Mh. Rais Samia, Wakazi wa Ukonga tumeikosea nini Serikali?

kimaus

JF-Expert Member
May 10, 2011
565
652
Mh. Samia, jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam kwa maoni yangu ndio jimbo lenye barabara mbovu kuliko jimbo lolote. Barabara zetu zote ni mbovu yaani ni kama tumesahaulika au tumeikosea Serikali. Barabara ya kutoka Banana kwenda Kivule hadi Msongola ni mahandaki. Kitunda mwanagati ni mahandaki. Ukonga Mombasa to kivule ni Mahandaki.Kitunda, Nyantila mpaka Buza ni mahandaki.
Huku kivule Serikali imejenga hospitali ya Wilaya, lakini kiukweli ni kama haifikiki, maana barabara ni mbovu mno. Hapo awali wakati wa Mwendazake tuliadhibiwa kwa kuwa wawakilishi wetu walitoka upinzani, lkn sasa hv viongozi wetu ni wa chama tawala.
Ukonga tumekosea wapi???
 
.,...hapo kabla mliadhibiwa kisa kuna mbunge kutoka upinzani!mbunge huyu wa upinzani alitokea Sudan au ni mtanzania?,middle class wa nchi hii wanashangaza,why mkuu usifanye push back ili uletewe barabara bora?lingusenguse huku toka uhuru ,mbunge ni wa ccm na hatujawahi hata mara moja kutembelewa na top 3 ya viongozi wetu, ila kuna watanzania huku wana push back kujiletea maendeleo
 
Unaweza ku push kujiletea maendeleo kaka lkn sio kujenga barabara ya lami. Mfano watu wamejenga culverts maeneo mengi tu, lkn linapokuja suala la barabara ya kiwango cha lami, si suala la wananchi.
Pia, nakubaliana na wewe hata mbunge wa upinzani ni mtanzania, lkn siasa za kiafrika unazijua. Nakumbuka kuna wakati wanasiasa walishawahi kunukuliwa wakiwaambia wananchi kuwa mnachagua upinzani, miradi ya maendeleo mtaisikia tu.
 
Huko majohe nilipita siku moja barabara mbaya kuliko zote dar makorongo mahandaki kama yale ya kujifunzia jkt
 
Mh. Samia, jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam kwa maoni yangu ndio jimbo lenye barabara mbovu kuliko jimbo lolote. Barabara zetu zote ni mbovu yaani ni kama tumesahaulika au tumeikosea Serikali. Barabara ya kutoka Banana kwenda Kivule hadi Msongola ni mahandaki. Kitunda mwanagati ni mahandaki. Ukonga Mombasa to kivule ni Mahandaki.Kitunda, Nyantila mpaka Buza ni mahandaki.
Huku kivule Serikali imejenga hospitali ya Wilaya, lakini kiukweli ni kama haifikiki, maana barabara ni mbovu mno. Hapo awali wakati wa Mwendazake tuliadhibiwa kwa kuwa wawakilishi wetu walitoka upinzani, lkn sasa hv viongozi wetu ni wa chama tawala.
Ukonga tumekosea wapi???
Poleni.Lkn si mna Mbunge wenu?,Vipi mmeshamueleza Mbunge wenu Kuhusu kero hiyo?.
 
Huko majohe nilipita siku moja barabara mbaya kuliko zote dar makorongo mahandaki kama yale ya kujifunzia jkt
We acha tu. Sielewi Jerry Slaa anafanya nini bungeni. Dar es Salaam lkn kama vile tupo Kintinku!!
 
Kutoka Mombasa hapo kwenda Bomba mbili, Njia nne mpaka kwa mhaya ni zaidi ya mahandaki.
 
Mh.Rais tunakuomba utufanyie jambo la barabara hata vifusi zipitike, kitunda -Magore-mwanagati, bombambili, na kivule msongola, hali ni mbaya sana, nauli juu, vyombo vya usafiri wa umma vimepungua kutokana na barabara, hali ni mbaya, tunakuomba hata umtume W/Mkuu afanye ziara ya kushtukiza ili ajionee hali.
 
Jimbo la Makongoro Mahanga wakati huo akiwa Waziri wa Ujenzi alipush barabara ya Banana Kitunda Relini.
Kwa sasa yupo Jerry Slaa yupo bizze kutafuta maokoto ya wajumbe ili arejee tena mjengoni hana time na Wapiga kura.
 
Back
Top Bottom