Mgombea atoa machozi

Robethn

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2015
Posts
2,103
Reaction score
354
IKULU KUNA NINI HADI MZEE ATOKWE NA MACHOZI!

MZEE WETU KASHINDWA KUJENGA HATA KIWANDA KIDOGO CHA KUSINDIKA MAZIWA JAPOKUWA ANAO NG`OMBE ZAIDI YA ELFU KUMI! HATARI!

Katika hali isiyo ya kawaida ni lazima tujiulize hiv Ikulu kuna nini?

Babu yetu hana uwezo wakuleta mabadiliko ndani ya nchii kwasababu ameshindwa kuwasaidia wananchi wake wa Monduli eneo linaloongoza kuwa na lidadi kubwa ya wafugaji na yeye mwenyewe kuwa na NG`OMBE ZAIDI YA ELFU KUMI, babu zaidi ya miaka 20 akiwa kiongozi kashindwa kuwajengea wafugaji hata kiwanda 1 cha maziwa ili kutoa uwezo kwa wanainchi husika kupata ajira na hatimaye kuinua kipato chao kila siku.

HALI AMBAYO NI TOFAUTI KABISA NA NYIMBO ZAKE ZA KILA SIKU ZA KUTENGENEZA AJIRA, Monduli kashindwa nchi nzima ndo ataweza kweli? Haaaa kweli ni nyimbo baadae zitakuwa ni NGONJERA.

Yawezekana ni ndoto za kuweza matumainikutengeneza ajira akiwa kazeeka kweli haya ndo maigizo yenyewe ya uzeeni!
F
ASITUFANYE WATOTO WADOGO WAKULISHWA UNGA WA NDELE NASEMA NOOOOOO. MZEE OUT

TAFAKARI,CHUKUA HATUA.
 
Kawafundisha wa kwao kutembea na mifugo toka Monduli hadi Kiteto hadi Mvomero.
Taabu sana huyu jamaa.
 
Wanainchi washajitambua hawawezi kumpatia uongozi mtu asiye na sifa.
 
Babu akaendeleze ufugaji, uongozi sio sahihi kwake.
 
Wasomi wanajitambua sana, hawawezi kubuluzwa na wanasiasa wasio na tija kwa taifa hili.
 
ahahahaaa hawezi hata jimbo lake limemshinda wanachi wake maishal magumu sana
 
Anasema uongo. Eti atafuta na kuondoa nyumba zote zenye paa la majani wakati Monduli ndio bingwa wa nyumba za nyasi. Lowassa acha sera za kusema uongo.

#HapaKaziTu
 
Prof Mark Mwandosya asema :

"Mwenyekiti alikuwa na majina yake mfukoni kutoka nyumbani kwake"

Mwl J.K Nyerere aliwakataza viongozi kushaurisna na wake zao na kufanya maamuzi yanayoathiri haki za wengi lakini Kikwete amefanya hivyo kule Dodoma na hata ktk masuala mengi ya taifa hili.

Kikwete ni mtu wa hila, ana roho ya inda na ni mzandiki.
Mzee Lowassa ni mtu makini, lakini Kikwete alipoona Lowassa anaikosoa serikali ya CCM, akamtuma Makonda amtukane. CCM hawajui kama Lowassa alikuwa anawatetea wananchi aliposema "viongozi wa serikali wanalalamika badala ya kutatua shida za wananchi, naomba viongozi wafanye maamuzi magumu; haiwezekani raia walalsmike na viongozi walalamike nani atatatua shida??

Lowassa alikuwa mchapakazi akashawishi maji ya ziwa Victoria yawanufaishe watanzania, akasukuma ujenzi wa shule za kata na mkakati wa chuo kikuu cha Dodoma.

Alipotaka kusitisha mkataba wa richmond ambao familia ya mkubwa ilikuwa na mkono wake akaambiwa "usithubutu hata kidogo" Watanzania kupitia Kikwete wakaingizwa mkenge kuwa ni Lowassa ndiye alishinikiza Richmond ipewe zabuni wakati hakuwepo hata katika kikao cha uteuzi wa mzabuni.

Lowassa akaendelea kusimamia haki akijua ipo siku atashika madaraka ya juu na kuuvunja mfumo mbovu ndani ya CCM hivyo kuleta mabadiliko na kurejesha haki.
Kikwete alipoona Lowassa anatakiwa na watu wengi kuwa Rais, akaamua kuizima hiyo ndoto akiwatumia vijana wake Nape, Makonda na Januari Makamba.
Profesa Mark Mwandosya anasema
'majina matano yaliyoletwa kamati kuu hayakupitia kamati ya maadili ila yalikuwa majina ya mwenyekiti kutoka mfukoni mwake''

Kwa mizengwe hiyo, haijalishi Magufuli alipitishwa na watu walionuia kumkomoa Kikwete, bado itakuwa ni kuendelea kuiunga mkono CCM na Kikwete na mizengwe yake ni kuendeleza mfumo mbovu.
Tatizo letu hatujui nini kilitokea Dodoma na tulikuja kusikia kesho yake tu kuwa Magufuli amepita tusijue mikiki mikiki iliyopelekea Magufuli kupita.

Mwandosya anasema mkutano ule ulipoa, hata mwenyekiti (Kikwete) alipoongea watu hawakumshangilia na hata Nape alipowataka wajumbe wamshangilie hawakufanya hivyo.

Maana yake nini? -> Lowassa kuondoka CCM ni kutafuta mabadiliko nje ya CCM ambayo bila shaka hayawezi kupatikana CCM kama alivyowahi kutabiri Nyerere. Hata Magufuli hawezi kuvunja mfumo huo na anatakiwa kumpigia kura Lowassa kama alivyokuwa amepanga kufanya alipoenda Dodoma kabla hajajua kama jina lake lingewekwa kama kiegesheo katika majina matatu ya Kikwete aliyoyajadili na mkewe.

Mwandosya anasema Magufuli hajawahi kuwa mwenyekiti wa CCM (W) hata kijiji wala kata atamudu vipi uenyekiti wa CCM taifa na kuvunja mfumo mbovu?
Maneno ya Prof huyu yanamaanisha kuwa kuna watu wengi wataendelea kuvaa nguo ya kijani ila watampigia kura Edward Lowassa.
 
Magufuli ndiye kituko zaidi ana taka apewe urais wakati hata tawi la CCM hajawahi kuongoza.
 
Anasema uongo. Eti atafuta na kuondoa nyumba zote zenye paa la majani wakati Monduli ndio bingwa wa nyumba za nyasi. Lowassa acha sera za kusema uongo.

#HapaKaziTu
kila siku mnalia hamna kazi halafu saivi mnajidai kazi tu
 

Attachments

  • 1441541780419.jpg
    28.6 KB · Views: 430
Heeee kama monduli kumejaa wafugaji na nyumba zenye mapaa ya manyasi kashindwa kuwasaidia kashindwa kuwajengea hata kiwanda aende akafuge tu
 
Hata Baba wa TAIFA alisema ikulu ni mahali patakatifu na sio sehemu ya kujipatia mali.
 
Huyo mzee kachoka uzeeni ndo anaweza kuleta ajira kweli, hizi ni nyimbo.
 
lowasa juuu zaidi....nimesema sirudi tena ccm kura yangu ni kwa lowasa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…