mcfm40
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,452
- 3,152
Kwa muda sasa serikali imekuwa haiachii pesa iingie kwenye mzunguko kwa kigezo cha kubana matumizi. Pesa inakusanywa lakini hairudishwi mitaani ili mzunguko uendelee na uchumi ukue.
Serikali imebana sana au kuondoa kabisa matumizi ya fedha kama katika kutoa tenda mbali mbali, kukodi kumbi za mikutano na makongamano, n.k. Kwa ujumla serikali imeishikilia pesa.
Matokeo yake sisi watu masikini ndio tunaumia. Vibiashara vyetu vidogovidogo vimekosa mnunuzi, bia bar haziuki, n.k.
Kubana pesa na kwenda kuzinunulia ndege, au kujengea mabarabara sawa, lakini impact yake kwa sisi masikini ni ndogo. Kuhamia dodoma sawa, lakini impact yake kwa sisi masikini, machinga na mama ntilie ni ndogo.
Mh ebu achia pesa iingie kwenye mzunguko kama kawaida cha msingi tu matumizi sahihi yazingatiwe! Kuna tetesi kutoka Hazina kwamba umeamua kushikilia pesa kwa hofu eti ukiyoa mafungu kama budget ilivyopitisha zitaliwa na wafanyakazi hewa n.k! Inasemekana unalipa tu mishahara na kugharimia mahitaji ya lazima ya wizara, hela nyingine yote unaizuia.
Hebu pia kaa na wachumi wako mjaribu kutatua hii hali hii mapema. Wananchi watashindwa uvumilivu.
Hii hali ikiendelea usishangse watu wakaamua kuingia mitaani bila hata kuchochewa kulalamikia ugumu wa maisha. Haiwezeksni kila unayeongea naye analalamikia ugumu wa maisha.
Mh achia hayo matrilioni yaingie mitaani. Halafu baadaye utayakusanya tena yarudi serikalini. Ndivyo uchumi wa nchi maskini unavyoendeshwa. Hali ni mbaya huku mitaani, haviuziki, havinunuliki! Tutafika kweli? Unatuumiiza sisi maskini mheshimiwa.
Kama kuna kitu kitafanikisha UKUTA kwa kiasi kikubwa ni hili la ukata na ugumu wa maisha, ambalo wengi wanasema wewe ndio umesababisha, na wala sio hili la kuminya demokrasia! La kuminya demokrasia nalo ni kubwa lakini kwa sasa watu wengi wana hasira kwasababu ya ukata unaoaminika umesababishwa na sera zako za kukurupuka.
Serikali imebana sana au kuondoa kabisa matumizi ya fedha kama katika kutoa tenda mbali mbali, kukodi kumbi za mikutano na makongamano, n.k. Kwa ujumla serikali imeishikilia pesa.
Matokeo yake sisi watu masikini ndio tunaumia. Vibiashara vyetu vidogovidogo vimekosa mnunuzi, bia bar haziuki, n.k.
Kubana pesa na kwenda kuzinunulia ndege, au kujengea mabarabara sawa, lakini impact yake kwa sisi masikini ni ndogo. Kuhamia dodoma sawa, lakini impact yake kwa sisi masikini, machinga na mama ntilie ni ndogo.
Mh ebu achia pesa iingie kwenye mzunguko kama kawaida cha msingi tu matumizi sahihi yazingatiwe! Kuna tetesi kutoka Hazina kwamba umeamua kushikilia pesa kwa hofu eti ukiyoa mafungu kama budget ilivyopitisha zitaliwa na wafanyakazi hewa n.k! Inasemekana unalipa tu mishahara na kugharimia mahitaji ya lazima ya wizara, hela nyingine yote unaizuia.
Hebu pia kaa na wachumi wako mjaribu kutatua hii hali hii mapema. Wananchi watashindwa uvumilivu.
Hii hali ikiendelea usishangse watu wakaamua kuingia mitaani bila hata kuchochewa kulalamikia ugumu wa maisha. Haiwezeksni kila unayeongea naye analalamikia ugumu wa maisha.
Mh achia hayo matrilioni yaingie mitaani. Halafu baadaye utayakusanya tena yarudi serikalini. Ndivyo uchumi wa nchi maskini unavyoendeshwa. Hali ni mbaya huku mitaani, haviuziki, havinunuliki! Tutafika kweli? Unatuumiiza sisi maskini mheshimiwa.
Kama kuna kitu kitafanikisha UKUTA kwa kiasi kikubwa ni hili la ukata na ugumu wa maisha, ambalo wengi wanasema wewe ndio umesababisha, na wala sio hili la kuminya demokrasia! La kuminya demokrasia nalo ni kubwa lakini kwa sasa watu wengi wana hasira kwasababu ya ukata unaoaminika umesababishwa na sera zako za kukurupuka.