moondampwani
JF-Expert Member
- Dec 4, 2014
- 535
- 170
Kama kweli basi ni wahuni tu
Nijuavyo mimi waalimu na madaktari walishagoma zamani ila migomo
yao ipo mioyoni,kwa macho haya wanaonekana wapo kazini ila mioyoni wamegoma.
selikari inalijua hilo ndo maana ikaanzisha division five almaarufu kama BRN
kuna mtoto anapata division 4 ya point 48,na wazazi tunashangilia kama mazuzu.
kwamba watoto wetu wamefaulu.
Upande wa madaktari toka kuteswa kwa Dr Ulimboka
anayeenda hospitali za umma atanielewa ninachokisema hapo.
Hali ni mbaya kama huna mtu unayefahamiana naye,ua labda upate bahati
wakshtukie kuwa labda wewe ni mtu fulani miongoni mwa wenye mamlaka hapo utahudumiwa.
Binafsi naona walishagoma labda kama wameamua kuweka hadharani japonajua watashindwa
kama walivyoshindwa hapo kwanza walipojaribu.Raia ndo tujiandae kuumia zaidi
na matokeo ya hiyo migomo.Asante bima ya afya ya serikali angalau sasa wengi
wana pa kukimbilia.
Kwa andiko hili siwezi kuwalaumu,maana nao walisoma ili wahudumie familia zao
pale wanapokuta elimu zao haziwasaidii kutunza familia zao
wanatumia njia mbadala,ili kutufikishia ujumbe sisi raia tujifunze kufanya
maamuzi sahihi pindi tupatapo nafasi ya kuchagua viongozi wa kuliongoza taifa.
Kama katibu mkuu wa CWT bado ni yule yule Oluochi niliyemuona wakati wa bunge la katiba, naweza ku bet kuwa mgomo utashindwa kabla ya kuanza.
Chadema watakuwa wanahusika.
Mkuu tatizo kubwa la nchi yetu ni wananchi,maana ndo wanahongwa T-shirt na kofia khanga na vitenge na kuwekaTatizo hiyo migomo ya kimya kimya haiwasumbui watawala. Wanahangaika migomo ikiwa wazi. Si umeona mgomo wa made revamped ulivyowatesa!! Au ule mgomo wa Ulimboka ulivyowakimbiza juu chini!? Hii ya kimya kimya inawaumiza tu wananchi ambao hawajui hata haki zao.
Walimu wa shule za umma wamekuwa kwenye migomo siku zote, hii inadhihirishwa kwenye matokeo ya wanafunzi Wa shule za umma
Taarifa kutoka duru za walimu na madaktari zinadai kwamba watumishi hawa wa umma wapo mbioni kugoma ili kuishnikiza serikali ya CCM kuwalipa madai yao kama ilivyowaahidi miaka kadhaa iliyopita kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu:
MADAKTARI
Madaktari wanaidai serikali madai mbalimbali ikiwemo kuboresha maslahi yao na mazingira ya kufanyia kazi, kuwalipa oncall allowance na posho ya kufanyia kazi katika mazingira hatarishi, kuboresha huduma za hospitali (dawa, vitanda, vitendea kazi, nk), kuthamini taaluma ya udaktari, nk. Utaona kwamba madai yao yamejikita katika sehemu kuu mbili ambazo ni uboreshwaji wa mazingira ya kazi na vifaa vya tiba na uboreshwaji wa kipato, kinga na afya za madaktari (Mishahara, posho na Bima ya afya).
WALIMU
Walimu wanaidai serikali mabilioni ya shilingi ikiwemo posho, malimbikizo ya mishahara, kupandishwa vyeo, nk. Walimu ndio watumishi wa umma wanaolipwa fedha kidogo zaidi kuliko watumishi wote wa serikali; na pia kazi yao haithaminiwi hata kidogo na serikali ya CCM. Kumbuka siku za nyuma Waziri wa CCM, Bi Hawa Ghasia aliwahi kuwadhihaki kwamba kama hawataki kulipwa mishahara kidogo basi watafute kazi nyingine tofauti na ualimu kwa kuwa siku zote kada ya ualimu wataendelea kulipwa mishahara kidogo so long as ni wengi sana ukilinganisha na watumishi wengine wa serikali. Hivyo, kama serikali ikiwalipa vizuri, itafilisika!
WAFANYAKAZI WENGINE
Nao wafanyakazi wa kada zingine wanaoidai serikali mabilioni ya shilingi wanasubiri walimu na madaktari walibumbulie, nao waunge tela. Safari hii sioni namna ambavyo serikali itakavyoweza kuuzuia mgomo huu mtakatifu. Ni rahisi kuzuia mafuriko kwa mikono kuliko kuuzuia mgomo huu. Sisi yetu macho¡-wafanyakazi wa serikali wakilianzisha nasi wananchi tuunge tela. Bila kufanya hivyo, serikali hii ya CCM itaendelea kuchezea maisha ya watanzania mpaka kiyama. Tazama jinsi hospitali na shule za makabwela zilivyo taabani huku kila kukicha tunasikia mafisadi wa CCM wakikwapua mabilioni ya shilingi bila kuchukuliwa hatua zozote.
View attachment 254823View attachment 254824View attachment 254825View attachment 254826View attachment 254827
MAONI YANGU
Mimi naona kama mgomo huu umechelewa sana. Ulipaswa ufanyike mapema na maslahi yanelikwishaboreshwa kitambo sana. Wafanyakazi wan chi hii ndio itakuwa chachu ya mabadiliko. Sisi raia wa kawaida tunapaswa kuwaunga mkono wafanyakazi kwani kuboreshwa kwa maslahi yao kuna manufaa makubwa sana kwa wananchi wa kawaida. Aidha, madai yao yanajumuisha uboreshaji wa huduma za tiba kwa wananchi; na hapa kila mwananchi atanufaika kwani ubovu wa huduma katika hospitali na shule zetu unamuathiri kila raia mnyonge isipokuwa wale mafisadi wachache wasiotibiwa katika hospitali za umma na wasiosoma katika shule za walalahoi (shule za kata).
:israel:
Ni kweli huyu jamaa nina hakika yuko ile idara - tiss
Naona unaipigia chapuo chadema
mkuu rallphryder hebu jirudishie akili kidogo, utazame hizo picha jinsi wamama wanavyoteseka hospitalini huku CCM mkifisidi pesa za umma kila siku. hebu tazama jinsi huyo mjazito alivyobebwa kwenye ambulance ya toroli maskini! kuweni na huruma japo kidogo na ustawi wa wananchi kwani hao watoto wanaosomea chini ya miti ni binadamu na wanastahili kusomea katika mazingira bora. wewe unadhani mafisadi wa CCM wanavyokwapua fedha za umma na kuwaacha wananchi wakiteseka hivi ni sahihi mkuu?
Taarifa kutoka duru za walimu na madaktari zinadai kwamba watumishi hawa wa umma wapo mbioni kugoma ili kuishnikiza serikali ya CCM kuwalipa madai yao kama ilivyowaahidi miaka kadhaa iliyopita kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu:
MAONI YANGU
Mimi naona kama mgomo huu umechelewa sana. Ulipaswa ufanyike mapema na maslahi yanelikwishaboreshwa kitambo sana. Wafanyakazi wan chi hii ndio itakuwa chachu ya mabadiliko. Sisi raia wa kawaida tunapaswa kuwaunga mkono wafanyakazi kwani kuboreshwa kwa maslahi yao kuna manufaa makubwa sana kwa wananchi wa kawaida. Aidha, madai yao yanajumuisha uboreshaji wa huduma za tiba kwa wananchi; na hapa kila mwananchi atanufaika kwani ubovu wa huduma katika hospitali na shule zetu unamuathiri kila raia mnyonge isipokuwa wale mafisadi wachache wasiotibiwa katika hospitali za umma na wasiosoma katika shule za walalahoi (shule za kata).
:israel:
Hapo sasa ndio umenyoosha maelezo vizuri kwamba ni kweli umetumwa kuratibu mgomo. Ila umechelewa, wananchi wanajua janja zenu chadema, na watawapa discipline ndani ya balot box.