GE2025 Mgombea Udiwani kata ya Kariakoo Haji Manara akiomba kura ndani ya Daladala

GE2025 Mgombea Udiwani kata ya Kariakoo Haji Manara akiomba kura ndani ya Daladala

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
"Tunapita mtaa kwa mtaa, kijiwe kwa kijiwe, Namuombea kura Rais. Mimi nagombea Udiwani Kariakoo, watakaopiga kura Kariakoo naomba kura kwangu lakini muwachague wabunge wangu wa CCM na madiwani" Alisema Manara na kuongeza kuwa.

"Nimeingia kwenye hii daladala, Naomba kura. Na maana ya kupita nyumba kwa nyumba, daladala kwa daladala" Alisema Manara.

Je, kitendo cha Manara kuwalipia abiria nauli ni upendo kwa wapiga kura wake au ni rushwa?

Soma Pia:​

 
Unaomba kura wakati unagombea mwenyewe? Si hata kura yako 1 tayari ni 100% ya kura zote 1.
 
Hahaha sisi wa mbagala mambo ya kariakoo yanatuhusu nini?

Kura waombe wapiga kura wa kariakoo, sisi wa kuja asubuhi na kurudi jioni unatupigia kelele tu.
 
Back
Top Bottom