Mgomo mkubwa wanukia Ijumaa

Mgomo mkubwa wanukia Ijumaa

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Taarifa za kiintelijensia nilizonazo ni kwamba madereva wa mabasi na malori wanatazamiwa kugoma nchi nzima kuanzia Ijumaa. Madereva hao wana malalamiko lukuki yakiwemo mikataba ya ajira,ubovu wa miundombinu,sheria kali za barabarani na nyinginezo.

Taarifa nilizonazo ni kuwa Madereva wa mabasi na malori nchi nzima watamaliza kufanya kazi zao Alhamisi. Watasubiri Ijumaa kujua hatma ya malalamiko yao. Ijumaa,madereva wote wa mikoa ya Dar na Pwani watakutana na ujumbe wa Serikali na wengineo Ubungo

Madereva wamewataka Mawaziri wanne:Sitta-Uchukuzi,Magufuli-Ujenzi na Kabaka-Ajira na Chikawe-Mambo ya Ndani wafike Ubungo saa moja asubuhi,siku ya Ijumaa tar 10 mwezi wa 4 kutoa majibu ya malalamiko ya madereva hao. Pamoja nao,wanatakiwa viongozi wa Polisi,TABOA,TAKUBOA na TBS.

Majibu yao yatazuia au kuchochea mgomo wa madereva wa mabasi na malori nchi nzima.

Mimi tu,kuwaletea habari!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Itafuata zamu yetu wakulima.Tutagoma kupeleka chakula sokoni ili nyie mafisadi wa mjini msipate chakula chetu.
Hivyo vyuo na mashule ya bweni mvitafutie chakula cha kichinachina
 
Nafikiri huu utakuwa mwanzo wa utungu . kuna mjamzito atajifungua muda si mrefu. CCM wajipime wenyewe nchi imewashinda kila nyanja.
 
Walimu wa nchi hii wanashindwa na madereva na makondakta ambao kila siku tunawabeza ni wanywa viroba huku Walimu wakilipa kisasi kwa wanafunzi kuwafundisha hovyo na kuwafelisha baadala ya kuikaba serikali elimu iwe bora na mishahara yao"!

Mathalani,kwa nini nyumba za NHC katikati ya miji wasipewe watumishi wa umma ie WAALIMU na MADAKTARI ili wawe karibu na vituo kazi na kuwapa nafuu ya maisha baadala ya wahindi ambao wanapack magari ya 100 million nje wakati wanaishi nyumba ya umma na wanaweza kujenga huku waalimu wakiadhrika??!!! Kwa nini walimu hawagomi??!! Ama ndio kuwa kada ya ualimu na upolisi zinaongoza kuwa na watu vihio ambao hawawazi nje ya box zaidi ya rushwa na kumkomoa mwananchi??!!

Naamini siku WAALIMU wakigoma nchi nzima mwezi mmoja basi shule zetu za kata zitaboreshwa sanjari na maslahi ya walimu,mgomo ni haki na haki haitolewi bure kwenye kisahani,ukipewa bure basi unahongwa kama sio kutongozwa ili utumike,kwa nchi zetu zenye watawala wapuuzi!!!!
 
Nilimsikia Mwenyekiti wa Madereva alilalamika sana kuhusu ajali ya MAFINGA akidai ajali ilisababishwa na shimo lililopo barabarani lakini hadi sasa aliyekamatwa ni dereva tu ambaye ni muhanga wa udhaifu wa Mwandisi wa eneo hilo na watu wengine wahusika na usalama wa barabara.

Pili, sheria zetu za nchi zinaruhusu magari yasiyozidi speed 80 lakini serikali ya CCM wenyewe wamenunua magari speed hadi 200 na wameacha wananchi wanunue magari speed 120, 180.

Hili suala la ajali linahitaji mjadala mpana kama ilivyo ugaidi
 
Huu mgomo umeshaanza muda mrefu wala si suala la tetesi. Hiyo Ijumaa ni kutekeleza hatua ya pili endapo serikali haitasikiliza madai yao. Hatua ya kwanza wameanza kwa kuendesha mabasi kulingana na alama za barabarani. Kwamba kama ni spidi 50 basi ni 50, kama ni spidi 30 basi ni 30. Na kwa upande fulani imeleta effect kubwa kwa wasafiri, mfano Dar - Iringa ilikuwa basi likitoka saa 12 asubuhi Ubungo linafika Iringa saa 7 mchana, ila kwa huu mgomo wao wanafika saa 11 jioni.
 
Sio kama mgomo ulishaanza hapana ni maelekezo ya seriKali kwamba mabasi yanatakiwa kuendeshwa kilomita 80 kwa saa(80km/hr) na atakakaye kiuka hilo atanyang'anywa leseni na aende kusoma upya.
 
Huu mgomo umeshaanza muda mrefu wala si suala la tetesi. Hiyo Ijumaa ni kutekeleza hatua ya pili endapo serikali haitasikiliza madai yao. Hatua ya kwanza wameanza kwa kuendesha mabasi kulingana na alama za barabarani. Kwamba kama ni spidi 50 basi ni 50, kama ni spidi 30 basi ni 30. Na kwa upande fulani imeleta effect kubwa kwa wasafiri, mfano Dar - Iringa ilikuwa basi likitoka saa 12 asubuhi Ubungo linafika Iringa saa 7 mchana, ila kwa huu mgomo wao wanafika saa 11 jioni.

Sio mgomo ni maagizo na amri iliyotolewa na sumatra wiki iliyopita mabasi yasitembee zaidi ya km 80/hr na yamepangiwa muda wa kufika. Kama hilo la Iringa huenda huo muda ndio wamepangiwa wawe wanaingia na wakiwahi zaidi basi adhabu ni kufungiwa. Huenda na amri hii nayo inachochea huo mgomo unaosemekana
 
Kumbe mabasi yanaweza kufika kwa mwendo kasi 80km/hr sasa hizo mbio za 140km/hr za nin? Onyo mwendokasi unaua
 
Walimu wa nchi hii wanashindwa na madereva na makondakta ambao kila siku tunawabeza ni wanywa viroba huku Walimu wakilipa kisasi kwa wanafunzi kuwafundisha hovyo na kuwafelisha baadala ya kuikaba serikali elimu iwe bora na mishahara yao"!

Mathalani,kwa nini nyumba za NHC katikati ya miji wasipewe watumishi wa umma ie WAALIMU na MADAKTARI ili wawe karibu na vituo kazi na kuwapa nafuu ya maisha baadala ya wahindi ambao wanapack magari ya 100 million nje wakati wanaishi nyumba ya umma na wanaweza kujenga huku waalimu wakiadhrika??!!! Kwa nini walimu hawagomi??!! Ama ndio kuwa kada ya ualimu na upolisi zinaongoza kuwa na watu vihio ambao hawawazi nje ya box zaidi ya rushwa na kumkomoa mwananchi??!!

Naamini siku WAALIMU wakigoma nchi nzima mwezi mmoja basi shule zetu za kata zitaboreshwa sanjari na maslahi ya walimu,mgomo ni haki na haki haitolewi bure kwenye kisahani,ukipewa bure basi unahongwa kama sio kutongozwa ili utumike,kwa nchi zetu zenye watawala wapuuzi!!!!

Madaktari waligoma hivi uliona nini kilimpata kiongozi wao? Na si ulisikia wananchi walivohamaki kugombana na madaktari?
Hata walimu wakigoma tutawazomea na kuungana na serikali dhalimu kuwaponda mawe walimu wetu!
Waache wafanye kazi Kwa kiwango cha malipo wanayopata!
 
Wasafiri wa mwanza, mbeya na songea wanaweza kulala njiani. Ikawa safari ya siku mbili
 
Huu mgomo umeshaanza muda mrefu wala si suala la tetesi. Hiyo Ijumaa ni kutekeleza hatua ya pili endapo serikali haitasikiliza madai yao. Hatua ya kwanza wameanza kwa kuendesha mabasi kulingana na alama za barabarani. Kwamba kama ni spidi 50 basi ni 50, kama ni spidi 30 basi ni 30. Na kwa upande fulani imeleta effect kubwa kwa wasafiri, mfano Dar - Iringa ilikuwa basi likitoka saa 12 asubuhi Ubungo linafika Iringa saa 7 mchana, ila kwa huu mgomo wao wanafika saa 11 jioni.

Kwa hili nawapongeza kwa kufuata sheria na alama za barabarani.
 
80km/hr kwa kilometa 600 ... lazima dereva asinzie.
 
Jana nilipokuwa kwenye daladala nilimsikia dereva mmoja akimwambia mwenzie juu ya Mgomo huu
 
Sheria zetu za nchi haziruhusu kuingizwa magari yanayozidi SPEED 80/km lakini nashangaa yameingia magari yanayozidi hizo speed, hivyo serikali yenyewe imeridhia
 
ijumaa siyo mgomo ni mkutano wa madereva wote na viongozi wa juu na idara zao za serikali. ila wasipofika hao tunaowahitaji kujibu hoja zetu na kuafikiana basi hapo ndo mgomo utakapoanzia
 
Back
Top Bottom