Fugwe
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 1,676
- 664
Usiwalaumu waKenya kwa uzembe na upuuzi wenu watanzania. This is free market era, kama hutimizi wajibu, kama hauko aggressive hakuna wa kukuonea huruma. Nyie endeleeni kutembeza mabakuli kwa wazungu badala ya kujenga uchumi na kuimarisha biashara na majirani zenu.
Tena Tz ikojitoa itakuwa imewasaidia sana majirani maana inawatesa mno, majirani zenu wanateseka sana kwa kututegemea sisi. Bandari dhaifu, reli hakuna na hivyo wanajikuta wakitumia gharama kubwa sana kufanya biashara pasipo na ulazima. Tunawasababishia bei kubwa za bidhaa kwa upuuzi wetu wa kushindwa kuwekeza kwenye reli na bandari. Hawaoni haja ya kuwa na jirani dhaifu, hakusaidii wakati wa raha, hakusaidii wakati wa shida. Kwa Rwanda, Burundi, Kongo, Zambia, Malawi wanaona Tanzania kama jirani dhaifu anayeshindwa kutumia fursa Mungu alizompa. Ukijitoa kwenye ushirikiano nao watashirikiana na nchi zingine na mambo yao yataenda. Timiza kwanza wajibu wako ndio uanze kulaumu majirani zako.
Hoja zako za mashiko lazima baadhi zimeegemea itikadi yako ambapo hatuko interested kujadili itikadi za watu fulani