Mgomo mkubwa wanukia nchini

Mgomo mkubwa wanukia nchini

Nijuavyo mimi waalimu na madaktari walishagoma zamani ila migomo
yao ipo mioyoni,kwa macho haya wanaonekana wapo kazini ila mioyoni wamegoma.

selikari inalijua hilo ndo maana ikaanzisha division five almaarufu kama BRN
kuna mtoto anapata division 4 ya point 48,na wazazi tunashangilia kama mazuzu.
kwamba watoto wetu wamefaulu.

Upande wa madaktari toka kuteswa kwa Dr Ulimboka
anayeenda hospitali za umma atanielewa ninachokisema hapo.
Hali ni mbaya kama huna mtu unayefahamiana naye,ua labda upate bahati
wakshtukie kuwa labda wewe ni mtu fulani miongoni mwa wenye mamlaka hapo utahudumiwa.

Binafsi naona walishagoma labda kama wameamua kuweka hadharani japonajua watashindwa
kama walivyoshindwa hapo kwanza walipojaribu.Raia ndo tujiandae kuumia zaidi
na matokeo ya hiyo migomo.Asante bima ya afya ya serikali angalau sasa wengi
wana pa kukimbilia.

Kwa andiko hili siwezi kuwalaumu,maana nao walisoma ili wahudumie familia zao
pale wanapokuta elimu zao haziwasaidii kutunza familia zao
wanatumia njia mbadala,ili kutufikishia ujumbe sisi raia tujifunze kufanya
maamuzi sahihi pindi tupatapo nafasi ya kuchagua viongozi wa kuliongoza taifa.

Tatizo hiyo migomo ya kimya kimya haiwasumbui watawala. Wanahangaika migomo ikiwa wazi. Si umeona mgomo wa made revamped ulivyowatesa!! Au ule mgomo wa Ulimboka ulivyowakimbiza juu chini!? Hii ya kimya kimya inawaumiza tu wananchi ambao hawajui hata haki zao.
 
Kama katibu mkuu wa CWT bado ni yule yule Oluochi niliyemuona wakati wa bunge la katiba, naweza ku bet kuwa mgomo utashindwa kabla ya kuanza.

Ni kweli huyu jamaa nina hakika yuko ile idara - tiss
 
Tatizo hiyo migomo ya kimya kimya haiwasumbui watawala. Wanahangaika migomo ikiwa wazi. Si umeona mgomo wa made revamped ulivyowatesa!! Au ule mgomo wa Ulimboka ulivyowakimbiza juu chini!? Hii ya kimya kimya inawaumiza tu wananchi ambao hawajui hata haki zao.
Mkuu tatizo kubwa la nchi yetu ni wananchi,maana ndo wanahongwa T-shirt na kofia khanga na vitenge na kuweka
madarakani majanga badala ya viongozi,hivyo wananchi huenda wakiwa na hali ngumu akili itakaa sawa.

wananchi wanatakiwa kuitambua nguvu ya kura yao na waitumie ipasavyo.
ipo siku tutampata kiongozi sahihi.
 
Walimu wa shule za umma wamekuwa kwenye migomo siku zote, hii inadhihirishwa kwenye matokeo ya wanafunzi Wa shule za umma
 
Walimu hawawezi kugoma hata siku moja wanaingiza hela kwa siku kila mwalimu anaweza kuondoka shule na 20000 au zaidi hiyo ni posho ambazo wanazipata kwa kuwalazimisha watoto watoe ada za tuition
 
Walimu wa shule za umma wamekuwa kwenye migomo siku zote, hii inadhihirishwa kwenye matokeo ya wanafunzi Wa shule za umma

Mbona kila mwaka serikali inatuaminisha kwamba matokeo ni mazuri kwa kishindo...kwamba 95 ya wanafunzi hufaulu kuingia sekondari kila mwaka? Matokeo ni mazuri siku zote, hata kama yakiwa mabaya serikali itashusha GPA ili yakae vizuri. Unaona eeh?
 
walimu hawawez goma

kama ni kweli chadema wanahusika, basi wanastahili pongezi na wanafaa kuongoza nchi hii...tuwape kura zote oktoba watusaidie kurudisha maadili ya kitaifa yaliyopotezwa na CCM.
 
Taarifa kutoka duru za walimu na madaktari zinadai kwamba watumishi hawa wa umma wapo mbioni kugoma ili kuishnikiza serikali ya CCM kuwalipa madai yao kama ilivyowaahidi miaka kadhaa iliyopita kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu:

MADAKTARI
Madaktari wanaidai serikali madai mbalimbali ikiwemo kuboresha maslahi yao na mazingira ya kufanyia kazi, kuwalipa oncall allowance na posho ya kufanyia kazi katika mazingira hatarishi, kuboresha huduma za hospitali (dawa, vitanda, vitendea kazi, nk), kuthamini taaluma ya udaktari, nk. Utaona kwamba madai yao yamejikita katika sehemu kuu mbili ambazo ni uboreshwaji wa mazingira ya kazi na vifaa vya tiba na uboreshwaji wa kipato, kinga na afya za madaktari (Mishahara, posho na Bima ya afya).

WALIMU
Walimu wanaidai serikali mabilioni ya shilingi ikiwemo posho, malimbikizo ya mishahara, kupandishwa vyeo, nk. Walimu ndio watumishi wa umma wanaolipwa fedha kidogo zaidi kuliko watumishi wote wa serikali; na pia kazi yao haithaminiwi hata kidogo na serikali ya CCM. Kumbuka siku za nyuma Waziri wa CCM, Bi Hawa Ghasia aliwahi kuwadhihaki kwamba kama hawataki kulipwa mishahara kidogo basi watafute kazi nyingine tofauti na ualimu kwa kuwa siku zote kada ya ualimu wataendelea kulipwa mishahara kidogo so long as ni wengi sana ukilinganisha na watumishi wengine wa serikali. Hivyo, kama serikali ikiwalipa vizuri, itafilisika!


WAFANYAKAZI WENGINE
Nao wafanyakazi wa kada zingine wanaoidai serikali mabilioni ya shilingi wanasubiri walimu na madaktari walibumbulie, nao waunge tela. Safari hii sioni namna ambavyo serikali itakavyoweza kuuzuia mgomo huu mtakatifu. Ni rahisi kuzuia mafuriko kwa mikono kuliko kuuzuia mgomo huu. Sisi yetu macho¡-wafanyakazi wa serikali wakilianzisha nasi wananchi tuunge tela. Bila kufanya hivyo, serikali hii ya CCM itaendelea kuchezea maisha ya watanzania mpaka kiyama. Tazama jinsi hospitali na shule za makabwela zilivyo taabani huku kila kukicha tunasikia mafisadi wa CCM wakikwapua mabilioni ya shilingi bila kuchukuliwa hatua zozote.


View attachment 254823View attachment 254824View attachment 254825View attachment 254826View attachment 254827

MAONI YANGU
Mimi naona kama mgomo huu umechelewa sana. Ulipaswa ufanyike mapema na maslahi yanelikwishaboreshwa kitambo sana. Wafanyakazi wan chi hii ndio itakuwa chachu ya mabadiliko. Sisi raia wa kawaida tunapaswa kuwaunga mkono wafanyakazi kwani kuboreshwa kwa maslahi yao kuna manufaa makubwa sana kwa wananchi wa kawaida. Aidha, madai yao yanajumuisha uboreshaji wa huduma za tiba kwa wananchi; na hapa kila mwananchi atanufaika kwani ubovu wa huduma katika hospitali na shule zetu unamuathiri kila raia mnyonge isipokuwa wale mafisadi wachache wasiotibiwa katika hospitali za umma na wasiosoma katika shule za walalahoi (shule za kata).

:israel:

Chagadema nyie kazi yenu kuu ni kuratibu migomo kama mlivyotoa ahadi kwamba mtahakikisha nchi haitawaliki. Kwa habari hii, mmejidhihirisha wazi tena kijinga sana kwamba ndio mnaratibu civil disorder kwa kujinufaisha kisiasa. Lakini kumbukeni huu uratibu mnaofanya, wananchi wenye akili timamu wameshawabaini na wanawasubiri kwenye sanduku la kura. Unapoandaa mgomo tena kibaya zaidi unawaunganisha madaktari kwa kuweka vipicha vyenu vya uchochezi, unadhani nani hajui kuwa ndio mnaandaa migomo hiyo!! We kundi gani la wafanyakazi limewatuma mlisemee katika makundi haya? Yaani kwa habari hii chadema mmeumbuka bayana na kutambulika wazi kuwa ni wachochezi wa migogoro. We unadhani mtu akifiwa na mpendwa wake kwa mgomo ulioasisiwa na chadema unadhani atawachagua?! Hebu mjipange vizuri maana kila njia inawabana! Mmetumia wachungaji majukwaa ya siasa, baadhi ya mapadri akiwemo mgombea wenu wa urais, lakini bado mmeona nanga inapaa mnakuja humu jukwaani kuratibu migomo!! Shame on you chadema.
 
Ni kweli huyu jamaa nina hakika yuko ile idara - tiss

Kwani migomo ni sifa! Chadema mmechoka sana siasa, sasa mnatafuta shari kuratibu migomo, na kwa hili mmeshafeli kabala ya kuanza kwani tumewashtukia. Chama cha chadema ovyo kabisa!
 
mkuu rallphryder hebu jirudishie akili kidogo, utazame hizo picha jinsi wamama wanavyoteseka hospitalini huku CCM mkifisidi pesa za umma kila siku. hebu tazama jinsi huyo mjazito alivyobebwa kwenye ambulance ya toroli maskini! kuweni na huruma japo kidogo na ustawi wa wananchi kwani hao watoto wanaosomea chini ya miti ni binadamu na wanastahili kusomea katika mazingira bora. wewe unadhani mafisadi wa CCM wanavyokwapua fedha za umma na kuwaacha wananchi wakiteseka hivi ni sahihi mkuu?

SWALI LA KIZUSHI
Hivi ni kwanini kila hatua inayolenga kuboresha maslahi ya wananchi kwa ujumla mnaihusisha na CHADEMA? ina maana nyie CCM hampendi kuona wananchi wakiondokana kero za huduma mbovu za umma?
 
Last edited by a moderator:
mkuu rallphryder hebu jirudishie akili kidogo, utazame hizo picha jinsi wamama wanavyoteseka hospitalini huku CCM mkifisidi pesa za umma kila siku. hebu tazama jinsi huyo mjazito alivyobebwa kwenye ambulance ya toroli maskini! kuweni na huruma japo kidogo na ustawi wa wananchi kwani hao watoto wanaosomea chini ya miti ni binadamu na wanastahili kusomea katika mazingira bora. wewe unadhani mafisadi wa CCM wanavyokwapua fedha za umma na kuwaacha wananchi wakiteseka hivi ni sahihi mkuu?

Hapo sasa ndio umenyoosha maelezo vizuri kwamba ni kweli umetumwa kuratibu mgomo. Ila umechelewa, wananchi wanajua janja zenu chadema, na watawapa discipline ndani ya balot box.
 
Last edited by a moderator:
Taarifa kutoka duru za walimu na madaktari zinadai kwamba watumishi hawa wa umma wapo mbioni kugoma ili kuishnikiza serikali ya CCM kuwalipa madai yao kama ilivyowaahidi miaka kadhaa iliyopita kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu:


MAONI YANGU
Mimi naona kama mgomo huu umechelewa sana. Ulipaswa ufanyike mapema na maslahi yanelikwishaboreshwa kitambo sana. Wafanyakazi wan chi hii ndio itakuwa chachu ya mabadiliko. Sisi raia wa kawaida tunapaswa kuwaunga mkono wafanyakazi kwani kuboreshwa kwa maslahi yao kuna manufaa makubwa sana kwa wananchi wa kawaida. Aidha, madai yao yanajumuisha uboreshaji wa huduma za tiba kwa wananchi; na hapa kila mwananchi atanufaika kwani ubovu wa huduma katika hospitali na shule zetu unamuathiri kila raia mnyonge isipokuwa wale mafisadi wachache wasiotibiwa katika hospitali za umma na wasiosoma katika shule za walalahoi (shule za kata).

:israel:

Sio Tanzania niijuayo leo hii. Kila mtu anajali maslahi yake mwenyewe..
 
Hapo sasa ndio umenyoosha maelezo vizuri kwamba ni kweli umetumwa kuratibu mgomo. Ila umechelewa, wananchi wanajua janja zenu chadema, na watawapa discipline ndani ya balot box.

kwa hiyo nyie CCM zile fedha bilion 300 za ESCROW za wananchi mlizokwiba ndizo zitawafanya wananchi wawape kura kwa kishindo au ni hizi bilion 600 mlilizokwapua juzi? hebu nyoosha maelezo wananchi waelewe ili wawape kura za kishindo kwenye ballot box (sio BALOT box kama ulivyoandika weye!).
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom