kama vile hii nchi haina watu wengine wenye uwezo zaidi basi ni wazi kuwa yeye ndiye mfadhili mkuu wa Firing squard kama watawala wengine madikteta waliowahi kutokea duniani.
Kujitenga na wauaji ni kuwatoa walioshindwa kukomesha mauaji kwani wanalifanyia drama.
Mtu anajitokeza kwenye vyombo vya habari vikubwa akiwa na viongozi wa CCM anasema kuwa alikua anateka watu kwa maelekezo ya Mbowe lakini hakamatwi kwa jinai aliyoifanya na kumuunganisha na Mbowe aliyemtaja ili athibitishe kuhusika kwa Mbowe . Drama inaisha kwa CCM na polisi kushangilia kuwa Chadema imepata kiboko yake wa kuubomoa.
Huu ujinga unafumbiwa macho na Amiri jeshi mkuu. Yaani mtu anateka watu anaua wetu akiwa Chadema halafu akirudi CCM basi makosa yake ya jinai yanakuwa ni manukato machoni mwa watawala.
Huu ndio uhalalishaji na uhusika na udhamini wa mauji.
Yanga ikifanya vizuri kocha anasifiwa ,ikifanya vibaya analaumiwa na hata kufukuzwa