Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,879
MGOMBEA urais kupitia Chama Cha Kijamii (CCK), David Mwaijojele, amesema iwapo wananchi watakipa ridhaa chama chake kushika madaraka, serikali yake itatunga sheria ambayo makahaba, wasagaji na mashoga watakuwa wanachapwa viboko 200 na kwenda jela miezi sita.
Aidha, alisema mafisadi, watakatishaji fedha na wanaotorosha fedha nje watapewa adhabu ya kwenda jela miaka 50 na kupigwa viboko 200 baada ya kuhukumiwa.
Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti hili jana, alisema suala la rushwa limekuwa tatizo sugu nchini, hivyo serikali yake itahakikisha linashughulikiwa ipasavyo ili liishe kabisa.
"Mwili wa mtu si wa kufanyia biashara kingono, makahaba, wasagaji na mashoga wanaitia aibu nchi. Naomba wananchi wanikabidhi nchi nitawanyoosha," alisema Mwaijojele.
Alisema mambo mengine ambayo serikali yake itayapa kipaumbele ni elimu, afya na kuboresha sekta ya kilimo ambayo asilimia kubwa ya Watanzania wanajishughulisha na kilimo kwa ajili ya kuendesha maisha yao.
Mgombea huyo alisema serikali yake pia itahakikisha vyombo vya habari vinakuwa huru zaidi ili kutekeleza majukumu yao vizuri ya kuhabarisha wananchi.
Kuhusu kampeni, alisema chama chake kimejipanga kufika katika mikoa na wilaya zote kwa kutumia fedha ambazo zinachangwa na wanachama na watu wenye mapenzi mema na chama hicho.
"Chama chetu hakina wabunge, hivyo hatupati ruzuku, kwa hiyo fedha za kampeni tutachangisha ndugu jamaa na marafiki, ili kufanikisha kampeni. Nawaomba wananchi waniunge mkono kuchangia chama chetu ili kiingie madarakani na kuwaletea maendeleo ya kweli," alisema.
Alisema maeneo ambayo yeye mgombea urais hatafika kutokana na hali ya uchumi, viongozi wa mikoa, wilaya, tarafa, kata, kijiji na vitongoji watamnadi kwenye mikutano yao ya kampeni.
Pia alisema chama hicho kinacho ilani ambayo kitaitumia kuinadi kwa wananchi ili kukichagua na kushika dola katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 28, mwaka huu.
"Uzuri chama changu kinao mtandao mkubwa wa wanachama na viongozi karibu katika kila mkoa na wilaya, nina imani watafanya kazi kubwa kukinadi chama," alisema.
NIPASHE
Aidha, alisema mafisadi, watakatishaji fedha na wanaotorosha fedha nje watapewa adhabu ya kwenda jela miaka 50 na kupigwa viboko 200 baada ya kuhukumiwa.
Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti hili jana, alisema suala la rushwa limekuwa tatizo sugu nchini, hivyo serikali yake itahakikisha linashughulikiwa ipasavyo ili liishe kabisa.
"Mwili wa mtu si wa kufanyia biashara kingono, makahaba, wasagaji na mashoga wanaitia aibu nchi. Naomba wananchi wanikabidhi nchi nitawanyoosha," alisema Mwaijojele.
Alisema mambo mengine ambayo serikali yake itayapa kipaumbele ni elimu, afya na kuboresha sekta ya kilimo ambayo asilimia kubwa ya Watanzania wanajishughulisha na kilimo kwa ajili ya kuendesha maisha yao.
Mgombea huyo alisema serikali yake pia itahakikisha vyombo vya habari vinakuwa huru zaidi ili kutekeleza majukumu yao vizuri ya kuhabarisha wananchi.
Kuhusu kampeni, alisema chama chake kimejipanga kufika katika mikoa na wilaya zote kwa kutumia fedha ambazo zinachangwa na wanachama na watu wenye mapenzi mema na chama hicho.
"Chama chetu hakina wabunge, hivyo hatupati ruzuku, kwa hiyo fedha za kampeni tutachangisha ndugu jamaa na marafiki, ili kufanikisha kampeni. Nawaomba wananchi waniunge mkono kuchangia chama chetu ili kiingie madarakani na kuwaletea maendeleo ya kweli," alisema.
Alisema maeneo ambayo yeye mgombea urais hatafika kutokana na hali ya uchumi, viongozi wa mikoa, wilaya, tarafa, kata, kijiji na vitongoji watamnadi kwenye mikutano yao ya kampeni.
Pia alisema chama hicho kinacho ilani ambayo kitaitumia kuinadi kwa wananchi ili kukichagua na kushika dola katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 28, mwaka huu.
"Uzuri chama changu kinao mtandao mkubwa wa wanachama na viongozi karibu katika kila mkoa na wilaya, nina imani watafanya kazi kubwa kukinadi chama," alisema.
NIPASHE