Mh Lowassa sio Masiha ajaye

Mh Lowassa sio Masiha ajaye

Tutaona,kusoma na kusikia mengi sana kuelekea 2015! Ha ha ha haaa kwa hiyo mamvi sio yule ajaye?
 
Naungana na mtoa hoja na hoja yake pia. Watu humu hawaangalii amesema nini wanaanza kuelezea biblia; ni akili ndogo. Lowasa hafai kuwa kiongozi nje ya Monduli ambako nahisi watu wa huko anafanana nao.
LOWASA NI MWIZI MKUBWA. Naomba mumtafakari MEMBE
Membe big No labda tumtafakari Mangula maana hata CCM ilipo mtupa hata kwenye nafasi ya Udiwani alieendea kuwa mtiifu na Mwaminifu na baadaye walicyomrudisha walau Chama kina adabu.
 
Ndugu usiwe kama mjinga, ila uwe mwenye hekima na kuona mbali. Nitakujibu kwa mafumbo.
Hivi umekaa na mkeo miaka 30 ktk ndoa hv unaweza mpandisha mahakaman kwa mambo yanayohusu unyumba wenu?

Ndugu, ni Nia yangu kuendeleza mazungumzo haya kwa hoja. Na iwapo kunatofauti katika namna tunavyo yaona mambo hapa, ni Nia yangu kuleta mawazo yangu kwa hoja tu, na sivinginevyo.

Sasa kwakuanza,
kushindwa kumpeleka mahakamani kunatakiwa kuonyeshe udhaifu upande gani? Wake au wa serikali hii iliyojaa madhambi ya aibu??!

Je nikweli kuwa lowasa ndiye mchafu pekee ndani ya serikali hii dhalimu? Kiasi cha Kum identify yeye tu na kuchafua kwapamoja na kwa nguvu zote namna hii?

Je makosa aliyo fanya lowasa ( kama ni kweli amefanya) ndio makosa makubwa sana kuwahi kufanyika kiasi hata nafasi ya kujitetea mbele ya kamati ile wakaona anyimwe???

mimi nadhani, Akili ya mtu mwerevu kama vile unavyotaka wewe kujipambanua kwa watu hapa, ingetakiwa kujiuliza hapa hasa tatizo liko wapi???

Kwanini
1. Amehukumiwa tu bila kusikilizwa
2. Hajapelekwa mahakamani kama ushahidi wa wizi wake wanao
3. Anatukanwa na kuchafuliwa ilihali yeye amenyamaza, hajibu wala hajitetei

Halafu eti huyu mtu anaeitwa mwizi, mnyonyaji Bado awe na ujasiri wakutaka kuwatumikia watanzania katika nafasi ya uraisi,.

Nasihivyo tu, naapate uungwaji mkono wa maelfu ya watu wana CCM kwa wapinzani?

Jesikweli kuwa kunakitu hawa wanakifahamu???

Ndugu, udhalimu hua na mwisho wake!!

Na haki sikuzote hujitetea yenyewe Ukweli hauwezi kujificha milele,.

Nakuhakikishia wanajua walichomfanyia huyu bwana na wanaogopa sana kurudi kwake!

Sasa kama nikweli wewe si mjinga kama unqvyotaka tuamini, jiulize hayo jipatie majibu halafu jitahidi kuto zungumzia mambo usiyo ya jua kanakwamba unayaelewa sana!

Sasa nasema hivi, Kushindwa Kumpeleka mwizi mahakamani nakukaa kuzungumzia wizi wake majukwaani, kumuhukumu, bila kutoa nafasi ya yeye kusikilizwa si HAKI!!!!!

Kama lowasa (au mtu mwingine yeyote) niwakuhukumiwa basi ni LAZIMA ahukimiwe kwa HAKI!!!!!

Nashukuru,
 
Amakweli nime amini usemi wa Kiswahili umsemao ,?" Mti wenye matunda ndio upopolewao" ninamaana kwamba Lowasa ni sawa na mti wenye matunda mengi tena matamu ambao kila mpita njia hutamani kutupa jiwe lake ili apate japo tunda. Kinyume chake ni kwamba mti usio na matunda kamwe hauwezi kupata dhoruba au shurba ya kupopolewa mawe. Hivyo naamini kuwa hakuna Kiongozi yeyote hapa tz aliyepitia Wakati mgumu na wanye majaribu mengi kama mh lowasa, katika Imani yangu naamini kuwa ili kiongozi yeyote awe bora ktk uongozi wake lazima apitishwe ktk misukosuko mingi. Mh. Lowasa kaiva na kakomaa. Watanzania wenzangu tusche tabia za majungu, kamwe hatutoendelea kwa kuendekeza tabia za kupigana majungu.
 
Nimeandika hii habari baada yakuona watu wanampamba Lowasa kama masiha ajaye, mkomboz na mtetezi wa wanyonge wakimsahau Mh Lowasa kwa vitendo vyake vyakinyonyaji na ukandamizaji akitumia udhaifu na ujinga wa watanzania kujitwalia umaarufu. Tufike mahali tuseme No kwa Mh Lowasa. Watanzania tumechoka.

Wewe TumainiEl, majuzi tu ulipost hapa thread kama msamaria mwema usie na upande wowote kumshauri Lowassa aache mbio hizi za Urais!

Katika thread ile ulionekana kama mwanausalama hivi mwenye nia njema na Lowassa na ukamalizia kwa kusema umeamua kusema hayo kwasababu Lowassa ni mzee wako!!! Nilijua ww ni mtu mwema usie na upande wowote kisiasa na pengine hujatumwa bali ni msukumo na kwa utashi wako binafsi!

Leo sio tu unaonekana umetumwa na kundi la wanasiasa bali pia umejituma mwenyewe kwa chuki kumshambulia "mzee wako uliedai unampenda, Lowassa" na sasa unamwita Fisadi/mchafu!

Nani akuamini tena na ule ushauri wako juu ya usalama wa Lowassa? Maana ulikuja kama mtu mwema pengine wa usalama, ndani ya hiyohiyo post ukamtisha, katika kujibu hoja za wadau ukaendelea kutoa matisho, leo ni shutma, lawama, mara unaingiza maneno ya mungu mara kashfa!!

Hueleweki na huaminiki tena, umevurugwa kajipange!
 
Lowasa huyu wa visasi na fitina kama ccm hawamjui mumeru wa monduli wacha wampishe kwenye cc yao.atalipiza tu kwa nape,mangula na sita pamoja na membe mtaondoka tz ole wenu
 
Hakika mangula nape na kikwete wamedai edo kakiuka maadili ya ccm hafai
 
Taifa gani lowasa aweza kuwa masihi? Labda la mafisadi na wezi wamali za umma.ikiwa tz inasifa taja basi lowasa atakuwa
 
Membe big No labda tumtafakari Mangula maana hata CCM ilipo mtupa hata kwenye nafasi ya Udiwani alieendea kuwa mtiifu na Mwaminifu na baadaye walicyomrudisha walau Chama kina adabu.

Mh Membe tunasubiri muda ufike tuweke tiki uingie ikulu y Magogoni. Huwezi mlinganisha Membe na mzee wa richmond
 
Masiya au masihi hana sifa mbaya. Hapa jirani yetu kulikuwa na mtoto mwizi anaibia hadi mali za baba yake. Sasa inanikumbusha mbali tukiwa wadogo huko Arusha. Ulizieni vizuri mzee wa watu akilalamika. Mtoto nyakua nyakua.
 
Ndungu wana jf na watanzania wote kwa ujumla napenda kuwa ambia Mh Lowasa sio Masiha ajaye.

Sisi wakristo tunajifunza ktk neno la Mungu yakuwa "MUNGU ANAWASHUSHA WENYE VIBURI NAKUWAINUA WANYENYEKEVU AMA WALIOJISHUSHA"

Mh Lowasa hata kabla yakuanza safari yake yenye matumaini alisha jiaminisha kwa pesa,mali na ushawish alio nao lazima yeye ndie Rais ajaye yani Masihi, tena akamuona mwenzake kama hafanyi kitu ila yeye ndio anaweza akawa anawatisha watu serikalini huku akijuwa yeye sio msafi na wakati huo neno linasema toa kwanza boriti ndipo utoe kibanz ktk jicho la mwenzako. Mh Lowasa kwakuwa Mungu anawachukia wenye viburi, hakika hukumaliza uwaziri wako mkuu na sasa unataka kuuwaminisha umma wote wa watanzania ulijiuzulu kisiasa wakati ukijuwa kweli ulikamatwa pabaya.

Napenda kusema mh Lowasa Anapaswa kujuwa Mungu hapokei rushwa wala sadaka chafu na anasema kamwe Roho yake haitoshindana na mwanadam na wewe ni mwanadam hivyo kamwe huwezi shindana nae, imefika wakati nikwambie hufanani na Masiha yeyote amewahi tokea ktk dunia hii.
Kuna watu wanakuita Daudi.

Napenda kusema hawa ni watu wasio mjuwa Daudi kijana alie kuwa shupavu na jasiri na kama wewe ungekuwa Daudi dalili ya kwanza nikukaa msituni na kondoo wa baba yako ufuwatwe na manabii kukumwagia mafuta uwe mfalme wetu, kinyume chake wewe umenunua mafuta nakujitaidi kuwaonga manabii wakupake mafuta uwe mfalme.

Sikiliza nikwambie mh Lowasa nikweli watakumwagia ndoo nzima yamafuta, ila wewe hutokuwa masihi ajaye maana Bwana anasema hakuwa nao ktk ibada zao.

Mfalme Daud aliuogopa ufalme ila wewe unautaman asubuh,mchana na usiku jambo hl limekufanya kuwa mbal na Bwana kiasi wapigana vita vyako peke yako Bwana hayupo.

Itafakari njia unapita ikiwa kama upo njia sahihi kisha upite nakusonga mbele.

Asante.

Kwa vyovyote vile utakuwa unapumuliwa kisogoni,dalili zote za kuwa bwabwa unazo
 
Kamwe sitamwamini Kiongozi yeyote kutoka siCm ama Serikali ya csiem.

Kwanza wana nafasi ya kukaa katika vikao vya Chama chao na kumshauri RAISI na kama RAIS hataki, wanaweza kumshinikiza Raisi. Maana yake ni Kuwa CHama ndo kimeunda serikali.

hakuna kiongozi yeyote (hasa hawa mawaziri) wanao kaa na raisi katika Cabinet, aje agombee uraisi eti halafu alete miujiza, wapi wewe, hakuna kabisa. Huyu mtu alishindwa nini kutekeleza ilani ya chama chake kuwaletea maendeleo wananchi eti angojee uraisi....

Mtu yuko NEC ama Kamati kuu, anashindwa kumshauri raisi kuhusu kuwaletea maendeleo wananchi, kukemea mchwa na panya buku wanaotafuta rasilimali na kodi za wananchi, badala yake wanalumbana kwenye media kukimbilia uraisi, tuwaogope kama ukomaaa... Anangoja uraisi ndo aweze,,,!!! Nooo

Tatizo wananchi bado waoga na wengine bado elimu ya uraia haijawafikia. Kuna wananchi hawajui kuwa wanalipa kodi. Kumbuka kila ukinunua bidhaa, VAT umelipa... Kila ukipokea mshahara PAYEE imelipwa..... Kila ukinunua mafuta taa, VAT wamekula

Sasa serikali kuhudumia wananchi na kueleza pesa zimetumikaje, ni haki ya wananchi, maana ni pesa yao...
 
Mh Membe tunasubiri muda ufike tuweke tiki uingie ikulu y Magogoni. Huwezi mlinganisha Membe na mzee wa richmond
Ina maana hujui Richmond ilikuwa ya nani? EL alijiuzuru kunusuru nchi ndugu yangu, umeona kesi ya Richmond iliishia wapi? Si imeuzwa tena kwa mapesa mengi ajabu, na nani kanunua? Si ipendi CCM Lakini kati ya wote nadhani EL angali anafaa kuongoza nchi hii. Na kama ni CDM tunaye Wil Slaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom