sodoliki
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 2,593
- 2,016
ni Augustino Ramadhani, ni mkristo , kwa hiyo mgongano wa dini hakuna, ni mzazibari, kwa hiyo mgongano wa kupokezana kijiti Haupo, ni muadilifu , amestaafu kama hakimu na kwa uadilifu, Hana Kashfa za rushwa , na Hana Mzigo kwa jumuia , kama kuwa na vimadaMgombea urais kwa tiketi ya CCM 2015 ameishapatikana
Mgombea urais wa JMT kwa tiketi ya chama cha mapinduzi ambae atapeperusha bendera yachama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ameisha patikana, ila bado tukumshauri na kumwomba akubali kugombea, kazi hiyo inafanywa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wenye busara na ushauri wa kutosha.
Sifa zamgombea huyo:
- Anakubalika na vyama vyote,ataliunganisha taifa hili ambalo akina Lowassa wamelisambaratisha na makundi yao.
- Ni mweledi
- Hana makundi
- Hana harufu yoyote ya ufisadi
- Ni mcha mungu
- Anakubalika sehemu zote za JMT,Tanzania bara na visiwani, anakubalika na dini zote hata wapagani
- Ana uzoefu wa kutosha na kupitilizawa uongozi
- Hajawahi kuomba wala kupokea rushwatangu azaliwe
- Ni kiongozi wa mfano(role model) tokakatika familia yake hadi sehemu za kazi
- Anakubalika kimataifa
- Ni kiongozi safi ambae watu wanamkubali, ndege angani wanamkubali,hata wanyama polini tembo faru watakuwa salama ndani ya uongozi wake
Chama cha mapinduzi si chama cha wapumbafu kiasi ati wawachague sijui Membe, Sijui Sitta, Sijui Ngulu Nchemba, Sijui Wassira ambao tayari wana wakundi wapeperushe bendera yake, Chama Cha Mapinduzi kimefanya busara zake zote kumshauri mgombea mtarajiwa achukue form. Muelewe CCM mgombea wake huyo ameombwa agombee, siyo amejipigia debe kama wengine.
Tusubiri tuone
EE Mungu ibariki Tanzania, tuondokane na jinamizi hili.