Mh. Pinda Awasihi UKAWA!!

Mh. Pinda Awasihi UKAWA!!

Kinachonisangaza ni kauli za viongozi wa ccm. Wakiwa Zanzibar walisema NAPE alisema UKAWA wasirudi maana ndio wanachafua bunge. Juzi wanasema Kamati kuu imesema haitawomba UKAWA kurudi wala kukaa meza moja,leo mzee wangu "chonde chonde" anawataka wakakae meza moja wazungumze. Hizi kauli zenye utata toka kwa viongozi wa chama kimoja,Serikali moja lkn kauli tofauti tuwaeleweje?
 
Sio rahisi CCM tunayoijua sisi ikae meza moja na ukawa,kama tayari wana 2/3 ya wajumbe wa kuweza kuendelea na kutunga katiba wy should they give a dam???haujamuelewa PINDA wewe

Mkuu hiyo 2/3 wameipata wapi? Naomba kueleweshwa tu?

Tiba
 
Maneno ya Viongozi wetu yana utata kibao. Mkuu wa nchi alisema muda wa kwenda kwa Wananchi haujafika mpaka wakati wa kura ya maoni. Wengine wanasema Ukawa wanakopita hata sisi tutakwenda ili kupangua hayo waliyosema kwa wananchi. Kama Ukawa wanakwenda kuwalaghai wananchi, na wao wanafuata nini ikiwa wakati wa kwenda kwao haujafika. Waziri Mkuu anawasihi Ukawa wakae meza moja waondoe tofauti zao ili warejee Bungeni, waziri mwingine alisema Ukawa waliondoka Bungeni pasipo sababu na wakipenda warudi bila sababu. Hizi kauli zinatolewa na viongozi walioko kwenye chama kimoja cha siasa. WHO IS WHO AND WHICH IS WHICH?
 
Jamani eeh! Hiyo ni danganya toto. You know what time it is! It almost time for the 2014-2015 budget.

They know very well that donor countries will contribute squat if they keep doing what they do best, suppress people's opinions.

Ukawa should not trust these clowns or entertain them even for a second.
 
Ni miaka mingi, na ameweza kumudu dhoruba za zahama hii.
kwa utawala huu tulio nao ni wazi utaona miaka mingi..ajirangumu, mishahara mibovu, ufisadi kupamba moto, dhuluma, ujangiri wa kutisha,rushwa daraja A, na kila aina ya huzuni kwa mwananchi wa kawaida!!!:A S angry:
 
Sasa hii serikali ni ya ajabu, Wasira jana kanyanyuka na Ugombe wake kawaponda Ukawa sasa Pinda anakuja kuvyake. Hii serikali haina msemaji??

Serikali ni kama familia. Baba akiwa dhaifu, familia inakuwa ya ovyo. Kila mtoto anajiamulia anavyojisikia. Na kwa sababu baba ni dhaifu, usishangae kumuona anachekacheka tu!
 
UKAWA hawana sababu ya kurudi na kakaa meza moja na ccm,dhihaka na matusi waliyoyapata yanatosha wao kusonga mbele kutoa elimu kwa watanzania ili kuleta TAnzania mpya tuitakayo. Maana watakapo kubali kwenda kukaa nao ndipo watakapoanza maneno mapya ya kashfa,kejeli na kila hila.
Hakuna muda wa kupoteza sasa!
 
Ni mjinga tu asiye na akili kama Nape ndio wanaona wanaweza kuandika katiba bila UKAWA. Katiba ya nchi ni tofauti na kuchakachua kura walivyozoea. Pinda ana akili ndio maana anawaangukia UKAWA waketi meza moja. Shida ya pinda ni uchovu uliomwelemea lakini anajua kufikiri na kulia.
 
Wamuombe radhi warioba kwanza...hata kama serekali mbili zitapita lkn watoe tamko la kumuomba radhi warioba
 
Geresha hii. Mzee huyu wa Inyonga ni kama kinyonga. Ana ndimi mbili. Tunakumbuka sakata la Jairo, alisema angekuwa na mamlaka angemtimua palepale na kuwa JMK amepewa taarifa, ila mambo yalikuja isha kirejareja. Na hili UKAWA wasipokuwa makini na jinsi wanavyopakwa mafuta kwa mgongo wa chupa, ITAKULA KWAO! Mizengo anapindisha mambo wakati mwingine kimizengwe! Kama kweli yuko siriazi, iitishwe Kamati kuu ya CCM na watoe hilo tamko, pengine hapo tutawaamini!
 
Awasihi kukaa meza moja kuangalia ni namna gani watasuluhishana na kuondoa tofauti zao!!

Naamini sasa Serikali ya CCM imeona umuhimu wa UKAWA bungeni,.
Hakuna kukaa na ukawa meza moja walale mbele wasitusumbue kabisa tena huu siyo wakati wa kusumbuana na wehu kama ukawa.
 
CCM wamwombe kwanza Komba ajisalimishe akiwa na jeshi lake la Interahamwe alilolificha msitun.Ndipo wazungumze na UKAWA.
 
Back
Top Bottom