Nyetk
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 1,648
- 1,696
Sote tunakubaliana kuwa madaktari wanayo madai ya msingi wanayotaka serikali iwatekelezee, ila kinachoanza kijikita sasa katika fikira zetu ni namna ya kudai haki zao na uhalali wa kila njia watakayotumia kudai haki hizo. Swali kubwa hapa ile Principle of double effect ina-aply namna gani katika hili au kuna kitu kinachokinga tusitumie fikra hii sahihi? Najaribu kutegua kitenawili hiki.
Miaka ya nyuma katika nchi yetu (kama ilivyo bado katika nchi nyingi duniani) sheria zetu zilizuia mwajiriwa kuanzisha na kumiliki biashara yenye ushindani na ile ya mwajiri wake. Mfano Mwalimu mwajiriwa asifungue shule binafsi inayofanana na ya mwajiri wake, muuza duka la spea asifungue la kwake kama hilo, daktari mwajiriwa asifungue biashara kam ya mwajiri wake, nk. Aliyetamani kufanya hivyo basi ilimbidi kwanza kuacha kazi ya kuajiriwa ndipo afungue shuguli kama ya mwajiri wake wa zamani. Sababu za sheria hii ziko wazi; kukwepa masahibu yanayotokana na mgongano wa maslahi.
Sheria hii iliondolewa bila tathmini ya kutosha na sasa waajiriwa wengi nchi hii wanamiliki biashara kama za waajiri wao. Mfano madaktari bingwa wa Muhimbili na Oshean Road akina Massawe, Marro, Mgaya, Lymo, Macha, Kamugisha....... wote wanamiliki kliniki/zahanati za kwao na sote ni mashahidi ya kinachoendelea. Serikali haijafanya tathmini kuona athari za uwajibikaji wa watumishi wake wanaomiliki miradi inayofanana ya ajira zao. Sasa hivi imeshapanda zaidi ya kupungua uwajibikaji. SASA NI HUJUMA YA WAZI MCHANA KWEUPEE!
Maswali ambayo watu hawajiulizi katika migomo hii ni kama haya:
1. Kwa nini mgomo wa madaktari umesimamiwa kidete zaidi na madaktari bingwa wa Muhimbili?
2. Kwa nini madaktari hawa wanakwepa sana muafaka na wako tayari kufukuzwa kazi na mwajiri wao?
3. Mnadhani wakati wa mgomo mabingwa hawa wanakuwa wamekaa majumbani kwao wanapulizwa na feni?
4. Nani atakubali afe kama kuna uwezekano wa kumwona daktari yuleyule mahali pengine?
Ungefanya tathmini ya mapato wanayoingiza madaktari binwa hawa kwenye kliniki zao wakati wa migomo kama hii hata wewe ungependa migomo iwe kila siku laiti ungekuwa mmoja wao!
Miaka ya nyuma katika nchi yetu (kama ilivyo bado katika nchi nyingi duniani) sheria zetu zilizuia mwajiriwa kuanzisha na kumiliki biashara yenye ushindani na ile ya mwajiri wake. Mfano Mwalimu mwajiriwa asifungue shule binafsi inayofanana na ya mwajiri wake, muuza duka la spea asifungue la kwake kama hilo, daktari mwajiriwa asifungue biashara kam ya mwajiri wake, nk. Aliyetamani kufanya hivyo basi ilimbidi kwanza kuacha kazi ya kuajiriwa ndipo afungue shuguli kama ya mwajiri wake wa zamani. Sababu za sheria hii ziko wazi; kukwepa masahibu yanayotokana na mgongano wa maslahi.
Sheria hii iliondolewa bila tathmini ya kutosha na sasa waajiriwa wengi nchi hii wanamiliki biashara kama za waajiri wao. Mfano madaktari bingwa wa Muhimbili na Oshean Road akina Massawe, Marro, Mgaya, Lymo, Macha, Kamugisha....... wote wanamiliki kliniki/zahanati za kwao na sote ni mashahidi ya kinachoendelea. Serikali haijafanya tathmini kuona athari za uwajibikaji wa watumishi wake wanaomiliki miradi inayofanana ya ajira zao. Sasa hivi imeshapanda zaidi ya kupungua uwajibikaji. SASA NI HUJUMA YA WAZI MCHANA KWEUPEE!
Maswali ambayo watu hawajiulizi katika migomo hii ni kama haya:
1. Kwa nini mgomo wa madaktari umesimamiwa kidete zaidi na madaktari bingwa wa Muhimbili?
2. Kwa nini madaktari hawa wanakwepa sana muafaka na wako tayari kufukuzwa kazi na mwajiri wao?
3. Mnadhani wakati wa mgomo mabingwa hawa wanakuwa wamekaa majumbani kwao wanapulizwa na feni?
4. Nani atakubali afe kama kuna uwezekano wa kumwona daktari yuleyule mahali pengine?
Ungefanya tathmini ya mapato wanayoingiza madaktari binwa hawa kwenye kliniki zao wakati wa migomo kama hii hata wewe ungependa migomo iwe kila siku laiti ungekuwa mmoja wao!