Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Ukiachilia mbali uwezo wa kusimamia / kutekeleza ahadi, kuna Wapiga kura wengi ambao wanamkubali Mgombea au Kiongozi kutokana na jinsi anavyowasilisha hoja!
Kwa vile anasema amezaliwa hapa JF- Kisiasa ngoja tuendelee kumfunda namna ya kujiwasilisha ipaswavyo!
Ufunguo:
Wakuu wote JF,
Mbadala: Ungeweza kuandika,
Ndg. Wana-JF au Wana- JF
- Kwanza ninaomba kwa unyenyekevu sana kuwashukuru Kamati Kuu ya CCM na Mwenyekiti wake Rais, Dr. Jakaya M. Kikwete kwa uamuzi wao mzito na wa pamoja wa kunipendekeza kugombea ubunge wa EAC, ninasema ninawashukuru sana kutoka moyoni mwangu kwa kunipa nafasi hiii.
I. Mwenyekiti ni sehemu ya Kamati Kuu hivyo kuanza kutamka Kamati Kuu na kisha kutumia kiunganishi na ni kujirudia. Pengine ulitaka kutumia maneno hususan, Mwenyekiti (lakini lazima uelewe kuwa hiyo ina maana kuwa yeye alikuwa na kura ya turufu au msukumo wake ndio ulikuwa mkubwa kuliko wa wengine; jambo ambalo halina mashiko mbele ya safari!).
Mbadala: Kitekinikali, ungeweza kuandika,
........ kumshukuru Mwenyekiti na Wajumbe (wake) wa Kamati Kuu......
II. Umetumia vitambulisho vya Wadhifa & Sifa ambavyo si sahihi katika mukhtadha huu wa Kikao cha Chama. Huna haja ya kumwita Rais hapo (ingawa kweli ni Rais), huna haja ya kumwita Dr. Na kama ni lazima, basi itifaki izingatiwe, uandike,. "Dr.h.c." au "Dr.(h.c.)"
- Ninawashukuru sana JF, wanachama wote hapa ndio nyumbani kwangu ndipo nilipokarabatiwa kisiasa na kufikia uwezo nilio nao sasa, I love JF this is my home politically nilizaliwa hapa,
Mbadala: Ungeweza kuandika,
Nawashukuru sana Wanachama wote wa JF maana hapa ndipo nimeendelea kukarabatiwa Kisiasa na pia katika nyanja mbalimbali. Hakika, JF imendelea kuchochea hisia na ndoto zangu za kuwa Mwanasiasa- Kiongozi bora.
NA KATIKA MIJADALA HAPA TUMEPITIA MENGI SANA NINAOMBA KUSEMA TENA NINAWAOMBA RADHI WOTE NILIOWAKOSEA KWA KUWARUSHIA MANENO YASIYOFAA KATIKA MIJADALA, .........NIA NA MADHUMUNI SIKU ZOTE NI TAIFA KWANZA.
Unaibua swali lisilo la lazima. Kwa nini uombe radhi leo (sasa). Ni bayana kuwa Binadamu hapendi kutoa msamaha katika mazingira yanayoashiria muda wa mwombaji kuhitaji kitu fulani toka kwake!
Mbadala: ungeweza kusema,
Hapa JF tunajadili hoja mbalimbali. Tuendelee kuwa wakweli na wawazi huku tukitumia lugha inayostahili kwa mujibu wa kanuni kuu za JF za ushiriki katika kutoa maoni yetu. Aidha tuendelee kuombana radhi pale tunapo sababisha usumbufu au maumivu kwa makusudi au pasipo kutarajia kwa mapungufu yetu ya kibinadamu. Siku zote, nia na madhumuni yawe kwanza, kuweka mbele Taifa letu, mengine yafuate.
SIWEZI KUSEMA NILIKUWA NIMELEWA KWA SABABU SIJAWAHI KUNYWA POMBE WALA KUVUTA SIGARA KATIKA MAISHA YANGU, KWA HIYO NINASEMA YALIKUWA NI MAPUNGUFU YANGU TU KAMA BIN-ADAAM, NINAOMBA MNISAMEHE SANA,
Swali lingine linaibuliwa tena, kwamba Je, ungekuwa unakunywa pombe, ungetumia hicho kama kisingizio? Zaidi ya yote sioni jinsi uvutaji wa sigara unahusiana (kisayansi) na matamshi au maandiko yasiyostahili, isipokuwa kama bila kujitambua ulikuwa unataka kutuelezea sifa (endapo ni sifa) zako kuwa wewe Mgombea, huywi pombe wala huvuti sigara.
Mbadala: Kutoyaadika haya maneno.
- AGAIN, jamani nawaomba twende mbele yaliyopita sio ndwele twende kwa mbele sasa tumalizie ngwe ya mwisho, JF idumu na MBARIKIWE WOTE NDUGU ZANGU!
Utata mwingine; ni yapi hayo yaliyopita yanayotakiwa kuachwa? Hapa kuna hoja kibao za siku za nyuma sana ambazo kamwe haziwezi kuachwa maana ama hazijajibiwa au hazijapata ufumbuzi kama vile matatizo ya Ufisadi nchini, Kero za Muungano wetu Tanzania, Hoja ya Mgombea Binafsi, Serikali kutakiwa kupunguza gharama kwa kuwa na Wizara, Mikoa / Wilaya, Wabunge wachache na uwezekano wa kuunganisha baadhi ya nyadhifa (Mikoani & Wilayani) n.k na JF is where people dare to talk openly! (kama unavyoamnini). Na ngwe ya mwisho ni ipi, je unamaanisha, uchaguzi wa nafasi unyogombea Bungeni au nini?
Mbadala: Ungeweza kuandika,
Ikiwa wewe ni mmoja wa wapiga kura au una ndugu / rafiki atakayekuwa mpiga kura katika ngwe iliyobakia Bungeni, ninayo heshima na taadhima kuwaombeni kura ili yumkini niweze kuwawakilisha ipaswavyo; ahadi ninayoitoa kwenu.
Pamoja na wengine wote, daima, tuzidi kuombeana yaliyo mema.
- MUCH RESPECT!:cool2:
William.
Hongera sana Willy, nakutakia kila la kheri. Hatuna haja ya kuanza kuogopa sijui kundi la nani n.k hiyo ni phobia tu, kitakacho kuinua ni uwezo wako ikiwa ni pamoja na jinsi unavyo jiwasilisha (presenting yourself) na huu ni mfano mmoja tu wa kukusaidia. Tafadhali uwe makini sana unapotaka kuongea kwenye kadamnasi.
Bado kitambo kidogo, pengine tutakuwa pamoja!:hand:
Kwa vile anasema amezaliwa hapa JF- Kisiasa ngoja tuendelee kumfunda namna ya kujiwasilisha ipaswavyo!
Ufunguo:
- § Maandishi ya Willy
- § Maandishi yangu
Wakuu wote JF,
Mbadala: Ungeweza kuandika,
Ndg. Wana-JF au Wana- JF
- Kwanza ninaomba kwa unyenyekevu sana kuwashukuru Kamati Kuu ya CCM na Mwenyekiti wake Rais, Dr. Jakaya M. Kikwete kwa uamuzi wao mzito na wa pamoja wa kunipendekeza kugombea ubunge wa EAC, ninasema ninawashukuru sana kutoka moyoni mwangu kwa kunipa nafasi hiii.
I. Mwenyekiti ni sehemu ya Kamati Kuu hivyo kuanza kutamka Kamati Kuu na kisha kutumia kiunganishi na ni kujirudia. Pengine ulitaka kutumia maneno hususan, Mwenyekiti (lakini lazima uelewe kuwa hiyo ina maana kuwa yeye alikuwa na kura ya turufu au msukumo wake ndio ulikuwa mkubwa kuliko wa wengine; jambo ambalo halina mashiko mbele ya safari!).
Mbadala: Kitekinikali, ungeweza kuandika,
........ kumshukuru Mwenyekiti na Wajumbe (wake) wa Kamati Kuu......
II. Umetumia vitambulisho vya Wadhifa & Sifa ambavyo si sahihi katika mukhtadha huu wa Kikao cha Chama. Huna haja ya kumwita Rais hapo (ingawa kweli ni Rais), huna haja ya kumwita Dr. Na kama ni lazima, basi itifaki izingatiwe, uandike,. "Dr.h.c." au "Dr.(h.c.)"
- Ninawashukuru sana JF, wanachama wote hapa ndio nyumbani kwangu ndipo nilipokarabatiwa kisiasa na kufikia uwezo nilio nao sasa, I love JF this is my home politically nilizaliwa hapa,
Mbadala: Ungeweza kuandika,
Nawashukuru sana Wanachama wote wa JF maana hapa ndipo nimeendelea kukarabatiwa Kisiasa na pia katika nyanja mbalimbali. Hakika, JF imendelea kuchochea hisia na ndoto zangu za kuwa Mwanasiasa- Kiongozi bora.
NA KATIKA MIJADALA HAPA TUMEPITIA MENGI SANA NINAOMBA KUSEMA TENA NINAWAOMBA RADHI WOTE NILIOWAKOSEA KWA KUWARUSHIA MANENO YASIYOFAA KATIKA MIJADALA, .........NIA NA MADHUMUNI SIKU ZOTE NI TAIFA KWANZA.
Unaibua swali lisilo la lazima. Kwa nini uombe radhi leo (sasa). Ni bayana kuwa Binadamu hapendi kutoa msamaha katika mazingira yanayoashiria muda wa mwombaji kuhitaji kitu fulani toka kwake!
Mbadala: ungeweza kusema,
Hapa JF tunajadili hoja mbalimbali. Tuendelee kuwa wakweli na wawazi huku tukitumia lugha inayostahili kwa mujibu wa kanuni kuu za JF za ushiriki katika kutoa maoni yetu. Aidha tuendelee kuombana radhi pale tunapo sababisha usumbufu au maumivu kwa makusudi au pasipo kutarajia kwa mapungufu yetu ya kibinadamu. Siku zote, nia na madhumuni yawe kwanza, kuweka mbele Taifa letu, mengine yafuate.
SIWEZI KUSEMA NILIKUWA NIMELEWA KWA SABABU SIJAWAHI KUNYWA POMBE WALA KUVUTA SIGARA KATIKA MAISHA YANGU, KWA HIYO NINASEMA YALIKUWA NI MAPUNGUFU YANGU TU KAMA BIN-ADAAM, NINAOMBA MNISAMEHE SANA,
Swali lingine linaibuliwa tena, kwamba Je, ungekuwa unakunywa pombe, ungetumia hicho kama kisingizio? Zaidi ya yote sioni jinsi uvutaji wa sigara unahusiana (kisayansi) na matamshi au maandiko yasiyostahili, isipokuwa kama bila kujitambua ulikuwa unataka kutuelezea sifa (endapo ni sifa) zako kuwa wewe Mgombea, huywi pombe wala huvuti sigara.
Mbadala: Kutoyaadika haya maneno.
- AGAIN, jamani nawaomba twende mbele yaliyopita sio ndwele twende kwa mbele sasa tumalizie ngwe ya mwisho, JF idumu na MBARIKIWE WOTE NDUGU ZANGU!
Utata mwingine; ni yapi hayo yaliyopita yanayotakiwa kuachwa? Hapa kuna hoja kibao za siku za nyuma sana ambazo kamwe haziwezi kuachwa maana ama hazijajibiwa au hazijapata ufumbuzi kama vile matatizo ya Ufisadi nchini, Kero za Muungano wetu Tanzania, Hoja ya Mgombea Binafsi, Serikali kutakiwa kupunguza gharama kwa kuwa na Wizara, Mikoa / Wilaya, Wabunge wachache na uwezekano wa kuunganisha baadhi ya nyadhifa (Mikoani & Wilayani) n.k na JF is where people dare to talk openly! (kama unavyoamnini). Na ngwe ya mwisho ni ipi, je unamaanisha, uchaguzi wa nafasi unyogombea Bungeni au nini?
Mbadala: Ungeweza kuandika,
Ikiwa wewe ni mmoja wa wapiga kura au una ndugu / rafiki atakayekuwa mpiga kura katika ngwe iliyobakia Bungeni, ninayo heshima na taadhima kuwaombeni kura ili yumkini niweze kuwawakilisha ipaswavyo; ahadi ninayoitoa kwenu.
Pamoja na wengine wote, daima, tuzidi kuombeana yaliyo mema.
- MUCH RESPECT!:cool2:
William.
Hongera sana Willy, nakutakia kila la kheri. Hatuna haja ya kuanza kuogopa sijui kundi la nani n.k hiyo ni phobia tu, kitakacho kuinua ni uwezo wako ikiwa ni pamoja na jinsi unavyo jiwasilisha (presenting yourself) na huu ni mfano mmoja tu wa kukusaidia. Tafadhali uwe makini sana unapotaka kuongea kwenye kadamnasi.
Bado kitambo kidogo, pengine tutakuwa pamoja!:hand: