Zinedine
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 1,187
- 694
Mimi naomba nukuu ya makubaliano ya kwanza baina ya madaktari na Pinda nione kama kweli Pinda aliwaahidi kuwaachisha kazi Mponda na Nkya.. Pinda anadai hapakuwepo na makubaliano hayo haya ni madai mapya kabisa, sasa isiwe hadithi ile ile ya kwanza walianza na Posho, tuliposema sana wakageuza madai na kuwa mazingira ya kufanyia kazi, Pinda alipotaka kukutana nao wakajataa wakisema hawawezi kwenda Karimjee ila Pinda awafuate wao Starlight, Haya wakutane Jumamosi wakasema ni siku ya Ibada kwao watakutana naye Jumatatu, tukasema mbona huenda kazini Jumamosi na Jumapili wakasema ooh hapana wanasubiri wajumbe wengine kutoka Bara.. haya Leo tena tunazidi kukata masiku ingawa mazungumzo yangeweza kuendelea huku mgomo wao ukiwa palepale - hawataki hadi Mponda na Nkya wajiuzuru... yaani hii sinema ya hostage taking inanoga kweli kweli utampenda kati ya The good, The bad and The Ugly - chaguo lako!
Hii ni miongoni mwa posts zako chache sana ambayo sjailewa mkuu. Hujui kwamba Mizengo kwa sasa ndiye mrithi halali wa Makamba snr, aliyekuwa na uwezo wa kusema jambo flani leo na kesho tu atadai hakusema hvyo. Hata kama makubaliano yale yasingewekwa humu jf au kutangazwa na media mbali*2 bado huitaji Phd kujua nani alisimamia ukweli baina ya PM na Drs. Siye pinda huyu huyu aliyekaribia kulia issue ya Jairo hali ya kuwa ameshasaini yale mambo!