mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,421
- 1,792
Ni siku chache zilizopita nimeona katika vyombo vya habari mh. January Makamba akilalamika na kutuhumu Jeshi la polisi kuwanyanyasa wananchi wasio na hatia. Alikuwa ameenda kuwapa pole wananchi wa Bumbuli tanga ambao walitendewa kama alivyoagiza PM wa Tanzania (Nasema mtapigwa tu, kwani serikali tumechoka) Ilikuwa ni katika mgogoror kati ya wananchi na mwekezaji katika kiwanda cha chai.
Na leo tena amekuja na hii mpya kuhusu Kodi mpya ya huduma za SIM CARDS:-
======================================================================================================
Dar es Salaam. Kuna kila dalili kwamba Serikali inajipanga kufuta kodi ya Sh1,000 kila mwezi kwa wamiliki wa laini za simu baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi, taasisi na baadhi ya kampuni za simu nchini.
Hiyo inatokana na kauli ya Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba aliyoitoa jana akisema kwamba wizara yake ilipinga tangu awali mpango huo kabla ya kupitishwa na kuwa sheria na kwamba anaamini itaondolewa. Kauli hiyo ya Makamba imekuja siku moja baada ya chama tawala, CCM, kukaririwa na vyombo vya habari kikiitaka Serikali kuangalia vyanzo vingine vya mapato badala ya tozo hiyo.
Akizungumza kwa simu jana Makamba alisema: Sikubaliani na hili suala na kupita kwake ilikuwa ni kuzidiwa nguvu. Lakini najua haliwezi likatekelezeka ni lazima litabadilishwa kwa kuangalia eneo lingine la kutoza kodi.
Alisema msimamo wa wizara yake katika suala hilo ni tofauti kwani imekuwa ikijitahidi kuhakikisha gharama za mawasiliano zinapungua... Wizara hatukubaliani na kodi hiyo. Nia yetu ni kupunguza gharama za kupiga simu kwa kuwa ni kitu kinachowezekana.
Nia yetu ni kushusha gharama iwe sifuri kabisa, kitu chochote kinachopandishwa bei sisi hatukubaliani nacho kwa kuwa ni kuwaumiza wananchi wetu hasa wa vijijini. Bidhaa ambayo inatakiwa kushuka ni mawasiliano hivyo lazima iwe hivyo.
Jana, Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa alisema kwamba Serikali inapokea maoni ya wadau mbalimbali ili kuona namna ya kufanya marekebisho ya tozo hiyo. Hata hivyo, alisema uamuzi wa kuanzisha tozo hiyo haukuwa wa Serikali bali ulipitishwa na kukubaliwa baada ya kujadiliana na Kamati ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge.
Hayo yalipendekezwa na Kamati ya Bunge siyo Serikali. Tena walipendekeza vyanzo 67 vya kodi likiwamo hilo la kadi za simu. Walipendekeza tukate Sh1,450 kwa mwezi, lakini sisi Serikali tukashusha hadi Sh1,000 yaani kila mwananchi akatwe Sh33.3 kwa siku na mapato yatakayopatikana yatakwenda kuboresha miradi ya maji, umeme vijijini na barabara, alisema Dk Mgimwa.
====================================================================================================
My take: Ni serikali ya CCM pamoja na Wabunge wa CCM ambao walipiga kelele na kuipitisha bajeti kandamizi. Wabunge wa CHADEMA siku ya kupitisha bajeti walikuwa ARUSHA.
Sasa Makamba ana nia gani kusema haya ikiwa na yeye ni kiongozi wa CCM na anajua issue yote??
Au anawadanganya wananchi wake ili wamuone kuwa anawatetea???
Ni PM wa serikali ya CCM aliyeruhusu wananchi kupigwa na POLISI kama walivyotendewa Bumbuli:-
Je, Makamba hajui kuwa askari POLISI wamepewa rungu na Mh. PM kupiga tu kwani serikali ya January Makamba wameshachoka???
TAFAKARI KAMA uNA AKILI TIMAMU UTAELEWA.....
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Na leo tena amekuja na hii mpya kuhusu Kodi mpya ya huduma za SIM CARDS:-
======================================================================================================
Dar es Salaam. Kuna kila dalili kwamba Serikali inajipanga kufuta kodi ya Sh1,000 kila mwezi kwa wamiliki wa laini za simu baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi, taasisi na baadhi ya kampuni za simu nchini.
Hiyo inatokana na kauli ya Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba aliyoitoa jana akisema kwamba wizara yake ilipinga tangu awali mpango huo kabla ya kupitishwa na kuwa sheria na kwamba anaamini itaondolewa. Kauli hiyo ya Makamba imekuja siku moja baada ya chama tawala, CCM, kukaririwa na vyombo vya habari kikiitaka Serikali kuangalia vyanzo vingine vya mapato badala ya tozo hiyo.
Akizungumza kwa simu jana Makamba alisema: Sikubaliani na hili suala na kupita kwake ilikuwa ni kuzidiwa nguvu. Lakini najua haliwezi likatekelezeka ni lazima litabadilishwa kwa kuangalia eneo lingine la kutoza kodi.
Alisema msimamo wa wizara yake katika suala hilo ni tofauti kwani imekuwa ikijitahidi kuhakikisha gharama za mawasiliano zinapungua... Wizara hatukubaliani na kodi hiyo. Nia yetu ni kupunguza gharama za kupiga simu kwa kuwa ni kitu kinachowezekana.
Nia yetu ni kushusha gharama iwe sifuri kabisa, kitu chochote kinachopandishwa bei sisi hatukubaliani nacho kwa kuwa ni kuwaumiza wananchi wetu hasa wa vijijini. Bidhaa ambayo inatakiwa kushuka ni mawasiliano hivyo lazima iwe hivyo.
Jana, Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa alisema kwamba Serikali inapokea maoni ya wadau mbalimbali ili kuona namna ya kufanya marekebisho ya tozo hiyo. Hata hivyo, alisema uamuzi wa kuanzisha tozo hiyo haukuwa wa Serikali bali ulipitishwa na kukubaliwa baada ya kujadiliana na Kamati ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge.
Hayo yalipendekezwa na Kamati ya Bunge siyo Serikali. Tena walipendekeza vyanzo 67 vya kodi likiwamo hilo la kadi za simu. Walipendekeza tukate Sh1,450 kwa mwezi, lakini sisi Serikali tukashusha hadi Sh1,000 yaani kila mwananchi akatwe Sh33.3 kwa siku na mapato yatakayopatikana yatakwenda kuboresha miradi ya maji, umeme vijijini na barabara, alisema Dk Mgimwa.
====================================================================================================
My take: Ni serikali ya CCM pamoja na Wabunge wa CCM ambao walipiga kelele na kuipitisha bajeti kandamizi. Wabunge wa CHADEMA siku ya kupitisha bajeti walikuwa ARUSHA.
Sasa Makamba ana nia gani kusema haya ikiwa na yeye ni kiongozi wa CCM na anajua issue yote??
Au anawadanganya wananchi wake ili wamuone kuwa anawatetea???
Ni PM wa serikali ya CCM aliyeruhusu wananchi kupigwa na POLISI kama walivyotendewa Bumbuli:-
Je, Makamba hajui kuwa askari POLISI wamepewa rungu na Mh. PM kupiga tu kwani serikali ya January Makamba wameshachoka???
TAFAKARI KAMA uNA AKILI TIMAMU UTAELEWA.....
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!